Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 9/93 uku. 2
  • Mikutano Ya Utumishi Kwa Ajili Ya Septemba

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mikutano Ya Utumishi Kwa Ajili Ya Septemba
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1993
  • Vichwa vidogo
  • Juma Linaloanza Septemba 6
  • Juma Linaloanza Septemba 13
  • Juma Linaloanza Septemba 20
  • Juma Linaloanza Septemba 27
Huduma Yetu ya Ufalme—1993
km 9/93 uku. 2

Mikutano Ya Utumishi Kwa Ajili Ya Septemba

Juma Linaloanza Septemba 6

Wimbo 164

Dak. 10: Matangazo ya kwenu na Matangazo yaliyoteuliwa kutoka kwa Huduma ya Ufalme Yetu.

Dak. 20: Imarisha Watoto Wako kwa Ajili ya Shule. Hotuba pamoja na mahoji na onyesho. Vijana Wakristo leo hukabiliana na masuala ambayo wengi katika kutaniko hawawezi hata kuwazia. Hasa wazazi ni lazima wajue vema juu ya magumu hayo ili waimarishe watoto wao kukabiliana na majaribu ya ushikamanifu wa maadili. Hoji vijana watatu wa umri mbalimbali. Ni ipi baadhi ya mibano hususa ambayo lazima wakabili kila siku shuleni? Ni nini huwasaidia wadumishe uhusiano mzuri pamoja na Yehova? Panga kuwe wonyesho wa familia ikiangalia pamoja mafungu 2 na 3 kwenye ukurasa 11 wa broshua ya Shule. Watoto waeleza kwamba hudhihakiwa na kuhisi wametengwa na wengine kwa sababu ya kushikilia viwango vya kidili vya juu vya Biblia. Kichwa cha familia chawatia watoto moyo akionyesha kufurahishwa kwake na mfano wao na kuwakumbusha Yehova hupendezwa sana na mwenendo wao. (Mit. 27:11) Ndugu anayeshughulikia sehemu hii amalizia kwa kuwapongeza vijana katika kutaniko kwa kazi zao njema na kuwasihi wawasiliane na wazazi wao ili kwamba watiwe nguvu kiroho mwaka huu wote wa shule.

Dak. 15: “Kuwasaidia Wengine Watambue Hazina Iliyo Kuu.” Ipitiwe kwa maswali na majibu. Kumbusha kutaniko uhitaji wa kuwa na maoni yanayofaa wanapotaja michango ya vichapo vyetu. Mnapoangalia fungu la 4, kuwe na wonyesho wa mhubiri akimtolea mzazi kitabu Kuishi Milele.

Wimbo 108 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Septemba 13

Wimbo 112

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Tia ndani ripoti ya hesabu na shukrani za utoaji wa hiari. Pongeza kutaniko kwa utegemezaji wenye ukarimu wa mahitaji ya kwenu na pia kazi ya ulimwenguni pote ya Sosaiti.

Dak. 10: “Nufaisha Wengine kwa Kutumia Magazeti.” Hotuba pamoja na maonyesho. Kazia thamani ya kutumia kikamili magazeti ya karibuni na ya zamani. Kuwe na maonyesho mawili, moja la kutoa magazeti ya karibuni na moja la kuonyesha jinsi ya kutumia toleo la zamani ili kutimiza uhitaji hususa wa mwenye nyumba.

Dak. 15: “Ni nini Tutakalotimiza Wakati wa Mwaka Huu wa Utumishi?” Hotuba pamoja na mazungumzo na wasikilizaji. Ishughulikiwe na mwangalizi msimamizi. Pitia mwaka wa utumishi uliopita wa kutaniko na uwatie moyo wote wafanye mipango ya utendaji ulioongezwa wakati wa mwaka wa utumishi wa 1994.

Dak. 10: “Jifunzeni Vitabu Kuishi Milele na Umoja Katika Ibada.” Baada ya kupitia makala hii na wasikilizaji, kuwe na mhubiri aliyejitayarisha vizuri akitoa wonyesho wa jinsi ya kubadili funzo kutoka kitabu Mtu Mkuu Zaidi hadi kitabu Kuishi Milele.

Wimbo 17 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Septemba 20

Wimbo 100

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Kazia makala zilizo kwenye magazeti ya karibuni ambayo yaweza kutolewa juma hili katika utumishi wa shambani.

Dak. 20: “Saidia Watu Walio Mfano wa Kondoo Wajenge Juu ya Msingi Imara” Zungumza pamoja na wasikilizaji. Kazia uhitaji wa kutayarisha kwa ajili ya kila ziara ya kurudia. Panga mhubiri aliye na sifa za kustahili atoe wonyesho wa kufanya ziara ya kurudia kwa mtu aliyechukua kitabu Kuishi Milele wakati uliopita, akitumia habari iliyo kwenye fungu la 3 au la 5.

Dak. 15: “Kuanzisha Mafunzo ya Biblia Nyumbani.” Maswali na majibu. Baada ya fungu la 4, panga kuwe na wonyesho mchangamfu wa ziara ya kurudia ambayo katika hiyo ni Biblia tu inayotumiwa, lakini ukitegemea sehemu za kitabu Kuishi Milele au Kutoa Sababu, kama ilivyodokezwa.

Wimbo 84 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Septemba 27

Wimbo 109

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Habari za Kitheokrasi.

Dak. 20: Wapendwa Wetu Waliokufa Wako Wapi? Mazungumzo ya familia. Kutumia habari iliyoteuliwa kutoka kurasa 100-102 za kitabu Kutoa Sababu, kichwa cha familia aangalia juu ya kifo cha rafiki wa karibu sana wa familia. Akazia kuwasaidia watoto wake waelewe maoni ya Biblia. Awauliza maswali ili kuhakikisha kwamba wanaelewa kifo ni nini na waweza kujieleza wenyewe waziwazi kulingana na umri wao. Pia, awaonyesha jinsi wanavyoweza kutumia kitabu Kutoa Sababu kuwafariji wengine.

Dak. 15: Toa Magazeti Wakati wa Oktoba. Panga kuwe na maonyesho matatu, mmoja ukionyesha kutoa Mnara wa Mlinzi la karibuni, mmoja ukionyesha kutoa Amkeni! la karibuni, na mmoja ambao katika huo mwenye nyumba ni mwenye shughuli sana na akubali trakti. Baada ya kila wonyesho, changanua na wasikilizaji kwa nini utoaji huo ulikuwa wenye matokeo. Toa maandikisho ya magazeti hayo au kitabu Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu.

Wimbo 21 na sala ya kumalizia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki