Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 8/12 uku. 1
  • Linda Dhamiri Yako

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Linda Dhamiri Yako
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2012
  • Habari Zinazolingana
  • Kuendelea Kuwa na Dhamiri Njema
    “Jitunzeni Katika Upendo wa Mungu”
  • Je! Wewe Unaongozwa na Dhamiri Nyepesi ya Kikristo?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Sauti ya Dhamiri Iliyomo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Dhamiri Njema Mbele za Mungu
    Jinsi ya Kudumu Katika Upendo wa Mungu
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2012
km 8/12 uku. 1

Linda Dhamiri Yako

1. Programu ya kusanyiko la pekee la mwaka wa utumishi wa 2013 ina kichwa gani, na ni nini kusudi la programu hiyo?

1 Kila siku, tunakabili hali ambazo zinaweza kutufanya tuchafue dhamiri yetu. Ndiyo sababu programu ya kusanyiko la pekee ni yenye kichwa “Linda Dhamiri Yako.” Programu hiyo ya mwaka wa utumishi wa 2013 itaanza Septemba 1, 2012. (1 Tim. 1:19) Programu hiyo imekusudiwa kumsaidia kila mmoja wetu afikirie kwa uzito jinsi ya kutumia zawadi hii ya pekee kutoka kwa Muumba wetu.

2. Ni maswali gani muhimu yatakayojibiwa wakati wa programu?

2 Tafuta Majibu ya Maswali Haya: Programu hiyo itajibu maswali saba makuu kuhusu dhamiri:

• Ni nini kinachoweza kuhatarisha dhamiri?

• Tunaweza kuizoeza dhamiri yetu katika njia gani?

• Inawezekanaje kuwa safi kutokana na damu ya watu wote?

• Kufikiri na kutenda kwetu kupatana na kanuni za Biblia hufunua nini kutuhusu?

• Tunawezaje kuepuka kuwaumiza wengine kuhusiana na mambo ya dhamiri?

• Vijana, mnaweza jinsi gani kuvumilia mnaposhinikizwa kufanya mambo yasiyofaa?

• Wale wanaofuata dhamiri yao inayoongozwa na roho hupokea baraka gani?

3. Tunaweza kunufaika na programu hiyo jinsi gani?

3 Kwa msaada wa Yehova, tunaweza kupinga jitihada za Shetani za kuharibu dhamiri yetu. Kupitia Neno la Mungu na tengenezo lake, Baba yetu wa mbinguni mwenye upendo anatuambia: “Hii ndiyo njia. Tembeeni ndani yake.” (Isa. 30:21) Programu hiyo ni mojawapo ya njia ambazo Yehova anatumia ili kutuandalia mwongozo kama huo. Hivyo basi, fanya mipango ya kuhudhuria programu yote. Sikiliza kwa makini, na ufikirie jinsi wewe binafsi unavyoweza kutumia habari inayozungumziwa. Zungumzieni programu hiyo mkiwa familia. Kutumia maagizo tunayopewa kutatuimarisha tuendelee ‘kuwa na dhamiri njema’ na kutatusaidia tusiruhusu tamaa za ulimwengu wa Shetani ambazo zinapitilia mbali zitushawishi kuharibu uhusiano wetu na Yehova.​—⁠1 Pet. 3:16.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki