Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Okt. 15
“Watu wengi hawana tumaini la wakati ujao na hilo linawafanya wahisi kwamba ni afadhali kuishi kwa ajili ya leo tu. Wewe una maoni gani? [Mruhusu ajibu.] Yesu alisema jambo hili linalopendeza. [Soma Mathayo 6:34.] Gazeti hili linaonyesha jinsi tunavyoweza kupangia wakati ujao bila kuuhangaikia sana.”
Amkeni! Okt.
“Sisi sote tumewapoteza wapendwa katika kifo. Je, unafikiri kwamba wanatutazama kutoka mbinguni? [Mruhusu ajibu.] Hebu ona kile ambacho Yesu alisema Lazaro alipokufa. [Soma Yohana 11:11.] Makala hii inaonyesha iwapo wafu wanaishi mahali fulani au ikiwa wamelala wakingojea ufufuo.” Zungumzia makala inayoanzia kwenye ukurasa wa 28.
Mnara wa Mlinzi Nov. 1
“Je, unafikiri dunia ingekuwa bora zaidi ikiwa watu wangekuwa wanyenyekevu zaidi? [Mruhusu ajibu.] Ona kile ambacho Yesu alisema kuhusu sifa hiyo. [Soma Mathayo 23:12.] Makala hii inazungumzia umuhimu wa kukuza sifa ya unyenyekevu, hata katika ulimwengu huu wenye mashindano.”
Amkeni! Nov.
“Zamani watu walitafuta mwongozo katika Biblia. Lakini siku hizi wengi wana mashaka. Wewe una maoni gani? [Mruhusu ajibu. Kisha soma 2 Timotheo 3:16.] Toleo hili la pekee la Amkeni! linatoa uthibitisho wenye kusadikisha kwamba Biblia imeongozwa na roho ya Mungu.”