“Inafaa Kuripoti Muda Gani?”
Umewahi kujiuliza swali hilo? Mwongozo unapatikana katika kitabu Tengenezo, ukurasa wa 86-87. Habari zaidi hutolewa mara kwa mara, kama vile katika Sanduku la Swali la Huduma Yetu ya Ufalme ya Septemba 2008. Kwa kuwa hali hutofautiana, hatujapewa orodha ndefu ya maagizo. Hivyo basi, haifai wazee au wahubiri wengine kutoa maagizo zaidi.
Iwapo swali linazuka na hakuna mwongozo uliochapishwa kuhusiana na swali hilo, kila mhubiri anaweza kujiuliza: Je, wakati huo ulitumiwa katika huduma? Au ulitumiwa katika shughuli nyingine ambayo si sehemu ya huduma? Ripoti ya huduma ya shambani tunayotoa kila mwezi inapaswa kutupa shangwe na si kutuacha na dhamiri isiyo safi. (Mdo. 23:1) Jambo muhimu si kuzingatia muda ambao tunaripoti, bali kuhakikisha kwamba tumehubiri kwa bidii muda huo.—Ebr. 6:11.