Mialiko ya Ukumbusho Itakayosambazwa Duniani Kote!
1. Ni kampeni gani ya pekee ya duniani kote ambayo imepangwa kufanywa kabla ya Ukumbusho?
1 “Endeleeni kufanya hivi kwa kunikumbuka mimi.” (Luka 22:19) Kwa sababu waabudu wa Yehova wanatii amri hii ya Yesu, watakusanyika pamoja na watu wanaopendezwa ili kuadhimisha kifo cha Yesu mnamo Machi 30, 2010. Mialiko ya pekee ya Ukumbusho itasambazwa duniani kote kuanzia Machi 13 hadi Machi 30.
2. Tunaweza kutoa mwaliko jinsi gani?
2 Jinsi ya Kutoa Mwaliko: Unaweza kumpa mwenye nyumba mwaliko ili aone picha kwenye ukurasa wa kwanza, kisha useme: “Katika jioni ya Machi 30, mamilioni ulimwenguni kote watakusanyika ili kuadhimisha kifo cha Yesu. Nimekuletea wewe na familia yako mwaliko wa kuhudhuria mkutano huo. Marafiki wako pia wamekaribishwa. Tafadhali zingatia wakati na mahali pa maadhimisho hayo katika eneo letu.” Ikitegemea hali unaweza kuamua kusoma andiko la Luka 22:19 na kumwonyesha amri ya Biblia ya kuadhimisha tukio hilo. Hata hivyo, kumbuka kwamba hatuna muda mrefu wa kusambaza mialiko hiyo katika eneo, kwa hiyo zungumza kifupi.
3. Tutawaalika akina nani?
3 Ikiwa kutaniko lenu lina eneo kubwa, wazee wanaweza kuwaambia wahubiri waache mialiko kwenye nyumba zisizo na watu wakati wa ziara ya kwanza. Inapofaa, unaweza kuwapa watu magazeti unapotoa mialiko hiyo. Hakikisha kwamba umewaalika watu unaowarudia, wanafunzi wa Biblia, watu wa ukoo, wanafunzi wenzako, wafanyakazi wenzako, jirani zako, na watu wengine unaofahamiana nao.
4. Kuthamini upendo ambao Yehova alionyesha kwa kuandaa fidia, kutatusukuma tufanye nini?
4 Jitayarishe Kushiriki Kikamili: Majira ya Ukumbusho ni kipindi kizuri cha kupanua utumishi wetu. Je, unaweza kurekebisha ratiba yako ili uwe painia msaidizi? Je, una watoto au wanafunzi wa Biblia ambao wanafanya maendeleo ya kiroho? Ikiwa ndiyo, zungumza na wazee ili ujue kama wapya hao wanastahili kushiriki katika kampeni hii ya pekee wakiwa wahubiri ambao hawajabatizwa. Uthamini wetu kwa upendo ambao Yehova alionyesha kwa kuandaa fidia, utatusukuma tuhudhurie Ukumbusho na pia kuwaalika wengi iwezekanavyo wajiunge nasi.—Yohana 3:16.