Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 5/91 uku. 2
  • Mikutano Inayotusiadia Kufanya Wanafunzi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mikutano Inayotusiadia Kufanya Wanafunzi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1991
  • Vichwa vidogo
  • JUMA LINALOANZA MEI 6
  • JUMA LINALOANZA MEI 13
  • JUMA LINALOANZA MEI 20
  • JUMA LINALOANZA MEI 27
Huduma Yetu ya Ufalme—1991
km 5/91 uku. 2

Mikutano Inayotusiadia Kufanya Wanafunzi

JUMA LINALOANZA MEI 6

Wimbo 63

Dak. 10: Matangazo ya kwenu na Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu. Eleza mipango ya utumishi wa shambani. Shiriki jambo moja au mawili yaliyoonwa juu ya maandikisho yaliyopatikana kufikia sasa.

Dak. 15: “Wageuze Watu Waliache Giza Waingie Nuruni.” Mazungumzo ya maswali na majibu. Katika fungu la 6, uwe na angalau mambo mawili yaliyoonwa na watu binafsi kutoka kwa wasikilizaji juu ya namna Mnara wa Mlinzi lilivyowanufaisha wao au familia zao.

Dak. 20: Kichwa Kipya cha Mazungumzo. Zungumza pamoja na wasikilizaji Kichwa cha Mazungumzo kipya. Pia, zungumzia mambo tofauti-tofauti ya kuzungumzia kutoka toleo la karibuni zaidi la Mnara wa Mlinzi. Watie moyo akina ndugu wafikirie watu ambao wameonyesha kupendezwa halisi katika fasihi na ambao huenda wakaonea shangwe kupokea uandikishaji. Uwe na mhubiri aliyejitayarisha vizuri afanye utoaji ufuatao. “Hujambo. Jina langu ni—. Ninakutembelea kifupi kwa sababu ningependa kukuuliza swali. Je! wewe wafikiri twaweza kutarajia kuondolewa dhiki na matatizo yaliyopo sasa ambayo sisi sote tunakabili? [Ruhusu jibu.] Ikiwa tutaamua kutokana na wakati uliopita, hakuna msingi mkubwa kwa tumaini. Lakini angalia unabii uliotolewa kwa ajili ya wakati wetu katika Luka 21. [Soma mistari 10, 11, 26.] Hali hizi zimekuwako tangu Vita ya Ulimwengu ya 1. Hata hivyo, hatuachwi bila tumaini. Hali izi hizi ambazo ni zenye kusumbua sana ainabinadamu hutoa ushuhuda kwamba karibuni Ufalme wa Mungu utasafisha dunia na kuleta baraka zenye kudumu. Ndivyo anavyoendelea kusema Yesu katika mistari 28 na 31. [Soma mistari.] Kwa hiyo hali hizi mbaya na zenye kuvunja moyo kwa kweli ni ushuhuda wa kwamba badiliko zuri ajabu litatukia karibuni. Je! hizo si habari njema? [Ruhusu jibu.] Makala hii katika Mnara wa Mlinzi [teua fungu au picha ifaayo] huonyesha baadhi ya mabadiliko ambayo yatatukia karibuni na jinsi wewe na familia yako mnavyoweza kuishi mkazifurahie. Kisha utoe uandikishaji. Malizia sehemu hii kwa kuwatia moyo wote watumie Kichwa kipya cha Mazungumzo.

Wimbo 192 na sala ya kumalizia.

JUMA LINALOANZA MEI 13

Wimbo 221

Dak. 8: Matangazo ya kwenu na ripoti ya hesabu. Tia ndani maelezo ya shukrani kwa upaji. Pongeza kundi kwa uchangamfu kwa utegemezo wao wa kifedha kwa masilahi ya Ufalme kwa kundi lenu na wa ulimwenguni pote pia.

Dak. 17: “Kutoa Habari Njema—Kwa Magazeti.” Mazungumzo ya maswali na majibu ya habari. Baada ya kuzungumzia fungu la 3, uwe na mhubiri aliyejitayarisha vizuri afanye utoaji wa magazeti mara tatu wa sekunde 30-60. Kila utoaji wapaswa uwe kwa mwenye nyumba aliye na hali tofauti. Mhubiri huyo apaswa aonyeshe kufahamiana na magazeti na kubadilikana katika kutumia mambo yanayofaana na hali za mwenye nyumba.

Dak. 20: “Kuzaa Tunda kwa Uvumilivu.” Hotuba ikitegemea habari katika kurasa 253-5 za Kitabu-Mwaka cha 1990. (Tumia tarakimu za karibuni zaidi) Wapongeze wahubiri kwa uchangamfu kwa ushiriki wa kundi lenu katika kutoa ushuhuda kwa ujasiri na kuzaa tunda yajapokuwa majaribu na hali zenye magumu.

Wimbo 65 na sala ya kumalizia.

JUMA LINALOANZA MEI 20

Wimbo 181

Dak. 5: Matangazo ya kwenu. Eleza mipango ya kutoa ushuhuda katika mwisho huu wa juma.

Dak. 15: “Kusaidia Wengine Tunapokuwa Katika Utumishi wa Shambani.” Hotuba, pamoja na ushiriki wa wasikilizaji. Hoji kifupi mhubiri ambaye ni mfano mzuri aeleze manufaa za kibinafsi alizopata kutokana na kufanya kazi pamoja na wengine katika utumishi wa shambani.

Dak. 10: Sanduku la Swali. Mazungumzo ya maswali na majibu. Kazia baraka zinazotokana na kufuata mapendekezo ya kitheokrasi.

Dak. 15: Mahitaji ya kwenu, au “Je! Wewe Ungali Mtumwa wa Mapokeo Yasiyo ya Kikristo? Maziko na Makesha.” Zungumza mafungu 44-55 katika mfululizo juu ya mapokeo uliochapwa katika Huduma ya Ufalme Yetu katika 1975. Tumia maswali yaliyochapwa kukazia mambo makuu.

Wimbo 115 na sala ya kumalizia.

JUMA LINALOANZA MEI 27

Wimbo 170

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ripoti za Kitheokrasi. Pitia toleo la Juni na jinsi linavyoweza kupatanishwa na Kichwa cha Mazungumzo, “Sasa Ndio Wakati wa Kumtafuta Mungu.” Maandiko yaliyodokezwa ni Isaya 55:6, 7 (Mungu wa kweli anaweza kupatikana) na Matendo 17:26, 27 (lazima mwanadamu amtafute Mungu sasa.). Huenda wengine wakataka kuendelea na Kichwa cha Mazungumzo “Kukombolewa Kutoka kwa Dhiki ya Ulimwengu,” hasa kuhusiana na lile toleo badala la kitabu Usalama Ulimwenguni Pote.

Dak. 20: “Tumia Biblia Katika Utumishi wa Shambani.” Mazungumzo ya maswali na majibu. Kuhusiana na fungu la 6, uwe na wonyesho mfupi wa kutoa toleo la Juni. Tumia andiko moja tu kutoka Kichwa cha Mazungumzo.

Dak. 15: “Jinsi Index Yaweza Kuinufaisha Familia.” Mazungumzo ya maswali na majibu. Wakati wa kuzungumza fungu la 2, uwe na wenzi wa ndoa wakionyesha matumizi ya Index, wakitaja vichwa vidogo tofauti-tofauti vya kupendeza chini ya kichwa kikuu “Ndoa.”

Wimbo 151 na sala ya kumalizia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki