Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 7/05 uku. 2
  • Ratiba ya Mkutano wa Utumishi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ratiba ya Mkutano wa Utumishi
  • Huduma ya Ufalme—2005
  • Vichwa vidogo
  • Juma Linaloanza Julai 11
  • Juma Linaloanza Julai 18
  • Juma Linaloanza Julai 25
  • Juma Linaloanza Agosti 1
Huduma ya Ufalme—2005
km 7/05 uku. 2

Ratiba ya Mkutano wa Utumishi

Juma Linaloanza Julai 11

Wimbo 49

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka katika Huduma Yetu ya Ufalme. Tumia mapendekezo kwenye ukurasa wa 8 (ikiwa yanafaa eneo lenu) kuonyesha jinsi ya kutoa gazeti la Mnara wa Mlinzi la Juni 15 na Amkeni! la Juni 22. Mapendekezo mengine yanayofaa eneo lenu yanaweza kutumiwa. Katika kila onyesho, wahubiri waonyeshe njia tofauti za kumjibu mtu anayesema, “Nina Shughuli.”—Ona kitabu Kutoa Sababu, uku. 19-20.

Dak. 17: Kutoa Broshua Mwezi wa Julai na Agosti. Hotuba, kisha mazungumzo na wasikilizaji yakitegemea nyongeza. Eleza kwa ufupi jinsi ya kutumia nyongeza hiyo, ukikazia sanduku kwenye ukurasa wa 3, na utaje mambo makuu kutoka katika Huduma Yetu ya Ufalme ya Januari 2005, ukurasa wa 8. Zungumzia mapendekezo yanayofaa eneo lenu ya kutoa broshua kwenye ziara ya kwanza. Panga maonyesho mawili au matatu ya kutoa broshua. Angalau onyesho moja lifanywe na mhubiri kijana.

Dak. 18: “Kuwahubiria Watu Wengi Iwezekanavyo.”a Unapozungumzia fungu la 5, pitia mapendekezo ambayo yanafaa eneo lenu katika Huduma Yetu ya Ufalme ya Juni 2005, ukurasa wa 6.

Wimbo 88 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Julai 18

Wimbo 173

Dak. 10: Matangazo ya kwenu na Habari za Kitheokrasi. Zungumzia kwa ufupi gazeti la Mnara wa Mlinzi, la Agosti 15, 2000, ukurasa wa 32. Kazia faida za kufuata ratiba ya kusoma Biblia kila siku, hata wakati wa likizo na tunapokuwa mbali na nyumbani.

Dak. 15: “Kuongoza Mafunzo ya Biblia Yenye Maendeleo—Sehemu ya 11.”b Panga onyesho fupi la mwalimu na mhubiri mpya wakijitayarisha kufanya ziara ya kurudia. Wanazungumzia ziara ya kwanza na kuchagua habari inayofaa ambayo watazungumzia katika ziara ya kurudia. Wanatayarisha pia utangulizi rahisi na swali linaloweza kuuliza mwishoni mwa ziara hiyo. Wanamalizia onyesho wanapotaka kuanza kufanya mazoezi ya utangulizi waliotayarisha.

Dak. 20: Wasaidie Wengine Waithamini Biblia. Mazungumzo ya maswali na majibu yakitegemea kitabu Mwabudu Mungu, ukurasa wa 24-25, fungu la 3-6. Tumia maswali ya funzo yaliyo katika kitabu hicho. Tia ndani maelezo kutoka katika ukurasa wa 32 wa broshua Kitabu kwa Ajili ya Watu Wote.

Wimbo 10 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Julai 25

Wimbo 138

Dak. 15: Matangazo ya kwenu. Soma ripoti ya hesabu na taarifa ya shukrani kwa ajili ya michango. Tumia mapendekezo yaliyo kwenye ukurasa wa 8 (ikiwa yanafaa eneo lenu), kuonyesha jinsi ya kutoa gazeti la Mnara wa Mlinzi la Julai 1 na Amkeni! la Julai 8. Mapendekezo mengine yanayofaa eneo lenu yanaweza kutumiwa. Katika onyesho moja, mhubiri atoe magazeti katika mahubiri yasiyo rasmi sokoni au sehemu nyingine ya umma inayofaa.

Dak. 10: Ikazie Kweli Katika Moyo wa Mtoto Wako. (Kum. 6:7) Hotuba itolewe na mzee ikitegemea Mnara wa Mlinzi, Agosti 15, 2002, ukurasa wa 30-31. Kazia kanuni za Kimaandiko ambazo humsaidia mzazi Mkristo kuwalea watoto ikiwa mwenzi wake si Shahidi.

Dak. 20: “Deni Letu kwa Wengine.”c Tia ndani maelezo kutoka katika Mnara wa Mlinzi, Julai 1, 2000, ukurasa wa 11, fungu la 13.

Wimbo 82 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Agosti 1

Wimbo 187

Dak. 15: Matangazo ya kwenu. Wakumbushe wahubiri watoe ripoti za utumishi za Julai. Waombe wasikilizaji wafungue ukurasa wa 70 wa kitabu Shule ya Huduma, na uzungumze nao fungu la 1 na 2 pamoja na sanduku lenye kichwa, “Jinsi ya Kutoa Maelezo Katika Mikutano.”

Dak. 15: “Wasaidie Watoto Wako Wafanye Maendeleo Katika Huduma.” Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Tia ndani onyesho la mzazi na mtoto wakitumia utangulizi rahisi. Mzazi anapaswa kumalizia onyesho hilo kwa kueleza kwa ufupi mpango wa kutoa michango.

Dak. 15: Je, Umejaribu Kubadili Utangulizi Wako Ufaane na Hali? Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji yakitegemea Huduma Yetu ya Ufalme ya Januari 2005, ukurasa wa 6. Pitia mapendekezo yaliyotolewa, na ueleze jinsi utangulizi unavyoweza kubadilishwa ili ufaane na toleo la vichapo la Agosti. Panga onyesho moja au mawili ya tangulizi zilizo katika Huduma hiyo.

Wimbo 218 na sala ya kumalizia.

[Maelezo ya Chini]

a Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.

b Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.

c Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki