Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 2/90 uku. 2
  • Mikutano Inayotusaidia Kufanya Wanafunzi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mikutano Inayotusaidia Kufanya Wanafunzi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1990
  • Vichwa vidogo
  • JUMA LINALOANZA FEBRUARI 5
  • JUMA LINALOANZA FEBRUARI 12
  • JUMA LINALOANZA FEBRUARI 19
  • JUMA LINALOANZA FEBRUARI 26
Huduma Yetu ya Ufalme—1990
km 2/90 uku. 2

Mikutano Inayotusaidia Kufanya Wanafunzi

JUMA LINALOANZA FEBRUARI 5

Wimbo 180

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Panga sasa kufanya upainia msaidizi katika Aprili. Agizeni magazeti ya ziada mtakayohitaji kwa ajili ya Aprili na Mei. Lijulishe kundi ni vitabu gani vya zamani kidogo vinavyopatikana, au tia moyo matumizi ya kitabu Usalama Ulimwenguni Pote kuwa badala.

Dak. 20: “Wafanya Kazi Stadi Wanaotumia Neno la Mungu Sawasawa.” Izungumzwe kwa maswali na majibu. Someni mitajo ya maandiko kwa kadiri wakati unavyoruhusu. Kazia kwamba kwanza kabisa sisi ni wahudumu. Jaribu kuwa stadi katika kutumia Biblia. Usiridhike na kuangusha fasihi tu. Mwangalizi wa Shule au wa utumishi atoa wonyesho wa kumsaidia mhubiri mpya azoeleane na sehemu za New World Translation (Chapa ya 1984).

Dak. 15: Sanduku la Swali. Hotuba ikitolewa na mzee. Onyesha kwa busara lakini kwa umahususi matumizi ya shauri kuhusu hali ya kwenu kama inavyohitajiwa. Waweza kuwaingiza wasikilizaji kwenye mazungumzo.

Wimbo 190 na sala ya kumalizia.

JUMA LINALOANZA FEBRUARI 12

Wimbo 85

Dak. 10: Matangazo ya kwenu na Matangazo yaliyochaguliwa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu. Watie moyo wote watoke nje katika utumishi wa shambani mwisho-juma huu. Pitia makala katika magazeti ya karibuni ambazo zaweza kutumiwa kwa matokeo katika eneo lenu. Ripoti ya hesabu. Soma shukrani za Sosaiti kwa ajili ya michango zilizopokewa katika Januari. Wasifu akina ndugu kwa ajili ya michango ya kutegemeza kundi la mahali penu.

Dak. 15: “Magazeti Maarufu Yatokezwa.” Hotuba na mazungumzo ya habari pamoja na maswali kadhaa. Tia ndani mambo machache yaliyoonwa mahali penu ya wahubiri wakiangusha magazeti katika kazi ya barabarani, ushahidi wa vivi hivi, au katika kawaida ya kuwapelekea watu magazeti.

Dak. 20: Madokezo Yenye Manufaa kwa Ajili ya Kuangusha Magazeti. Zungumzeni madokezo yafuatayo na upate maelezo ya wahubiri juu ya mafanikio waliyoyaonea shangwe katika kuyatumia: (1) Soma magazeti na upate kujua vizuri makala. (2) Chagua makala zitakazoipendeza jumuiya kipekee. (3) Jaribu kutoa ushahidi wa jioni kwa magazeti. (4) Sema juu ya habari moja tu, na kukazia gazeti moja tu, ukitoa lile jingine kama mwenzi. (5) Sema polepole na kwa uwazi ukiwa na sauti ya kirafiki. Watie moyo wote wajaribu madokezo hayo yenye manufaa wanapotafuta kuangusha magazeti katika eneo lenu.

Wimbo 6 na sala ya kumalizia.

JUMA LINALOANZA FEBRUARI 19

Wimbo 207

Dak. 8: Matangazo ya kwenu, kutia ndani mipango kwa ajili ya utumishi wa shambani wa mwisho-juma. Habari za Kitheokrasi.

Dak. 7: Manufaa za Funzo la Jamaa la Biblia la Kawaida. Hotuba. Kwa miongo mingi tengenezo la Yehova limetia moyo vichwa vya jamaa viongoze funzo la Biblia na washiriki wa jamaa. Ambako hilo limefanywa, manufaa zimekuwa nyingi. Funzo hilo limechangiza roho ya upendo na amani ndani ya kizio cha jamaa. Watoto wamefanya maendeleo kufikia kuwa watumishi wa Yehova walio wakfu, wamekuwa na uvutano chanya juu ya kundi la mahali, na pindi nyingi wameingia katika utumishi wa wakati wote. Jambo hilo limeleta shangwe kubwa kwa wazazi Wakristo na wengine ambao wametazama maendeleo yaliyofanywa.

Dak. 17: Kufikia Mioyo ya Vijana. Kwa ufupi mzee azungumza mambo makuu kutoka vichapo vilivyotayarishwa hasa ili kusaidia vijana. Kuongezea funzo la jamaa la kawaida, washiriki wa jamaa wanafaidika na mazungumzo ya kiroho kulingana na pindi zinazotokea. Toa wonyesho wa mazungumzo ya jamaa ambayo baba ana uhusiano mchangamfu pamoja na watoto. Mazungumzo yao ni mbadilishano wa maelezo usio rasmi, si kipindi cha maswali na majibu. Mtoto mmoja katika jamaa ameuliza kama aweza kucheza mpira na watoto wa jirani. Kuza habari kwenye kurasa 64-7 za kitabu Young People Ask au Amkeni! 4/83 kur. 15-17. Mzazi auliza maswali ya kuchunguza ili aone kama mtoto anaelewa na kukubaliana na kanuni za Kimaandiko zinazohusika. Kazia kwamba marafiki wa karibu si lazima wawe wa umri ule ule. Chagua vijana ambao wamesoma visehemu vya kitabu, na uombe maoni yao. Waongoze wataje ni kwa nini habari hiyo ni yenye kusaidia. Watie moyo vijana wasome kitabu, na ukazie uhitaji wa wazazi kuzoeleana na yaliyomo ili watie mambo makuu yanayofaa katika mazungumzo ya jamaa.

Dak. 13: Mzee ahoji wazazi ambao wamefanikiwa au wanapata mafanikio kulea watoto katika ukweli. Kazia shangwe iliyopokewa na mambo ambayo wameona kuwa yenye msaada katika kuwa na funzo na mazungumzo ya jamaa ya kawaida yenye kujawa na maana. Wasihi kwa moyo mchangamfu wazazi waongoze funzo la jamaa kwa ukawaida nao vijana waunge mkono. Sikuzote mastakimu hazitafaa. Wote katika jamaa wanahitaji kufanya kazi pamoja. Kwa kufanya hivyo, wanaweza kusaidiana kukaa kwenye njia inayoenda kwenye uhai.—1 Tim. 4:16.

Wimbo 123 na sala ya kumalizia.

JUMA LINALOANZA FEBRUARI 26

Wimbo 172

Dak. 5: Matangazo ya kwenu. Watie moyo wote wajipatie ugavi wa kutosha wa kitabu God’s Word na washiriki kikamili katika kutoa kitabu hicho kipya katika utumishi wa shambani mwisho-juma huu.

Dak. 22: “Kutangaza Habari Njema—Tukiwa na Kitabu God’s Word.” Maswali na majibu. Kuhusiana na fungu 4, mhubiri mwenye ujuzi atoe wonyesho wa utoaji katika utendaji wa mlango kwa mlango. Kazia jinsi ya kusababu na mwenye nyumba, kwa kutumia mafungu 2 na 4 katika sura 1. Mnapozungumza fungu 5 la makala, painia atoe wonyesho wa matumizi ya fungu la utangulizi kwenye ukurasa 5 kwa ajili ya kutoa kitabu hiki katika eneo la biashara au kazi ya barabarani mahali inapofaa.

Dak. 18: “Kuonyesha Tegemeo Katika Yehova kwa Kupainia.” Mazungumzo ya shauku na uchangamfu yakiongozwa na mwangalizi wa utumishi. Hoji painia mmoja au wawili, ukikazia shangwe walizopokea kwa kadiri magumu yalivyoshindwa. Simulia mambo yanayofanywa mahali penu katika kutoa msaada wenye manufaa kwa mapainia.

Wimbo 14 na sala ya kumalizia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki