Ngoma Zisemazo
●Je! wewe umepata kuona katika sinema au kusoma katika vitabu juu ya ujumbe unaopelekwa katika mapori kwa njia ya kupiga ngoma? Je! ujumbe unaweza kupelekwa kwa usahihi kwa kugeuza namna ya kupiga ngoma na mlio wake?
Wakati wa Desemba 1970 kusanyiko kubwa la mataifa yote la Mashahidi wa Yehova lilifanywa Lagos, Nigeria. Asubuhi moja kipindi cha pekee kilifanywa kwa ajili ya wajumbe waliokuwa wakizuru kutoka Amerika ya Kaskazini na Ulaya. Historia ya Mashahidi wa Yehova ilizungumzwa katika Nigeria. Wasikilizaji walifurahishwa pia na wonyesho wa “ngoma zisemazo.”
Alitokea mpiga ngoma. Shahidi mmoja akamnong’onezea ujumbe aliopaswa atoe. Ndipo ule ujumbe ulipopigwa mara tatu katika ngoma. Wasikilizaji waliulizwa hivi, “Je! mtu ye yote wa kabila la Yoruba aliye kati ya wasikilizaji aweza kufahamu ujumbe huo?” Mara hiyo mkono ulisimamishwa juu na ule ujumbe ukatolewa katika Kiyoruba na kutafsiriwa hivi katika Kiingereza: “Baba yetu uliye mbinguni, jina lako litukuzwe.” (Mt. 6:9) Lo! kulitokea vifijo wee! Tena, ujumbe mwingine ukapigwa katika ngoma. Mtu tofauti wa kabila la Yoruba katika wasikilizaji akaufahamu mara hiyo, ukisema: “[Yehova] ndiye mchungaji wangu, sitapungukiwa na kitu.” (Zab. 23:1) Maonyesho hayo mawili yaliondolea wasikilizaji wote mashaka wapate kusadiki kwamba kweli ngoma za Kiyoruba zaweza ‘kusema.’