Programu Mpya ya Siku ya Kusanyiko la Pekee
Programu ya siku ya kusanyiko la pekee inayoanza Septemba 1999 ina kichwa: “Kuchunguza Ndani ya Mambo Yenye Kina Kirefu ya Mungu.” (1 Kor. 2:10) Tutajifunza mambo gani yenye thamani?
Katika kutafuta ujuzi, watu wengi hawaburudishwi na yale wanayopata. Biblia hututia nguvu, kama tutakavyoonyeshwa na mwangalizi wa mzunguko katika sehemu yake yenye kichwa “Kuchunguza Neno la Mungu Huburudisha.” Msemaji mwenye kuzuru ataonyesha uhusiano uliopo kati ya kutafuta mambo yenye kina kirefu ya Mungu na kuhubiri habari njema anapojibu swali “Waionaje Kazi ya Kuhubiri Ufalme?”
Wazazi wanaweza kusaidiaje watoto wao wachunguze Neno la Mungu kwa kina kirefu? Madokezo yenye kusaidia yatatolewa katika sehemu “Kaza Kikiki Neno la Mungu Katika Watoto Wako.” Vijana Wakristo hupata uvutano mzuri kwa kushirikiana na watu wakomavu kiroho walio katika kutaniko. Vielelezo vya jinsi wanavyopata uvutano mzuri vitakaziwa katika sehemu “Vijana Wanaojifunza Kutokana na Watu Wenye Umri Mkubwa Zaidi.”
Kwa nini tutafute kwa bidii hazina za kiroho zilizofichika wakati huu? Yehova ni Mfunuaji wa siri. Msemaji mwenye kuzuru ataeleza yale ambayo Yehova amefunua katika nyakati za kale na katika nyakati zetu katika hotuba “Yehova Hufunua Mambo Yenye Kina Kirefu Hatua kwa Hatua.” Hiyo itaimarisha azimio letu la kuendelea “kuchunguza ndani ya mambo yenye kina kirefu ya Mungu.”
Panga sasa uhudhurie. Wale wanaotaka kuonyesha wakfu wao kwa Yehova kupitia ubatizo wapaswa kumjulisha mwangalizi-msimamizi haraka iwezekanavyo. Tamaa yetu kubwa ya kuchunguza kwa uangalifu Neno la Mungu itaimarishwa na yale tunayosikia. Kwa hiyo, usikose siku hiyo ya pekee yenye mafundisho ya kiroho!