Je, Unajitayarisha kwa Ajili ya Ukumbusho?
Ilikuwa Nisani 13 ya mwaka wa 33 W.K. Yesu alijua kwamba ana jioni moja tu ya mwisho ya kuwa pamoja na wanafunzi wake kabla ya kifo chake. Angesherehekea Pasaka ya mwisho pamoja nao na kisha kuanzisha mwadhimisho mpya yaani, Mlo wa Jioni wa Bwana. Bila shaka, tukio hilo muhimu lingehitaji matayarisho. Kwa hiyo, akawatuma Petro na Yohana kufanya matayarisho. (Luka 22:7-13) Kila mwaka tangu wakati huo, imekuwa muhimu kwa Wakristo wanaoadhimisha Ukumbusho kujitayarisha kwa ajili ya tukio hilo. (Luka 22:19) Ni mambo gani ya msingi tunayohitaji kutayarisha kwa ajili ya Ukumbusho utakaofanyika Aprili 3?
Matayarisho Yanayofanywa na Wahubiri:
Wahubiri hujitayarisha ili kushiriki kikamili katika kampeni ya kuwaalika watu kwenye Ukumbusho.
Huandika orodha ya mafunzo ya Biblia, watu wa ukoo, wanafunzi wenzao, wafanyakazi wenzao, na watu wengine wanaowafahamu ili kuwaalika.
Husoma na kutafakari usomaji wa Biblia kwa ajili ya Ukumbusho.
Hupanga kufika mapema kwenye Ukumbusho ili kuwakaribisha wageni.