Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Februari 1
“Watu wengi wana dini zao. Je, unafikiri kwamba Mungu anajali jinsi tunavyomwabudu? [Mruhusu ajibu, kisha usome Mathayo 15:9.] Gazeti hili linazungumzia mambo manne ambayo Yesu alisema yanatambulisha dini ya kweli.” Mwonyeshe makala inayoanzia ukurasa wa 16.
Amkeni! Februari
“Watu fulani wanaamini kuna Muumba, lakini watu wengine wana maoni kwamba jambo hilo halipatani na akili wala si la kisayansi. Maoni yako ni nini? [Mruhusu ajibu.] Kulingana na Biblia, imani ya kweli inategemea mambo ya hakika. [Soma Waebrania 11:1.] Makala hii inazungumzia baadhi ya mambo yanayothibitisha kwamba kuna Muumba.” Mwonyeshe makala inayoanzia ukurasa wa 22.
Mnara wa Mlinzi Machi 1
“Je, unafikiri kwamba Biblia ni Neno la Mungu au ni kitabu kizuri tu? [Mruhusu ajibu.] Ona vile Biblia yenyewe inavyosema. [Soma 2 Timotheo 3:16, 17.] Gazeti hili litakusaidia kufanya uamuzi unaofaa kuhusu jambo hili, na pia litakuonyesha umuhimu wa kufanya hivyo.”
Amkeni! Machi
“Kama ilivyo kwa watu wengi, yaelekea wewe pia unavutiwa na uzuri wa vitu vya asili. Je, unafikiri kwamba vitu vya asili vimebuniwa kwa akili? [Mruhusu ajibu, kisha usome Zaburi 104:24.] Gazeti hili linataja vitu vya asili vyenye kupendeza na mambo ambayo tunajifunza kutokana navyo.”