Waangalizi Wanaoongoza—Mwangalizi wa Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
1 Mwangalizi wa Shule ya Huduma ya Kitheokrasi ni mzee wa kiroho ambaye hujitahidi katika kusema na kufundisha na ambaye hustahili heshima yetu na ushirikiano wetu. (1 Tim. 5:17) Madaraka yake ni yapi?
2 Yeye hutunza maktaba ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi kwenye Jumba la Ufalme. Yeye hupendezwa sana kuwatia moyo wote wanaostahili wajiandikishe katika shule. Yeye huhakikisha kwamba maandishi sahihi yanawekwa ili migawo ifanywe kwa utaratibu angalau majuma matatu kabla ya kila kipindi cha shule. Anahitaji kuwajua vizuri wote kutanikoni, akimfikiria kila mwanafunzi na uwezo wake. Ijapokuwa huenda ndugu mwingine akamsaidia katika kutayarisha ratiba ya shule, mwangalizi husimamia kibinafsi migawo kwa njia inayofaa.
3 Ili kufundisha shule kwa matokeo mazuri, mwangalizi lazima ajitayarishe kwa bidii kila juma, akijifunza kikamili habari iliyopangwa kuwa mgawo. Kufanya hivyo humwezesha kufanya kutaniko lichangamke kuhusu utaratibu wa masomo, kuchunguza kama habari iliyopangwa kuwa mgawo imeelezwa kwa usahihi, na kukazia mambo makuu yatakayotiwa ndani ya mapitio ya kuandika.
4 Baada ya hotuba ya kila mwanafunzi, mwangalizi atampongeza mwanafunzi na kueleza kwa nini sifa fulani ya usemi ilikuwa nzuri au kwa nini yahitaji kufanyiwa maendeleo. Wakati mtu yeyote anahitaji ufundishaji wa ziada kutayarisha migawo ya shule, mwangalizi au mtu aliyechagulia naye anaweza kutoa msaada wa kibinafsi.
5 Ili kunufaika kikamili na kazi ngumu ya mwangalizi wa Shule ya Huduma ya Kitheokrasi na washauri wowote wa ziada walio chini ya mwelekezo wake, twapaswa kuhudhuria shule kwa ukawaida. Pia twapaswa kutimiza migawo yetu na kutumia shauri tunalopokea na vilevile lile ambalo wanafunzi wengine wanapewa. Katika njia hii, tutafanya maendeleo hatua kwa hatua katika uwezo wetu wa kutoa habari za Ufalme hadharani na nyumba hadi nyumba.—Mdo. 20:20; 1 Tim. 4:13, 15.