Mikutano Ya Utumishi Kwa Februari
Juma Linaloanza Februari 3
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu.
Dak. 15: “Shiriki Kazi Ambayo Haitarudiwa Kamwe.” Maswali na majibu. Wakati ukiruhusu, tia ndani mambo makuu kutoka “Kufuliza Kulinda—Jinsi Gani?” kwenye kurasa 714-715 za kitabu Proclaimers.
Dak. 20: “Kutoa Habari Njema kwa Hisi ya Uharaka.” (Mafungu 1-5) Baada ya maelezo mafupi kuhusu fungu la 1, mwenye kuongoza azungumzia mafungu 2-5 akiwa na watangazaji wawili au watatu. Wanapitia mambo makuu ya utoaji mbalimbali uliodokezwa na kutoa maelezo juu ya sababu kwa nini huu na utoaji kama huo mbalimbali waweza kuwa na matokeo katika eneo la kwenu. Watangazaji wanakuwa na duru ya kujizoeza huo utoaji mbalimbali. Mwenye kuongoza atoa pongezi, adokeza njia za kuufanya uwe wenye matokeo zaidi. Kisha anauliza wasikilizaji njia ambazo mradi wa kuanzisha mafunzo unaweza kufikiwa. Anatoa mawazo mahususi ya jinsi ya kuanzisha funzo hatimaye katika kitabu Ujuzi.
Wimbo 34 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Februari 10
Dak. 5: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu.
Dak. 10: “Kutoa Habari Njema kwa Hisi ya Uharaka.” (Mafungu 6-8) Toa wonyesho wa utoaji mbalimbali katika mafungu 6-7. Kazia uhitaji wa kufanya ziara ya kurudia kupendezwa kunapoonyeshwa.
Dak. 30: “Wanatakwa—Mapainia-Wasaidizi 2,500.” Ipitiwe kwa maswali na majibu ikiongozwa na mwangalizi wa utumishi. Kazia sanduku lililo kwenye ukurasa wa 3. Pitia ratiba za mfano zilizo kwenye ukurasa wa 6. Kila mtangazaji aliyebatizwa anapaswa kuchunguza kwa uangalifu na kwa sala kama anaweza kujiandikisha kwa mwezi mmoja au zaidi. Watangazaji wasiobatizwa wanaweza kuongeza ushiriki wao katika huduma kwa kujiwekea mradi wao wenyewe wa saa kila mwezi.
Wimbo 43 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Februari 17
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Taja mambo ya kupendeza ya kuzungumzia katika magazeti ya karibuni yanayoweza kutumiwa katika utumishi juma hili.
Dak. 13: “Ukumbusho—Tukio la Umaana Mkubwa!” Maswali na majibu. Toa kitia-moyo cha kufanya mwezi mzima wa Machi uwe wa pekee kwa kufanya upainia msaidizi. Kazia matumizi ya mialiko ya Ukumbusho.
Dak. 22: Kuanzisha Mafunzo ya Biblia Nyumbani. Katika miezi ya karibuni, mamia ya maelfu ya vitabu vilivyojalidiwa yameangushwa. Hii huandaa msingi wa kuanzisha mafunzo zaidi ya Biblia nyumbani. Pitia yale yaliyotimizwa kwenu katika kuangusha vitabu na fasihi nyingine. Watie moyo watangazaji wafuatie kupendezwa kote. Panga uwe na watangazaji kadhaa wasimulie hususani jitihada inayohitajiwa upande wao ili kuanzisha mafunzo mapya ya Biblia nyumbani. Kazia kwamba sehemu muhimu ya utume wetu ni kufanya wanafunzi. (Mt. 28:19, 20) Hili laweza kufanywa kwa matokeo ikiwa tunajitahidi kutumia madokezo yaliyo katika nyongeza ya Huduma ya Ufalme Yetu ya Juni 1996.
Wimbo 47 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Februari 24
Dak. 18: Matangazo ya kwenu. Tangaza majina ya wote wanaofanya upainia msaidizi Machi. Eleza kwamba si kuchelewa mno kuleta ombi. Tia moyo wote washiriki kikamili katika utumishi wa shambani Jumamosi, Machi 1. Eleza mipango ya ziada inayofanywa kwenu kwa ajili ya mikutano ya utumishi wakati wa mwezi huo. Pitia kwa uangalifu Sanduku la Swali.
Dak. 12: “Vipi Jamaa Zako?” Mume na mke wazungumzia makala hii pamoja na kuamua jinsi ya kuwafikia jamaa wasioamini wakiwa na habari njema.—Ona Mnara wa Mlinzi, Februari 15, 1990, kurasa 25-27.
Dak. 15: Pitia Toleo la Fasihi la Machi—Siri ya Kupata Furaha ya Familia. Zungumza kifupi sababu zifanyazo mvunjiko wa familia katika jamii ya kisasa. (Ona Mnara wa Mlinzi, Oktoba 15, 1992, kurasa 4-7.) Pitia yaliyomo ya kitabu hicho, kwenye ukurasa wa 3. Alika wasikilizaji wachague sura ambazo zaweza kuandaa msingi wa utoaji. Taja sanduku la kufundisha lenye msaada linaloonekana mwishoni mwa kila sura. Panga uwe na mtangazaji mwenye uwezo atoe wonyesho wa jinsi ya kutoa hicho kitabu. Kumbusha wote wachukue nakala zao ili kutumia mwisho-juma huu.
Wimbo 48 na sala ya kumalizia.