Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 12/07 uku. 1
  • Tunahitaji Kudumisha Bidii Katika Huduma

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Tunahitaji Kudumisha Bidii Katika Huduma
  • Huduma ya Ufalme—2007
  • Habari Zinazolingana
  • Watu Wenye Juhudi ya Kazi Njema
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • “Wakeni Roho”
    Huduma ya Ufalme—2009
  • Je, Utaiga Bidii ya Yehova na Yesu Katika Majira Haya ya Ukumbusho?
    Huduma Yetu ya Ufalme—2015
  • Uwe Mwenye Bidii Katika Kueneza Ujumbe wa Ufalme
    Huduma Yetu ya Ufalme—1990
Pata Habari Zaidi
Huduma ya Ufalme—2007
km 12/07 uku. 1

Tunahitaji Kudumisha Bidii Katika Huduma

1 Kila mwaka tangu 1992, Mashahidi wa Yehova wametumia zaidi ya saa bilioni moja katika kazi ya ulimwenguni pote ya kuhubiri na kufanya wanafunzi. Jinsi tulivyo na furaha kushiriki kwa kadiri fulani katika kazi hiyo nzuri!—Mt. 28:19, 20.

2 Bila shaka, shukrani na sifa zote zinapaswa kumwendea Yehova ambaye ametutegemeza katika huduma yetu ‘nyakati hizi hatari.’ (2 Tim. 3:1) Tunahitaji kufanya nini ili tuendelee kushiriki kwa bidii katika kazi hii muhimu?

3 Msingi wa Kuwa na Bidii: Upendo wetu kwa Mungu na jirani, na tamaa ya kuishi kulingana na wakfu wetu, ndiyo hutuchochea tuendelee kushiriki kwa bidii katika huduma yetu ya Ufalme. (Mt. 22:37-39; 1 Yoh. 5:3) Upendo unatusukuma tujidhabihu ili tuweze kushiriki kwa ukamili katika kazi ya kuhubiri.—Luka 9:23.

4 Jitahidi Kudumisha Bidii: Adui yetu Ibilisi anafanya jitihada ili tupunguze bidii yetu katika huduma. Baadhi ya mambo anayotumia kutuvunja moyo ni, ubaridi wa watu katika eneo letu, ulimwengu wenye vikengeusha fikira vingi, hali ngumu za maisha na mahangaiko yanayotokana na kuzorota kwa afya.

5 Hivyo jitihada kubwa inahitajika ili tudumishe bidii yetu. Kwa hiyo ni muhimu tuendelee kusitawisha ‘upendo tuliokuwa nao mwanzoni.’ Hilo linatia ndani kuwa na kawaida ya kusoma na kutafakari Neno la Mungu, Biblia na kutumia maandalizi yote ya kiroho kutoka kwa “mtumwa mwaminifu na mwenye busara.”—Ufu. 2:4; Mt. 24:45; Zab. 119:97.

6 Kama unabii wa Biblia unavyoonyesha, siku ya Yehova ya kuharibu waovu imekaribia sana. (2 Pet. 2:3; 3:10) Tukiwa na hilo akilini acheni tuendelee kudumisha bidii yetu katika huduma, tukishiriki kwa ukamili katika kazi inayoendelea sasa ulimwenguni pote ya kuhubiri na kufanya wanafunzi!

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki