Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g90 9/8 kur. 13-15
  • Krusedi ya Jeuri kwa Nini?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Krusedi ya Jeuri kwa Nini?
  • Amkeni!—1990
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Kumtii Ibilisi
  • Mikutano Huleta Jeuri
  • Usumbufu Hatari Unaoongezeka
    Amkeni!—1990
  • Shetani Kavaa Kificha-Sura
    Amkeni!—1990
  • Vijana wa Leo—Je, Ni Windo Rahisi kwa Ushetani?
    Amkeni!—1994
  • Ibada ya Shetani Katika Wakati Wetu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—1990
g90 9/8 kur. 13-15

Krusedi ya Jeuri kwa Nini?

USHETANI, au ibada ya Ibilisi, ulianza kule nyuma wakati wa wanadamu wa kwanza. Kuwapo kusikoonekana wazi kwa Shetani katika bustani ya Edeni ndiko kulikoongoza jozi ya kwanza ya kibinadamu iondoke kwa Muumba wao, Yehova Mungu. (Mwanzo 3:1-6; Ufunuo 12:9) Kuliwatia alama milele kuwa washirika wa kwanza wa Shetani.

Katika mileani ambazo zimefuata, Ushetani umetokeza matukio yao mabaya yenye mafumbo ya kiroho kwa namna mbalimbali—uchawi, mizungu yenye kuua, kunuiza tego za roho waovu, na nyingine nyingi. Hata hivyo, kwa ujumla jina la Shetani na utambulisho wa ibada yake limeendelea kutotajwa lisijulikane na wafuasi na wazoevu wa ibada hiyo.

Tangu karne ya 20 iingie, ibada ya kishetani imehuishwa waziwazi na kwa ufidhuli, na leo imevamia sehemu nyingi za ulimwengu. Ushetani umetokea katika tamasha ya kidini ukiwa na sura mpya ya ujasiri. Haifichwi tena bila kutajwa jina, kwa kuipaka chokaa. Bali, Shetani huabudiwa kwa njia zenye jeuri ziwezazo kuwaziwa.

Mmoja wa waanzilishi wa mapema wa Ushetani katika karne hii alikuwa Mwingereza jina lake Aleister Crowley. Katika 1905, katika Los Angeles, Kalifornia, Crowley alikipanga kitengenezo kikundi cha Ushetani chenye kuitwa “Ordo Templi Orientis.” Muda si muda yeye akawa ndiye kiongozi mkubaliwa wa kiibada chenye kukua. Katika kitabu chake Book of Law, Crowley alitetea msemo mpya wa imani ya kidini: “Fanya utakalo itakuwa ndiyo sheria kamili.” Ni kutokana na falsafa hii kwamba Crowley alitetea kuvunjwa kwa kila fungu la sheria za kiadili na kanuni ya Biblia ijulikanayo kwa binadamu. Hivyo uuaji, jeuri, kuingilia wanawake kinguvu, na kuwatoa wanadamu kama dhabihu kukawa sehemu ya desturi ya kidini.

Kuhusu dhabihu ya kibinadamu, Crowley aliandika hivi: “Kwa karibu makusudi yote, dhabihu ya kibinadamu ndiyo bora kabisa, na mtoto wa kiume mwenye unyoofu mkamilifu na akili ya juu ndiye mhanga mwenye kuridhisha na kufaa kabisa.” Wakati mmoja Crowley alijitaja kuwa “binadamu aliye mwovu kabisa ulimwenguni.” Baada ya kutumia wakati akiwa katika makao ya wenye kichaa, yaripotiwa kwamba alikufa akiwa mzoelevu wa kutumia heroini katika nyumba ya kukodishwa rahisi katika Uingereza.

Hata hivyo, sikitiko ni kwamba falsafa ya Crowley ya uhuru wa ‘kufanya lile ambalo mtu ataka’ kwa jina la dini haikufa pamoja naye. Angalia maoni haya ya mwandikaji mmoja: “Kivuli cha Aleister Crowley kimejaa katika [eneo la Los Angeles], lakini matendo yake ya kupita kiasi si kitu hata kidogo yakilinganishwa na waabudu wa leo wa ibilisi.”

Kumtii Ibilisi

Waabudu wa Shetani huamini kwamba Shetani kwamba Ibilisi ndiye hutawala ulimwengu. Zaidi ya hilo, kulingana na Robert J. Barry, akiandika katika The National Sheriff, “mwisho wa ulimwengu ujapo, majeshi ya Lusiferi yatashinda majeshi ya Mungu na Kristo nayo yatatawala mbinguni. Kwa hiyo, mwabudu wa Shetani huapa kutii ibilisi, si ili apate usaidizi wake tu katika ulimwengu huu, bali pia katika ulimwengu unaokuja.”

Waabudu wengine wa Shetani husemwa kwamba wanaamini “Kristo na Shetani wameunganisha majeshi yao ili kuleta mwisho wa ulimwengu.” Kristo husemwa na kiibada kimoja cha kishetani kuwa humtumia Shetani kuwa mbabe mkuu wa pigano. Hivyo, kulingana na Maury Terry, katika kitabu chake The Ultimate Evil, “kuabudu Shetani kulikuwa ni kama kuabudu Kristo. Na kuua kwa jina la Shetani kulikuwa hasa ni kuua kwa ajili ya Kristo: utume wa kimungu.”

Aleister Crowley ndiye aliyesema kwamba alitaka “ukufuru, uuaji, kuingilia wanawake kinguvu, mapinduzi, lolote lililo baya,” liwe sehemu ya fundisho na mazoea ya kidini ya kiibada hicho. Kwa kweli, kiongozi mmoja wa kiibada aliutangaza wazi sana wito huu: “UUE!” Na ni wazi kwamba jambo hilo hasa ndilo washirika wa viibada vya kishetani wamekuwa wakifanya.

Mtu mmoja alieleza sababu zao za kufanya jeuri: “Kuingilia wanawake kinguvu ni kwa kusudi la kumzindua bikira, jambo ambalo lina maana maalumu kwa waabudu wa Shetani. Kuteketeza vitu ovyo-ovyo ni ufananisho wa ule mteketezo mkubwa, au Har–Magedoni, na visa vya kuua kimakusudi hufanywa ili vieneze mvurugo na kutimiza unabii katika Danieli: ‘Lakini waovu watatenda kwa uovu.’”

Kutazama imani fulani za waabudu wa Shetani hufunua pia kwamba wao huamini ya kuwa Adolf Hitler hustahili kuabudiwa. Kwa uhakika, mwandikaji mmoja alisema hivi: “Wao huuona uharibifu ulioletwa na Hitler kuwa mwonjo tu wa ule unaokuja—nao hutaka kuwa tayari kwa tukio kubwa hilo.”

Ni nini sababu kuu ya kumkweza Hitler? Mwandishi wa habari za uchunguzi Maury Terry aeleza kwamba sababu moja “ilikuwa jedwali-wakati yenye namba nyingi ambamo kila herufi ya alfabeti iligawiwa namba fulani. Chini ya mfumo huo, A ilikuwa sawa na 100 na Z ililinganishwa na 125. Namba ambazo zililingana na herufi zilizo katika jina la mwisho la Hitler (107, 108, 119, 111, 104, 117) zilijumlika kuwa 666—ile namba ya hayawani mkubwa wa kitabu cha kibiblia cha Ufunuo. Ile namba ya ibilisi.”

Hiyo husaidia kueleza ni kwa nini namba 666 hutumiwa kwa mapana, kupakwa katika kuta za mahali pa mikutano ya koveni au kuta za peupe na madaraja. Herufi HT na HH husemwa kuwa humsimamia Hitler, na zile radi za SS ya Ujeremani husemwa kuwa hufananisha “mbinguni hadi helo [moto wa mateso], uwezo.” Ile swastika (msalaba) hutumiwa na waabudu wa Shetani pia. “Zote ni alama za yule hayawani, Shetani-Hitler, ambao wao humtumikia,” akasema mfuasi mmoja.

Mikutano Huleta Jeuri

Yaripotiwa kwamba kuna pindi maalumu zaidi ya 20 za mikutano ya koveni wakati wa mwaka. Mingi yayo hufanyika katika nyakati zinazolingana na za ile iitwayo miadhimisho ya Kikristo eti. Hiyo ni kupatana na jambo ambalo wao huliona kuwa njia ya kuyatia unajisi mambo yote ambayo huonwa kuwa mema na matakatifu. “Halloween” ni sikukuu ya kishetani iliyo ya maana. Mikutano au sabati zao hufanywa mahali pa siri, ambapo huenda pakabadilika kulingana na hali. Terry aliandika kwamba, “Kabla ya kila mkutano wa koveni huwa ni lazima Shetani atulizwe kwa kitendo cha kuingilia bikira [msichana mchanga] kinguvu, kufanya teketezo, au kuua mtu au mnyama kwa desturi ya ibada.”

Dhabihu ya mbwa na paka ni jambo kubwa kwa kiibada hicho. Kwa kielelezo, katika mahali pamoja karibu na Jiji la New York, mbwa 85 waitwao “German shepherds” na “Dobermans” walipatikana katika kipindi kimoja cha miezi 12, ikifikiriwa kwamba wote hao walitendwa hivyo na Wanashetani. Mara nyingi, sehemu za mwili huondolewa na kuliwa kwa imani ya kwamba zina nguvu za kufanya mizungu ya kiuchawi. Damu hupitishwa kwa kuzungushwa na kunywewa kutokana na vikombe vya fedha vilivyoibwa makanisani—hayo yote yakiwa ni sehemu ya ibada ya Shetani. Bila shaka, dhabihu ya kibinadamu huonwa kuwa ndilo toleo kubwa kabisa ambalo humfurahisha hata zaidi. Na mara nyingi yeye hutulizwa kwa njia hiyo.

Lakini Shetani huyu ni nani? Je! kweli yeye yuko? Au ni uwazio tu wenye kufuatwa kwa juhudi ya kupita kiasi?

[Sanduku/Picha katika ukurasa wa 15]

Kutoa Dhabihu Ili Kumtuliza Ibilisi

Aprili uliopita ulimwengu ulishtuliwa na ugunduzi wa masalia ya wanaume kumi na wawili waliokuwa wameuawa kidhabihu nje ya jiji la Matamoros la Meksiko, karibu na mpaka wa Texas. Gazeti Time liliripoti hivi:

“Ili wajipendekeze kwa ibilisi, wauaji hao walichemsha bongo na mioyo ya mihanga wao, huku wakichanganya mchemko huo pamoja na mifupa ya miguu na mikono na vichwa vya wanyama. Hao waabudu wa ibilisi walikuwa wakatili sana hivi kwamba iliwachukua wastadi wawili wa kukagua maiti . . . karibu siku nne kumaliza kuchunguza jinsi maiti hizo zilivyouawa.”

Hao waabudu wa Ibilisi waliamini wangepokea ulinzi kutoka kwa mungu wao wakimtuliza kwa dhabihu za kibinadamu. Luteni wa polisi alisema kwamba wauaji hao walisali kwa ibilisi “ili polisi wasiwakamate, ili risasi zisiwaue na ili waweze kupata pesa zaidi.”

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki