Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 5/90 uku. 4
  • Kutangaza Habari Njema Kupitia Mafunzo ya Biblia

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kutangaza Habari Njema Kupitia Mafunzo ya Biblia
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1990
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • FURSA NYINGI
  • TUMIA UFAHAMU
  • Anza Mafunzo ya Biblia—Sasa Ndio Wakati Unaofaa
    Huduma Yetu ya Ufalme—1988
  • Je! Wewe Unathamini Fasihi Yetu?
    Huduma Yetu ya Ufalme—1992
  • Kuanzisha Mafunzo ya Biblia Nyumbani
    Huduma Yetu ya Ufalme—1993
  • Je! Unatoa Mafunzo ya Biblia?
    Huduma Yetu ya Ufalme—1992
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1990
km 5/90 uku. 4

Kutangaza Habari Njema Kupitia Mafunzo ya Biblia

1 Mwaka huu wa utumishi uliopita katika Afrika ya Mashariki, mafunzo ya Biblia zaidi ya 18,000 yaliongozwa kila mwezi. Labda nusu ya wahubiri 12,500 katika eneo hili walishiriki kadiri fulani katika utendaji huu wenye shangwe. Bila shaka, ikiwa karibu nusu ya wahubiri walishiriki katika utendaji huu, ingemaanisha kwamba ile nusu nyingine haikuushiriki. Wengi wetu zaidi wawezaje kuonea shangwe uradhi maalumu unaotokana na kufundisha mtu mwingine ukweli?

2 Kwa sababu twampenda Mungu na jirani, twataka kushiriki ukweli pamoja na wengine. Lakini twahitaji msaada kutoka kwa Yehova katika huduma yetu. (1 Kor. 3:6, 7) Kwa hiyo, je! isingekuwa vizuri kufikia Yehova katika sala na kumwomba atusaidie tuanzishe funzo la Biblia la nyumbani? (1 Yn. 5:14, 15) Kisha lazima tutende kwa kupatana na ombi letu na kushiriki katika huduma ya shambani kwa ukamili kwa kadiri ambayo mambo yetu yaruhusu, tukitoa funzo la Biblia la nyumbani popote fursa ijitokezapo.

FURSA NYINGI

3 Wakati wa miaka michache iliyopita, tumeangusha mamilioni ya vitabu, vijitabu, na broshua kwa watu katika eneo letu. Vitabu Kuishi Milele, Amani ya Kweli, na Kweli, miongoni mwa vingine, vyaweza kupatikana katika makao ya maelfu ya watu ambao si Mashahidi wa Yehova. Hilo lawakilisha shamba kubwa mno la fursa ya kuanzisha mafunzo ya Biblia mapya.

4 Mwenye nyumba atuarifupo kwamba anazoeleana na kazi yetu au kwamba tayari ana fasihi yetu, twapaswa kumwambia jinsi tunavyopendezwa na hilo. (Ona Reasoning, ukurasa 20.) Ikiwa ana kichapo, twaweza kudokeza kwa fadhili kwamba akilete na kuturuhusu tumwonyeshe sehemu fulani za kupendeza ambazo zingekuwa na manufaa kwake na kwa familia yake. Ikiwa itikio ni chanya, twaweza kutoa funzo la Biblia la nyumbani.

5 Namna nyingine ya yaliyotangulia ingekuwa kwa sisi kudiriki na kuuliza kama mwenye nyumba ana fasihi yetu. Hilo laweza kuwa lenye tokeo hasa katika eneo ambalo tumeangusha fasihi nyingi. Baada ya utangulizi wa kirafiki, tungeweza kusema kwamba kwa sababu ya ziara zetu nyingi, wengi wa majirani wetu wana baadhi ya fasihi zetu. Sisi twapendezwa kuona watu wakinufaika na habari hiyo iliyochapishwa. Kisha tungeweza kumwuliza mwenye nyumba kama ana yoyote ya fasihi zetu. Kama anayo, tungeweza kumwuliza kwa fadhili kama twaweza kuiona na kisha kujitolea kumwonyesha jinsi ya kujifunza hiyo. Wonyesho mfupi waweza kutokeza funzo la Biblia la nyumbani. Kama hana fasihi yetu, twaweza kutoa toleo la wakati huu au kumwuliza moja kwa moja kama familia yake ingependa kuwa na funzo la Biblia la nyumbani.

TUMIA UFAHAMU

6 Kwa kuwa watu wengi wana shughuli nyingi kikweli, hasa katika maeneo makubwa ya miji na wakati wa majira ya kupanda na kuvuna, ni hekima kuwa mwenye busara na kutokaa mno. Ukiona wapaswa kupunguza mafunzo ya ziara chache za kwanza kuwa nusu saa basi hilo laweza kufanywa. Funzo likiisha kuimarishwa na upendezi wa mwenye nyumba kusitawishwa, kipindi kirefu zaidi cha wakati chaweza kutumiwa kwa funzo. Bila shaka, wengine watataka kujifunza kwa kipindi kirefu zaidi tangu pale mwanzo. Madhumuni yangekuwa ni kufikia mahali ambapo funzo laongozwa kwa angalau saa moja kila juma.

7 Kuna wenye mfano wa kondoo katia shamba ambao wahitaji msaada wetu, na wengi wao wana fasihi zetu. Bila shaka, baadhi yao wanapiga kite na kuugua juu ya mambo yenye kuchukiza yanayofanywa duniani leo. (Eze. 9:4) Ni pendeleo letu si kugawanya tu fasihi juu ya Ufalme ambao utatatua ole za aina-binadamu bali pia kufikia wenye mioyo minyoofu kwa ukweli kupitia mafunzo ya Biblia.—Mt. 28:19, 20.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki