Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Julai 15
“Ikiwa tukio kama hili [lililo kwenye jalada] lingeripotiwa siku zetu, watu wengi wangelitilia shaka. Unaonaje? [Ngoja jibu. Kisha soma Marko 4:39.] Kuna uthibitisho gani kwamba miujiza iliyofanywa na Yesu ilikuwa ya kweli? Gazeti hili la Mnara wa Mlinzi linachunguza swali hilo.”
Amkeni! Julai 22
“Katika ulimwengu wa leo, wahalifu wanaendelea kuvumbua mbinu mpya za kulaghai watu ambao si chonjo. Je, jambo hilo linakuhangaisha? [Ngoja jibu.] Gazeti hili la Amkeni! linazungumzia hatua chache za kujihadhari zinazoweza kutusaidia tujilinde na ulaghai.” Soma Methali 22:3.
Mnara wa Mlinzi Ago. 1
“Kwa kuwa wanadamu wamegawanyika sana, wengine wanahisi kwamba njia pekee ya kufikia amani ya ulimwengu ni kuwa na serikali ya ulimwenguni pote. Je, unafikiri jambo hilo linawezekana? [Ngoja jibu. Kisha soma Danieli 2:44.] Gazeti hili linazungumzia kile ambacho Ufalme wa Mungu unatimiza sasa na jinsi utakavyoleta amani ulimwenguni pote hivi karibuni.”
Amkeni! Ago. 8
“Sisi sote huhuzunika tunaposikia watoto wakitumiwa vibaya. Labda umejiuliza, ‘Je, kweli Mungu anajali?’ [Ngoja jibu. Kisha soma Zaburi 72:12-14.] Makala hii inazungumzia jinsi Mungu anavyohisi kuhusu watoto na jinsi atakavyoleta suluhisho la daima kwa wale wote wanaoonewa.”