Ratiba ya Juma Linaloanza Februari 28
JUMA LINALOANZA FEBRUARI 28
Wimbo 5 na Sala
□ Funzo la Biblia la Kutaniko:
cf sura ya 18 ¶10-18 (Dak. 25)
□ Shule ya Huduma ya Kitheokrasi:
Usomaji wa Biblia: Esta 1-5 (Dak. 10)
Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi (Dak. 20)
□ Mkutano wa Utumishi:
Dak. 5: Matangazo.
Dak. 10: Uwe Mwenye Kutia Moyo Unapofundisha. Mazungumzo yanayotegemea kitabu Shule ya Huduma, ukurasa wa 202. Ukitumia toleo la mwezi ujao, onyesha jinsi ya kutumia mapendekezo yaliyo katika fungu la mwisho.
Dak. 10: Faidika kwa Kuyachunguza Maandiko Kila Siku. Mazungumzo yanayotegemea dibaji ya kijitabu Kuyachunguza Maandiko—2011. Ikiwa hakipatikani, tumia dibaji ya kijitabu Kuyachunguza Maandiko—2010. Watie moyo wote wachunguze andiko kila siku. Waombe wasikilizaji waeleze wakati ambao wametenga kwa ajili ya kusoma andiko na jinsi ambavyo wamenufaika. Pitia kifupi andiko la mwaka wa 2011. Zungumzia sehemu yenye kichwa “Andiko la Siku Halitazungumziwa Tena Katika Mikutano ya Utumishi wa Shambani.”
Dak. 10: Jitayarishe Kutoa Magazeti Katika Mwezi wa Machi. Mazungumzo. Tumia dakika moja au mbili kueleza mambo yaliyomo katika magazeti ya karibuni. Kisha chagua makala mbili au tatu na uwaombe wasikilizaji wapendekeze maswali na maandiko yanayoweza kutumiwa magazeti hayo yanapotolewa. Onyesha jinsi kila gazeti linavyoweza kutolewa.
Wimbo 33 na Sala