Mikutano Ya Utumishi Kwa Februari
Juma Linaloanza Februari 5
Dak 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu. Habari za Kitheokrasi.
Dak 15: “Kutangaza Kweli Kila Siku kwa Kumwiga Yesu.” Maswali na majibu. Soma fungu la 5.
Dak 20: “Ufunuo—Ufunguo wa Furaha ya Kweli.” Zungumzia utoaji mbalimbali uliodokezwa, na uwe na wonyesho mmoja wa kila kichapo kitolewacho.
Wimbo 14 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Februari 12
Dak 10: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu. Tangaza mipango ya utumishi wa shambani ya mwisho-juma.
Dak 15: “Jitayarishe kwa Utendaji wa Magazeti Katika Aprili.” Kazia thamani ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! katika kujulisha habari njema. Soma makala, na uonyeshe jambo ambalo kutaniko la kwenu litafanya ili kufanya mwezi wa Aprili kuwa mwezi wa pekee wa ugawanyaji wa magazeti. Shughulikia mipango ya Aprili 6.
Dak 20: Mahitaji ya kwenu. Waweza kupanga kushughulikia mambo makuu ya mkusanyiko wa wilaya, ziara ya mwisho ya mwangalizi wa mzunguko, mipango ya mchango na maazimio ya kutegemeza mradi wa ujenzi wa tawi au mambo haya yote yaliyo juu ikiwa hakuna mambo ya lazima yanayohitaji kushugulikiwa.
Wimbo 133 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Februari 19
Dak 10: Matangazo ya kwenu.
Dak 15: “Nufaika na Shule ya Huduma ya Kitheokrasi ya 1996—Sehemu ya 2.” Hotuba ya kutolewa na mwangalizi wa shule. Kazia uhitaji wa kusoma Neno la Mungu kila siku.
Dak 20: “Wasaidie Waelewe.” Pitia utoaji mbalimbali uliodokezwa kwa kufanya ziara za kurudia. Mzee azungumza na watangazaji wawili au watatu sehemu za kitabu Upeo wa Ufunuo na jinsi ziwezavyo kukaziwa. Toa wonyesho wa utoaji mmoja au mbili. Toa madokezo ya jinsi ya kusitawisha kupendezwa hadi funzo la Biblia liweze kuanzishwa katika kitabu Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele.
Wimbo 53 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Februari 26
Dak 10: Matangazo ya kwenu. “Programu Mpya ya Siku ya Kusanyiko la Pekee.” Ikiwa inajulikana, tangaza tarehe ya kusanyiko lifuatalo. Tia moyo wote wahudhurie.
Dak 15: Kutayarisha Utoaji Wenye Kuvutia. Mwangalizi wa utumishi au mzee mwingine azungumza na watangazaji wawili au watatu manufaa za kuwa na utoaji wa mlango kwa mlango unaokazia jambo linalovutia katika eneo lenu. Kwa mfano, habari za ripoti za kwenu kuhusu jitihada za karibuni za kuboresha hali ya maisha; matatizo yenye kuongezeka ya ndoa, watoto wenye utovu wa nidhamu, au magumu ya kupata kazi ya kuajiriwa; au habari zinazoonyesha kwa nini watu wanakuwa wenye shaka zaidi kuhusu masuluhisho ya binadamu. Taja baadhi ya habari za karibuni katika jamii yenu, na uzungumze jinsi zinavyoweza kutumiwa ili kuanzisha mazungumzo.
Dak 20: Kutoa Kitabu Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele Wakati wa Machi. Kazia baadhi ya sehemu zenye kupendeza za kitabu hiki zinazoweza kutumiwa ili kuanzisha mazungumzo. (1) Vuta uangalifu kwenye picha zenye kuvutia, kama zile ambazo zimeonyeshwa kwenye kurasa 4-5, 86, 124-125, 188-189. (2) Onyesha jinsi kila sura inavyomalizia kwa maswali ya pitio, na ueleze jinsi hayo yanavyoweza kutumiwa kuwa msingi wa utoaji. Mwenye nyumba aweza kuulizwa ikiwa angependa kujua majibu. Chagua baadhi ya maswali miongoni mwa yale yaliyoorodheshwa kwenye kurasa 11, 22, 61, 149. (3) Rejezea kwenye sanduku lililo kwenye ukurasa wa 102, na utoe madokezo ya kuonyesha jinsi “Baadhi ya Sehemu za Siku za Mwisho” ziwezavyo kutumiwa ili kuchochea kupendezwa. (4) Kazia jinsi kitabu hiki kimetayarishwa hasa ili kuongoza mafunzo yenye maendeleo. Sura zenyewe ni fupi, habari ni rahisi kueleweka, maandiko yenye nguvu yamenukuliwa, na maswali yenye kuchochea hukazia mambo makuu. Wahimize wote watoe kitabu hiki wakiwa na lengo la kuanzisha mafunzo.
Wimbo 151 na sala ya kumalizia.