Kuboresha Ustadi Wetu Katika Huduma—Kusitawisha Upendezi wa Watu Wanaopokea Magazeti Yetu kwa Ukawaida
Kwa Nini Ni Muhimu: Watu wengi wanaosoma magazeti yetu hawapendi kujifunza Biblia pamoja nasi. Huenda wanazipenda sana dini zao, au wanahisi kwamba hawana muda wa kutosha ili kujifunza. Hata hivyo, wanaposoma magazeti yetu kwa ukawaida huenda wakakuza tamaa kuelekea Neno la Mungu. (1 Pet. 2:2) Huenda makala fulani zikawavutia, au hali zao zikabadilika. Kuwatembelea kwa ukawaida kutawafanya wastarehe zaidi na kutatusaidia kujua mambo wanayopenda na mambo yanayowahangaisha. Hatimaye, huenda tukaanzisha funzo la Biblia.
Jaribu Dokezo Hili kwa Mwezi Mzima:
Andika orodha ya watu utakaowapelekea magazeti kwa ukawaida. Wapelekee magazeti ya karibuni, na uwajulishe kwamba utawaletea magazeti ya mwezi ujao.