Ratiba ya Mkutano wa Utumishi
Juma Linaloanza Machi 10
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ukitumia mapendekezo kwenye ukurasa wa 4 au mapendekezo mengine yanayofaa eneo lenu, panga kuwe na maonyesho ya jinsi ya kutoa Mnara wa Mlinzi la Februari 1 na Amkeni! la Februari pamoja na mwaliko wa Ukumbusho.
Dak. 20: Kwa Nini Tukutanike Pamoja? Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji yakitegemea Mnara wa Mlinzi la Mei 15, 2007, ukurasa wa 11-13. Waombe wasikilizaji waeleze jinsi ambavyo kuhudhuria mikutano kumewanufaisha na jinsi ambavyo wameshughulika na vipingamizi ili wahudhurie mikutano kwa kawaida.
Dak. 15: “Tunaweza Kumpa Yehova.”a Kadiri wakati unavyoruhusu, waombe wasikilizaji watoe maelezo kuhusu maandiko ambayo hayakunukuliwa.
Juma Linaloanza Machi 17
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Wakumbushe wasikilizaji wabebe Mnara wa Mlinzi la Machi 1 na Amkeni! la Machi katika Mkutano wa Utumishi juma lijalo na wajitayarishe kuzungumzia utoaji unaofaa eneo lenu. Matangazo yaliyoteuliwa katika Huduma Yetu ya Ufalme.
Dak. 15: Sanduku la Swali. Sehemu hii ishughulikiwe na mzee. Soma na uzungumzie makala yote.
Dak. 20: “Tunaweza Kuwasaidiaje Watakaohudhuria Ukumbusho?”b Unapozungumzia fungu la 5, panga onyesho la jinsi funzo la Biblia linavyoweza kuanzishwa na mgeni ambaye amehudhuria Ukumbusho.
Juma Linaloanza Machi 24
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Soma ripoti ya hesabu na taarifa ya shukrani.
Dak. 15: Jitayarishe Kutoa Magazeti ya Karibuni. Mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Baada ya kuzungumzia kwa ufupi Mnara wa Mlinzi la Machi 1 na Amkeni! la Machi, waulize wasikilizaji ni makala gani zinaweza kuwavutia watu katika eneo lenu na kwa nini. Waombe wasikilizaji wataje mambo hususa katika gazeti hilo ambayo wamepanga kutumia. Ni swali gani watakalouliza ili kuanzisha mazungumzo? Kisha watasoma andiko gani kutoka kwenye makala? Ukitumia mapendekezo yaliyotolewa kwa ajili ya eneo lenu, onyesha jinsi ya kutoa Mnara wa Mlinzi la Machi 1 na Amkeni! la Machi.
Dak. 20: Tunaleta Habari Njema za Jambo Bora. Baada ya utangulizi usiozidi dakika moja, mzee atoe hotuba inayotegemea Mnara wa Mlinzi la Julai 1, 2005, ukurasa wa 18-19, mafungu 10-14. Waombe wasikilizaji waeleze jinsi ambavyo ujumbe wa Ufalme uliwafariji na kuwapa tumaini walipousikia mara ya kwanza.
Juma Linaloanza Machi 31
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Wakumbushe wahubiri watoe ripoti ya utumishi ya Machi.
Dak. 20: Tumia Vizuri Kitabu cha Mwaka cha 2008. Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Zungumzia “Barua Kutoka kwa Baraza Linaloongoza,” kwenye ukurasa wa 3-5. Waombe wasikilizaji wawili au watatu wasimulie mambo yaliyoonwa ambayo yaliwatia moyo sana katika Kitabu cha Mwaka. Panga mapema ili mhubiri mmoja au wawili waeleze jinsi ambavyo wamepanga ratiba yao ili wasome Kitabu cha Mwaka. Malizia kwa kuwatia moyo wote wasome kitabu chote. Ikiwa Kitabu cha Mwaka cha 2008 hakijafika, tumieni cha mwaka wa 2007 na mwatie moyo akina ndugu wasome cha mwaka wa 2008 kitakapofika, kama ilivyopendekezwa.
Dak. 15: “Kujengana Tunapokuwa Katika Huduma.”c
Juma Linaloanza Aprili 7
Dak. 10: Matangazo ya kwenu.
Dak. 20: Kwa Nini Unaahirisha Kubatizwa? Hotuba itolewe na mzee ikitegemea Mnara wa Mlinzi la Julai 1, 2006, ukurasa wa 29-30, mafungu 14-17. Wahoji kwa ufupi wahubiri wawili au watatu waliobatizwa wakiwa matineja. Ni nini kilichowachochea wachukue hatua hiyo muhimu wakiwa wachanga? Ubatizo uliwasaidiaje wakomae kiroho, na hivyo kuwalinda?
Dak. 15: Je, Umejaribu Njia ya Moja kwa Moja? Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji ikitegemea nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Januari 2002, ukurasa wa 6. Zungumzia madokezo yaliyoonyeshwa na jinsi yanaweza kubadilishwa ili yafae kuanzisha funzo la Biblia katika kitabu Biblia Inafundisha. Kisha kuwe na onyesho moja au mawili. Watie moyo wasikilizaji wajaribu angalau mara moja juma lijalo kuanzisha funzo la Biblia katika kitabu Biblia Inafundisha wakitumia njia ya moja kwa moja.
[Maelezo ya Chini]
a Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.
b Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.
c Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.