Mapendekezo kwa Ajili ya Utumishi
Mnara wa Mlinzi Oktoba 1
“Tunawaonyesha jirani zetu nakala hii yenye kupendeza ya gazeti la Mnara wa Mlinzi. [Mwonyeshe jalada la gazeti.] Watu fulani wanafikiri kwamba kusali ni kupoteza tu muda kwa sababu hakuna anayesikiliza. Wengine wanaamini kwamba Mungu husikiliza sala zao. Wewe una maoni gani? [Mruhusu ajibu.] Ona mambo ambayo Biblia inasema kuhusu sala. [Soma Isaya 30:19.] Gazeti hili linathibitisha kwamba Mungu husikiliza na kujibu sala zenye mambo yanayofaa na zinazotolewa kwa njia inayofaa.”
Amkeni! Oktoba
“Tunawatembelea jirani zetu kwa muda mfupi kwa sababu watu wengi wanajiuliza kwa nini Mungu anawaacha watu wateseke. Je, unafikiri ni kukosa heshima kumuuliza Mungu swali hilo? [Mruhusu ajibu.] Mwanamume mwadilifu Ayubu alitamani kumuuliza Mungu maswali. [Soma Ayubu 23:3-5.] Gazeti hili linazungumzia maswali matatu ambayo watu wengi wangependa kumuuliza Mungu ikiwa wangepata fursa, na lina majibu yenye kuridhisha kutoka kwenye Biblia.”