Ni Nani Wanaofanya Mapenzi ya Yehova Leo?
1. Tutaanza kuzungumzia broshua Mapenzi ya Yehova lini, na tutafaidikaje?
1 Kuanzia juma la Oktoba 28, katika Funzo la Biblia la kutaniko, tutaanza kujifunza broshua Ni Nani Wanaofanya Mapenzi ya Yehova Leo? Broshua hiyo mpya iliyotolewa katika Kusanyiko la Wilaya la “Linda Moyo Wako!” imekusudiwa kuwaelekeza wanafunzi wa Biblia kwenye tengenezo. Kujifunza broshua hii kutaongeza uthamini wetu wa kuwa sehemu ya tengenezo la Yehova na kutatusaidia tujue jinsi ya kuitumia kwenye utumishi.—Zab. 48:13.
2. Tutafuata utaratibu gani kujifunza broshua Mapenzi ya Yehova kutanikoni?
2 Jinsi Tutakavyojifunza Broshua Hiyo: Ndugu anayeongoza anapaswa kupanga wakati vizuri ili kuwe na muda wa kutosha wa kuzungumzia kila somo. Ataanza kila somo kwa kusoma swali ambalo ndilo kichwa cha somo linalozungumziwa. Kisha, atamwalika msomaji asome fungu la kwanza. Halafu, ndugu huyo anayeongoza atawauliza wasikilizaji swali la utangulizi ambalo ametayarisha. Kisha, kila kisehemu kinachoanza kwa maneno yaliyoandikwa kwa wino mzito kinapaswa kusomwa na kuzungumziwa kimoja baada ya kingine. Baada ya kisehemu hicho kusomwa, ndugu anayeongoza atawaalika wasikilizaji watoe maelezo ya jinsi kisehemu hicho kinavyojibu swali ambalo ni kichwa cha somo hilo. Pia, broshua hiyo ina picha nyingi ambazo wahubiri wanaweza kuzizungumzia. Maandiko ya msingi yanapaswa kusomwa wakati ukiruhusu. Kabla ya kuendelea na somo linalofuata, anayeongoza atapitia somo kwa kuuliza maswali yaliyo chini ya ukurasa. Ikiwa kuna sanduku lenye kichwa “Pata Kujua Mengi Zaidi,” atahakikisha limesomwa, kisha atawaalika wahubiri waeleze jinsi mwanafunzi wa Biblia anavyoweza kunufaika kwa kufuata pendekezo hilo. Mwishoni mwa somo ikiwa bado kuna wakati, ndugu anayeongoza anaweza kutumia vichwa vya masomo kama maswali ya pitio. Kumbuka kwamba si lazima ufuate utaratibu huu unapojifunza Biblia na mtu.
3. Tutafaidikaje kwa kujifunza broshua Mapenzi ya Yehova?
3 Ili ufaidike kikamili, jitayarishe vizuri. Jitahidi kutoa maelezo. Mnapoendelea na mazungumzo, fikiria kwa nini sehemu hiyo itawanufaisha wanafunzi wa Biblia. Na tuendelee kuwasaidia wengine wajiunge nasi kufanya mapenzi ya Mungu kwa kujifunza broshua hii mpya ili wao pia wapate tumaini la kuishi milele.—1 Yoh. 2:17.