Jitayarishe kwa Utendaji wa Magazeti Katika Aprili
Kama ilivyoandikwa kwenye 1996 Calendar, Mlo wa Jioni wa Bwana utaadhimishwa Aprili 2 mwaka huu. Tukitiwa moyo na pindi hii tukufu, acheni kila mmoja wetu ashiriki kwa bidii kugawanya magazeti Aprili yote. Kwa hakika, kwenye Jumamosi ya kwanza, Aprili 6, acheni kila mmoja wa Mashahidi wa Yehova katika Afrika Mashariki ambao sasa ni zaidi ya 21,000 washiriki katika kazi ya magazeti. Kila baraza la wazee latiwa moyo kuratibu utendaji wa magazeti wa aina mbalimbali kwa siku yote ili wengi iwezekanavyo waweze kushiriki katika siku hii ya pekee ya magazeti. Mipango yaweza kufanywa kwa ajili ya ushahidi wa barabarani kwenye vipindi tofauti-tofauti wakati wa siku na vilevile ushahidi wa kawaida wa nyumba kwa nyumba na duka kwa duka. Mikutano ya utumishi wa shambani yaweza kupangwa mahali na nyakati mbalimbali siku hiyo ili kuwezesha wote washiriki katika siku hii ya pekee ya utendaji wa magazeti.
Katika maeneo fulani tutakuwa na matoleo ya magazeti ya Aprili ya wakati ufaao ya kutumiwa katika utumishi wa shambani. Katika maeneo mengine unaweza kutumia matoleo yoyote yaliyopo kwa kuwa magazeti yetu yote yana chakula cha kiroho cha wakati ufaao.
Kwa kufuatia kampeni ya Aprili uliopita ya trakti Habari za Ufalme, Aprili huu wapaswa kuwa mwezi wenye kutokeza wa ugawanyaji wa magazeti. Sasa ndio wakati wa kufanya mipango. Wengi watataka kujiandikisha wawe mapainia-wasaidizi. Ingawa huo mwezi una miisho-juma minne pekee, kuna sikukuu kadhaa wakati wa mwezi huo na bila shaka, wengi wa watangazaji wetu wachanga hawatakuwa shuleni katika kipindi hiki. Hiyo ni fursa nzuri kama nini ya kushiriki katika utumishi wa painia-msaidizi au angalau kuongeza utumishi wako. Inatumainiwa kwamba makutaniko yaliyo na magazeti ya ziada yataweza kuyagawanya mwezi huo. Makutaniko jirani yapaswa kuwa chonjo ili kupata nakala za ziada kutoka makutaniko yaliyo na magazeti mengi. Acheni sisi sote tuwe “watendaji wa neno.” Kama ilivyotabiriwa kuhusu Mesiya kwenye Zaburi 69:9, na tuweze pia kusema: “Wivu wa nyumba yako umenila.”—Yak. 1:22; Yn. 2:17.