HAZINA ZA NENO LA MUNGU | NEHEMIA 9-11
Watumishi Waaminifu Huunga Mkono Mipango ya Kitheokrasi
Njia mbalimbali ambazo watumishi wa Mungu waliunga mkono kwa hiari ibada ya kweli
Taifa lilijitayarisha na kusherehekea Sherehe ya Vibanda kwa njia inayofaa
Kila siku watu walikusanyika kusikiliza Sheria ya Mungu ikisomwa, na walipata shangwe kwa kufanya hivyo
Watu waliungama dhambi zao, walisali, na walimwomba Yehova awabariki
Watu walikubali kuendelea kuunga mkono mipango yote ya kitheokrasi
Waliendelea kuunga mkono mipango ya kitheokrasi kwa:
Kuoa au kuolewa na waabudu wa Yehova pekee
Kutoa michango ya pesa
Kushika Sabato
Kuandaa kuni kwa ajili ya madhabahu
Kumtolea Yehova mazao ya kwanza ya mavuno na wazaliwa wa kwanza wa mifugo