Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 4/96 uku. 8
  • Tafuta Walio na Mwelekeo Ufaao

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Tafuta Walio na Mwelekeo Ufaao
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Habari Zinazolingana
  • Sema Kweli na Jirani Yako
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • “Imani Hufuata Jambo Lililosikiwa”
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Mnara wa Mlinzi na Amkeni!—Majarida ya Wakati Ufaao Yenye Kweli
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
  • Jitayarishe kwa Utendaji wa Magazeti Katika Aprili
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1996
km 4/96 uku. 8

Tafuta Walio na Mwelekeo Ufaao

1 Kusudi moja la kazi ya kuhubiri ni kupata wale walio na “mwelekeo ufaao kwa ajili ya uhai udumuo milele.” (Mdo. 13:48, NW) Ugawanyaji wa magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! umethibitika kuwa njia bora ya kutimiza jambo hili, kwa kuwa majarida yetu hufanya watu wawe macho kuhusu tumaini la Ufalme. Mwezi wa Aprili tutatoa magazeti hayo. Yatumainiwa kwamba, mahali ambapo kupendezwa kutapatikana, twaweza kuanzisha mafunzo mapya ya Biblia katika kitabu Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele. Haya ndiyo madokezo yanayoweza kuwa na matokeo kwako:

2 Unapotumia “Mnara wa Mlinzi,” Aprili 1, unaweza kukazia “Msifuni Mfalme wa Umilele!,” linalokazia hotuba ya watu wote ya mkusanyiko wa wilaya wa mwaka jana, na useme:

◼ “Watu wengi tunaoongea nao wanamwamini Mungu. Wengine wanaona ugumu wa kumwamini. Wewe wahisije? [Ruhusu itikio.] Tunazungukwa na uthibitisho wa kweli kwamba lazima kuwe kuna Mungu. [Soma Zaburi 104:24.] Tunapoona kamera au kompyuta, mara moja sisi hutambua kwamba lazima iwe ilitengenezwa na mfanyizaji mwenye akili. Je, lingekuwa jambo la kiakili kusema kwamba vitu vilivyo tata zaidi, kama vile dunia na sisi wanadamu, vilitokea tu?” Tumia fungu moja kutoka makala hiyo kuonyesha sababu isiyo na kasoro ya kuamini Mungu kisha utoe andikisho.

3 “Mnara wa Mlinzi” la Aprili 15 lakazia “Sababu Kwa Nini Ibada ya Kweli Hupokea Baraka ya Mungu.” Kabla ya kutoa gazeti hilo, unaweza kuuliza:

◼ “Kukiwa na mamia ya dini zilizopo ulimwenguni, je, wafikiri zote zaweza kukubaliwa na Mungu? [Ruhusu elezo.] Yesu alitabiri kwamba ijapokuwa madai ya watu wengi wa kidini, zile zisizofanya mapenzi ya Mungu zitakataliwa. [Soma Mathayo 7:21-23.] Ni muhimu tutambue dini ya kweli ambayo Yesu alifunza juu yayo.” Fungua kwenye kichwa “Ni Lazima Dini ya Kweli Itokeze Matunda Gani?,” kinachoanzia ukurasa wa 16, na uzungumze juu ya kielelezo kimoja ili kuonyesha jambo kuu.

4 Unapotoa habari kuu katika “Amkeni!” la Aprili 22, “Wakati Vita Havitakuwapo Tena,” unaweza kufikiria kusema hivi:

◼ “Katika karne hii kumekuwako na mamia ya vita, kutia ndani vita viwili vya ulimwengu. Hata hivyo kwa kawaida viongozi wote wa ulimwengu husema wanataka amani. Kila mtu nijuaye anasema vivyo hivyo. Ikiwa kila mtu anataka amani, kwa nini hawawezi kuipata? [Ruhusu itikio.] Unafikiri ni nini kinachohitajiwa ili tuone amani ya kweli duniani?” Baada ya itikio la mwenye nyumba, fungua kurasa 8 na 9 usome maandiko kama vile Zaburi 46:8, 9. Ukitumia picha na maandiko yaliyonukuliwa, onyesha jinsi Ufalme wa Mungu utakavyoleta amani ya ulimwenguni pote itakayodumu milele. Kisha uliza kama mwenye nyumba angependa kuwa na andikisho la magazeti hayo.

5 Ukipata wengi wanaosema kwamba wana shughuli, unaweza kujaribu huu:

◼ “Tunapendezwa kusaidia watu wanaoishi maisha zenye shughuli na ambao hupata wakati mchache wa kufikiria sehemu ya kiroho ya maisha. Majarida yetu, Mnara wa Mlinzi na Amkeni!, yamefanyizwa ili kuandaa habari fupi juu ya masuala ya maana yanayokuathiri na familia yako. Ningependa kukuachia nakala hizi uzisome.”

6 Hakikisha kumpa kila mtu fursa ya kuandikisha magazeti yetu. Kwa hakika watanufaika na kusoma Mnara wa Mlinzi na Amkeni!, ambayo huleta “habari njema ya mambo mema.”—Isa. 52:7.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki