Andiko la Mwaka wa 2013
“Uwe Hodari na Mwenye Nguvu. . . . Yehova Mungu Wako Yupo Pamoja Nawe.”—Yoshua 1:9.
Mnamo 1473 K.W.K., Waisraeli walikuwa karibu kuingia katika Nchi ya Ahadi, lakini maadui wenye nguvu walikuwa mbele yao. Mungu alimwamuru Yoshua hivi: “Uwe hodari na mwenye nguvu sana.” Yoshua angefanikiwa ikiwa tu angeendelea kuwa mwaminifu. Aliambiwa: “Usitetemeke wala usiwe na hofu, kwa maana Yehova Mungu wako yupo pamoja nawe kila mahali unapoenda.” Na kwa kweli Mungu alithibitika kuwa pamoja naye, kwani Waisraeli waliwashinda adui zao katika muda wa miaka sita tu.—Yos. 1:7-9.
Wakristo wa kweli wako karibu kuingia katika ulimwengu mpya ulioahidiwa, hivyo wanahitaji kuwa hodari na wenye nguvu. Kama Yoshua tunakabili maadui wenye nguvu ambao wanajitahidi kuvunja utimilifu wetu. Hatupigani vita kwa mikuki na mapanga, bali tunatumia silaha za kiroho, na Yehova anatufundisha jinsi ya kuzitumia kwa ustadi. Hata ukikabili hali gani, uwe na hakika kwamba ukiwa hodari, mwenye nguvu, na mwaminifu, Yehova atakuwa pamoja nawe na atakusaidia kushinda.