Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 1/10 uku. 2
  • Sanduku la Swali

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Sanduku la Swali
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2010
  • Habari Zinazolingana
  • Sanduku la Swali
    Huduma Yetu ya Ufalme—1989
  • Sanduku La Swali
    Huduma Yetu ya Ufalme—2000
  • Wasaidie Watoto Wanufaike Zaidi na Mikutano
    Huduma Yetu ya Ufalme—1988
  • Mikutano ya Mashahidi wa Yehova Inaweza Kukunufaishaje?
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2010
km 1/10 uku. 2

Sanduku la Swali

◼ Sote tunawezaje kuchangia hali nzuri ya kujifunza kwenye mikutano ya kutaniko? (Kum. 31:12)

Kwa kuwa tunamheshimu Yehova sana na tunathamini mikutano ya kutaniko ambayo ametuandalia, sote tunatiwa moyo kufika mapema na kuwa tayari kufunzwa naye. Inafaa kuketi kwenye viti vya mbele, na kuacha viti vya nyuma kwa ajili ya wazazi walio na watoto wachanga na wale ambao pindi moja moja hufika wakiwa wamechelewa. Kabla ya mikutano kuanza, walio na vifaa vya elektroniki, kama vile simu za mkononi, wanapaswa kuzizima au kupunguza sauti ya vifaa hivyo ili visiwakengeushe fikira wasikilizaji. Iwapo wote ambao wamehudhuria wanaonyesha heshima kipindi chote wanapokuwa mikutanoni, vikengeusha fikira vinakuwa vichache na vidogo.—Mhu. 5:1; Flp. 2:4.

Wapya wanapoanza kuhudhuria mikutano, ndugu au dada anayewafahamu anaweza kujitolea kuketi pamoja nao. Hilo linakuwa jambo zuri hasa ikiwa wana watoto wadogo wanaohitaji kuzoezwa kuketi kwa utulivu. Huenda ikawa kuhudhuria mikutano ni jambo ambalo hawajazoea. Ikiwa ndivyo, yaelekea watapenda kuketi nyuma ambapo hawatawakengeusha wengine fikira ikiwa itawabidi wazazi waondoke kwa muda kwenye jumba kuu ili kuwashughulikia watoto. (Met. 22:6, 15) Familia zenye watoto wadogo hazipaswi kuketi katika chumba kingine ambapo watoto wanaweza kujihisi huru kupiga kelele. Inafaa mzazi amtie nidhamu mtoto au ashughulikie mahitaji mengine ya mtoto wake nje ya jumba kuu, kisha arudi naye kwenye jumba kuu.

Wakaribishaji husaidia kudumisha hali inayofaa katika nyumba ya ibada. Wao huzisaidia familia na wale ambao pindi moja moja hufika wakiwa wamechelewa, wapate mahali panapofaa pa kuketi. Wakaribishaji wanatumia busara kuwasaidia wengine wapate mahali pazuri pa kuketi bila kukengeusha fikira za wasikilizaji isivyo lazima. Wanatumia busara pia wanaposhughulikia hali zozote zisizotazamiwa ambazo zinaweza kuwasumbua wasikilizaji. Tabia ya mtoto inapoanza kukengeusha fikira za wengine, wakaribishaji wanaweza kumsaidia mzazi kwa fadhili.

Wote ambao wamehudhuria mikutano ya ibada wanaweza kuchangia hali nzuri ya kujifunza kumhusu Yehova na kusudi lake la kuleta ulimwengu mpya wenye amani na uadilifu.—Ebr. 10:24, 25.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki