Mikutano Ya Utumishi Kwa Septemba
Juma Linaloanza Septemba 5
Dak 10: Matangazo ya kwenu na Matangazo yafaayo kutoka Huduma ya Ufalme Yetu.
Dak 20: “Panua Hazina Yako ya Utumishi wa Ufalme.” Mwangalizi wa utumishi pamoja na mzee mwingine wazungumzia mambo makuu kwenye makala. Pitia utendaji wa kutaniko wa mwaka uliopita, ukitoa pongezi pamoja na madokezo ya kufanyia maendeleo. Kazia mradi wa kuongeza ushiriki wa wetu wa kibinafsi katika huduma.
Dak 15: “Sitawisha Kupendezwa Katika Kitabu Kuishi Milele.” Wahubiri watatu au wanne, kutia na kijana, wazungumzia makala na kisha wanakuwa na kipindi cha mazoezi. Wanaonyesha utoaji wa aina mbili au tatu kisha wazipitia, wakipeana madokezo yenye kutumika na pongezi.
Wimbo 32 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Septemba 12
Dak 7: Matangazo ya kwenu.
Dak 20: Mwenendo wa Kikristo Shuleni. Mazungumzo na mzee akiwa pamoja na matineja watatu au wanne. Shuleni, vijana wetu wanakabiliwa na misongo mbalimbali ya kuridhia heshima yao kwa kanuni za Biblia. Mingi yayo hutoka kwa utendaji usiohusiana moja kwa moja na ule wa darasani. Michezo, kupeana miadi, na vikusanyiko vya kijamii hutokeza hatari. Mzee azungumzia “Shughuli za Baada ya Masomo” pamoja na matineja, akitumia broshua Shule, kurasa 16-19. Vijana watoa maelezo kuonyesha wanakabili misongo ya kushiriki katika mambo haya na hivyo wathamini shauri lililotolewa.
Dak 18: “Hawajaacha Kutoa Ushahidi.” Maswali na majibu. Onyesha kwamba ingawa sisi sote hatuwezi kutumia kiasi sawa cha wakati kwenye huduma, twapaswa kuwa na shangwe na tujitahidi kuwa wenye nafsi yote.
Wimbo 60 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Septemba 19
Dak 10: Matangazo ya kwenu. Soma ripoti ya hesabu na shukrani zozote za upaji wa hiari.
Dak 15: “Tumia Vema Magazeti Yetu.” Mazungumzo ya maswali na majibu. Eleza kifupi mipango ya kutaniko ya kutoa ushahidi wa magazeti wa kila juma. Toa onyesho kwa madokezo ya fungu la 4. Tia moyo kila mhubiri awe na agizo hususa la magazeti.
Dak 20: “Kuanzisha Mafunzo ya Biblia na Kitabu Kuishi Milele.” Zungumza pamoja na wasikilizaji. Panga kuwe na maonyesho mawili ukitumia utoaji uliopendekezwa.
Wimbo 67 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Septemba 26
Dak 10: Matangazo ya kwenu. Karibisha wasikilizaji watoe maono mafupi juu ya kuangusha kitabu Kuishi Milele au kuanzisha mafunzo nacho.
Dak 15: Mahitaji ya kwenu. Au toa hotuba kwenye makala “Je! Vizuizi Hukuvunja Moyo?” kutoka kwa Mnara wa Mlinzi wa Septemba 1, 1994, kurasa 27-8.
Dak 20: Kutoa Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Wakati wa Oktoba. Magazeti yetu hutimiza sehemu kubwa katika kazi yetu ya kuhubiri ya ulimwenguni pote; hii imekuwa njia ambayo mamilioni wamesikia kweli kwa mara ya kwanza. Kazia umaana wa kuyatumia kwa kuendelea na kuyatoa kwenye mahubiri ya mlango kwa mlango hata kama fasihi nyinginezo zatolewa. Taja manufaa za Siku ya Magazeti ya kila juma. Zungumzia jinsi mahubiri ya barabarani na ushahidi wa duka kwa duka hufungua fursa nyingi za maangusho. Kumbusha akina ndugu waweke maandishi ya maangusho, wakiwa na mradi wa kuanzisha njia ya kupelekea watu magazeti kwa ukawaida. Eleza kwamba maandikisho yanapaswa kutolewa bila kuhukumu kimbele mwenye nyumba. Kazia umaana wa kujitayarisha vizuri kabla ya kuondoka. Panga kuwe na wahubiri watatu, mmoja wao awe kijana, wakitoa maonyesho mafupi ya utoaji wa magazeti.
Wimbo 76 na sala ya kumalizia.