Kujenga Uthamini kwa Ajili ya Vidio The Bible—Mankind’s Oldest Modern Book
Maswali yafuatayo yanakazia mambo ambayo huenda uliyaona ulipotazama vidio hiyo: (1) Ni mambo gani ya hakika yanayoonyesha Biblia kuwa kitabu kisicho na kifani? (2) Toa mfano wa jinsi ambavyo Biblia hata ingawa ni ya kale sana, inapatana na sayansi ya kisasa. (3) Tuna uhakika gani kwamba Biblia ya leo ni sawa na maandishi ya awali? (4) Ni jambo gani lenye kutokeza katika hati za kale za Biblia, nalo linakupa uhakika gani? (5) John Wycliffe, Johannes Gutenberg, William Tyndale, Mary Jones, na Charles Taze Russell walichangiaje kuenezwa kwa Neno la Mungu ulimwenguni? (6) Kanisa lilipingaje sana Biblia, lakini ni nini kilichoiwezesha kuokoka hadi siku yetu? (7) Tengenezo la Yehova limetafsiri na kutokeza Biblia kwa kadiri gani? (8) Shauri la Biblia limesaidiaje watu wakabiliane na matatizo ya kucheza kamari kusikodhibitiwa (1 Tim. 6:9, 10), kutengana na ukosefu wa uaminifu katika ndoa (1 Kor. 13:4, 5; Efe. 5:28-33), na kujishughulisha mno na mali za kimwili (Mt. 16:26)? (9) Kuna uthibitisho gani kwamba kutumia kanuni za Maandiko kwaweza kushinda uzalendo, ukabila, na chuki ya kijamii ulimwenguni? (10) Kujifunza yaliyomo katika Biblia kumekuletea furaha kubwa kwa njia gani? (11) Ni nani ambao unafikiri watanufaika na vidio hii, nawe utawatoleaje?