Mapendekezo kwa Ajili ya Utumishi
Mnara wa Mlinzi Novemba 1
“Vita vinapotokea, pande zote mbili huamini kwamba Mungu ndiye anayewasaidia. Je, unafikiri Mungu huunga mkono vita? [Mruhusu ajibu.] Gazeti hili la Mnara wa Mlinzi linazungumzia sababu zilizomfanya Mungu aruhusu vita wakati uliopita, na jinsi atakavyokomesha vita milele.” Soma Zaburi 46:9 na umwachie magazeti.
Awake! Novemba
“Watu wengi ulimwenguni pote wanahangaishwa na unafiki na mafundisho ya uwongo ya dini mbalimbali. Je, unafikiri dini zitaendelea kuwepo? [Mruhusu ajibu.] Gazeti hili linazungumzia unabii muhimu unaopatikana kwenye kitabu cha Biblia cha Ufunuo unaotabiri kuhusu kupungua kwa wafuasi na kuangamizwa kabisa kwa dini za uwongo.”