Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w77 3/15 uku. 141
  • Usiamue kwa Kutazama Sura

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Usiamue kwa Kutazama Sura
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
  • Habari Zinazolingana
  • Je! Wewe Huona Sura ya Nje-Nje Tu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Je! Wewe Hustahi Mahali Pako pa Ibada?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
  • Mipango ya Mahali pa Ibada
    Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
  • Kwa Nini Uhudhurie Mikutano Kwenye Jumba la Ufalme?
    Vijana Huuliza
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
w77 3/15 uku. 141

Usiamue kwa Kutazama Sura

■ Biblia hutushauri tusihukumu moyo wa mtu kwa kutazama sura yake. Hata akija kwenye mkutano wa Wakristo wa kweli amevaa matambara, apaswa kuonyeshwa upendo na kufkiriwa.​—Yak. 2:1-4.

Matokeo mema yanayoweza kuja juu ya mtu huyo kwa sababu ya kumtendea kwa upendo yaonekana kutokana na yaliyompata kijana mmoja Mali, Afrika. Mmoja wa Mashahidi wa Yehova alikuwa akijifunza Biblia na kijana huyu na alimkaribisha mara nyingi ahudhurie mikutano katika Jumba la Ufalme. Ingawa aliahidi kufanya hivyo, kijana huyo hakufika. Ili aepuke kukaribishwa tena, mwishowe alifika.

Mavazi yake yalikuwa machafu, yalikuwa mafupi mno tena yalikuwa matambara. Isitoshe, alivaa kofia ya kusokotwa ambayo kanda zake zilifika magotini, nazo ziliunganishwa mwishoni zikawa kama mpira wa sufu. Alivaa hivyo akikusudia Mashahidi wa Yehova wakatae asiingie katika Jumba la Ufalme lao. Lakini jinsi alivyoshangaa kukaribishwa kwa uchangamfu!

Kijana huyo aeleza matokeo: “Sijaona aibu niliyoona wakati huo maishani mwangu. Nilikwenda kwenye Jumba la Ufalme ili nikafukuzwe, lakini lo! nikakaribishwa kama mmoja wa Mashahidi! Nakuambia, ingalikuwa vizuri kama ningalivaa mavazi ya adabu; kila mtu alikuwa amevalia vizuri.” Kilichoongeza aibu yake ni kwamba mmoja wa rafiki zake alikuwa amehudhuria pia. Mara baada ya mkutano rafiki yake alimjia akamwambia: “Wewe huna haya kuja kwenye Jumba la Ufalme na mavazi machafu hivyo? Sikutazamia utende hivyo.” Tangu wakati huo, kijana huyo alianza kujifunza Biblia na kuhudhuria mikutano bila mchezo. Sasa anashiriki kwa bidii nyingi kueleza wengine kweli ya Biblia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki