Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g90 6/8 kur. 24-29
  • Polandi Yakaribisha Mashahidi wa Yehova

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Polandi Yakaribisha Mashahidi wa Yehova
  • Amkeni!—1990
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • ‘Ulimwengu Mpya Tu Ndio Bora Zaidi’
  • Udugu Wenye Umoja
  • Usimulizi Mzuri Kwenye Vyombo vya Habari
  • Ubatizo
  • “Ndiyo Tamati Kamili”
  • “Mashahidi wa Yehova Kutoka Urusi Siku Nyangavu Zaidi Ziko Mbele”
    Amkeni!—1992
  • Mikusanyiko Uthibitisho wa Udugu Wetu
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
  • Ujitoaji Kimungu—Una Manufaa kwa Mambo Yote
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Kitabu-mwaka cha Mashahidi wa Yehova 1990
    1990 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—1990
g90 6/8 kur. 24-29

Polandi Yakaribisha Mashahidi wa Yehova

KATIKA Agosti 1989, wonyesho wenye kutokeza sana wa amani na umoja wa kimataifa ulitukia katika Polandi. Pindi yenyewe ilikuwa ni “Ujitoaji Kimungu” Mikusanyiko ya Mashahidi wa Yehova iliyofanywa katika miji ya Polandi ya Poznan na Chorzów, Agosti 4-6, na katika Warsaw, Agosti 11-13.

Ni nini kilichofanya mikusanyiko hiyo kuwa maalum sana? Katika nyakati za ki-siku-hizi Mashahidi wa Yehova wamekuwa na mikusanyiko ambayo imekuwa mikubwa zaidi, iliyochukua muda mrefu zaidi, na iliyowakilishwa na mataifa mengi zaidi. Lakini watu zaidi ya 166,000 watakuambia kwamba ni mara chache kuwa na mikusanyiko ambayo imesababisha idili nyingi hivyo, ikadhihirisha umoja wa Kikristo, au kuwa na wonyesho wa kusukumwa na moyo wa upendo wa Kikristo.

‘Ulimwengu Mpya Tu Ndio Bora Zaidi’

Wajumbe walitoka angalau mataifa 37, pamoja na watu mmoja mmoja kutoka mengine mengi. Washiriki watano wa Baraza Linaloongoza la Mashahidi wa Yehova walishiriki katika programu. Wageni zaidi ya 12,000 walitoka Ulaya ya Magharibi, United States, na Japani, na kufanya hiki kiwe kikundi kikubwa zaidi cha wasafiri wa kimataifa kilichopata kushughulikiwa katika Polandi.

Maelfu mengine walitoka Urusi na Chekoslovakia, na pia nchi nyingine za Ulaya ya Mashariki. Huu ndio uliokuwa mkusanyiko wa kwanza kabisa kwa wengi wa wajumbe hawa, ingawa wengi wamekuwa Mashahidi kwa miaka 30 au zaidi. Hisia za hao ambao kwa mara ya kwanza waliweza kukusanyika na ndugu zao Wakristo zaweza kujumlishwa kwa kufaa na mjumbe mmoja kutoka Kazakhastan, Urusi, aliyesema:

“Kwa miaka mingi tumekuwa tukingojea siku hii, na sasa tupo hapa kwenye mkusanyiko huu wa kimataifa. Twaona vigumu kufahamu yote haya na kuamini. Ni kama ndoto. Haiwezekani kueleza kwa maneno kila kitu tulichoona na kusikia. Tulipoona uwanja huu mkubwa, wenye umbo la bakuli umejaa watu na kusikia muziki, macho yetu yalijaa machozi. Na sala—wakati sisi sote tulipokuwa tumeungana tukiwa zizima—ilitutia hofu. Ilikuwa yenye uzito sana na ya kauli moja. Mkusanyiko huu katika Warsaw ni tukio murua (bora sana) na tukufu hivi kwamba ulimwengu mpya tu ndio utakuwa bora zaidi. Sikuzote sisi tutakumbuka siku hizi nzuri ajabu.”

Walipoelekeana kwenye mikusanyiko na makumi ya maelfu ya Mashahidi wenzao, wengi wa wageni hawa kwa wazi waliguswa moyoni. Katika Warsaw walipiga vifijo na nderemo zilizosambaa kwenye uwanja wote kwa dakika zaidi ya tano. Ni kama mjumbe mmoja kutoka Ulaya ya Magharibi alivyotamka: “Katika dakika hiyo, ni wachache waliokuwa wakifikiria juu ya hali ya hewa yenye joto au mabenchi magumu au kwenda nyumbani kwenye viti vyororo. Walitaka maagizo zaidi na ushirika wenye upendo.”

Kila siku ripoti zilitolewa na wajumbe wa kigeni, ambao walisimulia mambo yaliyoonwa kutoka nchi zao. Ya mwisho ya ripoti hizo 24 katika Warsaw aliachiwa mjumbe kutoka Urusi. “Sisi hatuna maneno ya kutosha kueleza shangwe yetu kwamba twaweza kuwa miongoni mwenu,” akaanza. “Tunathamini sana kwamba wengi wetu sana wameweza kuja hapa na kwamba tumepokewa kwa ukaribishaji mkubwa nanyi. Pia tunashangilia kuweza kukutana kibinafsi na wengi sana kati yenu ndugu. Baadhi yetu tumetoka sehemu za mbali sana, kama vile Vladivostok kwenye pwani ya Bahari Pasifiki, mwendo wa garimoshi wa siku sita. Baadhi yetu tulikuwa na matatizo ya kupata tiketi kwa sababu wengi sana walitaka kufunga safari wakati uo huo, na kulikuwako viti vichache tu. Lakini kwa msaada wa Yehova, tukafika.”

Kwa kufaa, katika maelezo yake ya kumalizia Jumapili, mshiriki mmoja wa Baraza Linaloongoza alishukuru serikali za Ulaya ya Mashariki kwa kuruhusu wengi sana wa Mashahidi wa Yehova kutoka nchi zao wahudhurie mikusanyiko hiyo.

Udugu Wenye Umoja

Katika kueleza mambo aliyoona kwenye mikusanyiko ya Polandi, dada mmoja Shahidi alisema: “Ilikuwa kinyume cha Babeli.” Ingawa mvurugo na mafarakano yalitokea kwenye Mnara wa Babeli watu walipoanza kusema lugha tofauti-tofauti, hapa kulikuwako udhihirisho mzuri sana wa umoja katika wazo, mwenendo, na vitendo, ijapokuwa tatizo la lugha.—Mwanzo 11:1-9.

Umoja huo kati ya waamini wenzi wa mataifa tofauti-tofauti haukukosa kuonwa na watu wa nje. Kichapo Sztandar Mtodych kilisema: “Abiria wa ndege pekee waliokuwa wanawasili kwenye uwanja-ndege wa Warsaw ambao hawakuwa wamevurugika wala kupotea katika umati walikuwa ni Mashahidi wa Yehova. Waamini wenzao walikuwa wametayarisha matangazo katika lugha nyingi, dawati za kutoa habari, na vibao vya ishara na waliandaa usafirishaji kwenda mjini.”

Uimbaji kwenye mikusanyiko hiyo ulikuwa jambo la kutokeza, huku makumi ya maelfu wakiimba kwa umoja katika lugha 20 tofauti-tofauti, wote wakisema mawazo yale yale katika roho ya upendo na umoja. Pia, katika Warsaw visehemu vya programu vilitafsiriwa katika lugha 16 (kule Poznan katika 13 na kule Chorzów katika 15). Hilo lilikuwa halijapata kufanywa tena hapo mbeleni katika Polandi.

Watafsiri hao 16 walisimama kwenye uwanja moja kwa moja mbele ya kikundi cha lugha fulani yao. Mnenaji alinena kutoka jukwaani, na kila mtafsiri alitafsiri katika lugha ya wasikilizaji katika kisehemu hicho cha uwanja. Vipaaza-sauti vilivyoelekezwa moja kwa moja kwenye kisehemu hicho cha lugha viliwezesha mtu kusikia lugha yake mwenyewe bila ya kuvurugwa isivyofaa na tafsiri zilizokuwa zikitolewa katika lugha nyinginezo katika visehemu vile vingine.

Yajapokuwapo matatizo makubwa ya kiuchumi katika Polandi, maelfu ya wageni waliandaliwa mahali pa kulala pa watu binafsi na ndugu zao Wapolandi. Elfu kumi na sita walilazwa na akina ndugu katika Poznan, 21,000 katika Warsaw, na 30,000 katika Chorzow. Jamaa moja ilitoa makao kwa watu 18 na kulisha 21. Na kundi moja la Mashahidi 146 lililaza watu 1,276!

Usimulizi Mzuri Kwenye Vyombo vya Habari

Televisheni, radio, na ripoti za magazeti kwa sehemu kubwa zilisimulia kikweli na bila upendeleo. Kikisema katika kichwa cha habari kwamba “Mashahidi wa Yehova Huzoea Dini Yao Katika Nchi 212,” kichapo cha Polandi Sztandar Mtodych kiliwasifu kwa kutumia katika makala yacho vichwa vidogo kama, “Bila Kigeu-geu,” “Wenye Utaratibu,” “Wenye Kiasi,” na “Wenye Bidii ya Kazi.” Kuhusu uwanja katika Warsaw, kilisema: “Hakuna hata kigutu kimoja cha sigara au kipande cha karatasi kilichotupwa na mtoto mwasi. Mashahidi wa Yehova hawavuti sigara, na watoto wao si waasi.”

Gazeti Zycie Warszawy lilitaja kwamba matayarisho ya mkusanyiko yalikuwa yameendelea kwa mwaka mzima na kusema: “Kati ya mambo mengine, nyanja ambamo mikusanyiko ilifanyika zilitengenezwa hali upya.”

Gazeti Express Wieczorny liliripoti: “Jambo lililovutia watazamaji wote lilikuwa ni utaratibu uliokuwa kwenye uwanja wote. Utupaji wa takataka kwenye sehemu zilizowekwa, vyoo vya muda lakini safi, vibanda vingi vya kutoa habari—yote hayo yalistaajabisha.” Ili kutimiza hilo Mashahidi zaidi ya 3,500 walitumia wakati kutayarisha na kurembesha uwanja wa Warsaw.

Gazeti hilo pia lilihoji baadhi ya wajumbe, likiwauliza: “Mkusanyiko wa Warsaw ulimaanisha nini kwako?” Shahidi mmoja Mpolandi alisema: “Nimeguswa moyo na uhakika wa kwamba niliweza kukutana na ndugu zangu kutoka Chekoslovakia na Urusi, nchi ambazo katika hizo Mashahidi wa Yehova hawajatambuliwa kirasmi kuwa shirika la kidini.”

Na Shahidi mmoja kutoka Urusi alinukuliwa kuwa alisema: “Mimi nafikiri ndilo tukio kuu zaidi maishani mwangu. . . . Kwa mara ya kwanza maishani mwangu niliweza kukutana na wengi sana wa ndugu zangu kutoka ulimwenguni pote. Na zaidi mkutano huu ulikuwa umepangwa vizuri sana; hotuba zilitafsiriwa katika lugha 16, ndugu zetu Wapolandi walikuwa wakaribishaji wetu—hakika kila jambo lilikuwa zuri sana.”

Zycie Warszawy lilisema: “Mkusanyiko wa ulimwengu wa Mashahidi wa Yehova katika Warsaw sasa umekwisha. . . . Kutayarishwa kwa mikusanyiko hiyo kuliwezeshwa, kama tukumbukavyo, baada ya Shirika la Kidini la Mashahidi wa Yehova katika Polandi—sasa lenye waamini zaidi ya 80 elfua—kusajiliwa miezi kadhaa iliyopita. Tangu Mei 12 kikundi hiki ambacho hapo awali kilikuwa haramu kimeonea shangwe kukubaliwa kisheria.”

Likiita mikusanyiko ya Mashahidi wa Yehova “udhihirisho wa umoja,” gazeti hili lilisema kwamba “kwa habari ya utaratibu, kuwa na amani, na hali ya usafi, washiriki wa mkusanyiko ni vielelezo vya kuigwa.”

Ubatizo

Kila mtu, awe aliweza kuzungumza Kipolandi au la, alivutwa sana na tamasha yenye kusisimua ya ubatizo. Katika Warsaw hesabu kubwa ya viti ilikuwa imewekwa kwenye uwanja wa kucheza pale karibu tu na jukwaa ili wale ambao wangebatizwa waketi. Lakini wakati wa programu ya asubuhi, ilisisimua kuona wakaribishaji wakifanya haraka kupeleka viti vya ziada kwenye uwanja kwa kuwa kikundi cha wenye kutaka kubatizwa kiliendelea kuongezeka. Halafu, wakati wa kuanza kwa hotuba ya ubatizo, umati huo mkubwa wa wasikilizaji ulinyamaza. Walikuwa wanakaribia kujionea kitu ambacho hawatasahau kamwe. Msemaji alipowaalika wenye kubatizwa, uwanja wote ulipiga vifijo kwa kusukumwa na moyo. Halafu, kama kwamba ni kwa ishara iliyokuwa imetanguliwa kupangwa, lakini kwa kweli likiwa ni jambo lililochochewa na mioyo iliyofurika yenye kusukumwa na roho ya Mungu, hao wenye kubatizwa waliitikia kwa shauku wakipunga mikono yao katika kusalimu wasikilizaji waliojaa pomoni na kuwazunguka.

Julisho-wazi la imani la hao wenye kutaka kubatizwa katika kujibu yale maswali mawili yanayoulizwa wenye kubatizwa kwa ujumla lilisikiwa waziwazi na kwa kuazimia—na kweli kweli wengi wao walikuwa wamefikia hatua hii ya wakfu kupitia shida na majaribu mengi. Baada ya sala, wenye kubatizwa walitenganishwa katika vikundi viwili na wakatembea kutoka uwanjani huku wasikilizaji wakiimba “Walio Wakfu kwa Yehova.” Akina ndugu walitoka uwanjani kupitia njia ya chini ya ardhi yenye kuongoza kwenye vyumba vyao vya kuvalia, nao akina dada walipitia njia nyingine ya chini ya ardhi ikiongoza kwenye vyumba vyao. Wakaribishaji na wazamishaji, wote wakiwa wamevaa mavazi meupe, wakatwaa vikao vyao, na mara moja wataka kubatizwa, waliovalia mavazi ya kuogelea yenye kiasi, wakaanza kumiminika kurudi kwenye uwanja, ambamo vidimbwi 12 vya ubatizo vilikuwa vimewekwa, 6 upande mmoja wa uwanja kwa ajili ya akina dada, na 6 upande ule mwingine wa uwanja kwa ajili ya akina ndugu.

Vifijo vyenye idili viliendelea kwa dakika 45 ambazo katika hizo 1,905 walibatizwa katika Warsaw. (Juma lililotangulia, 1,525 walikuwa wamebatizwa kule Poznan na 2,663 kule Chorzow, ikawa jumla kuu ikawa 6,093, au asilimia 3.7 ya kilele cha hudhurio.) Angalau ndugu wawili waliolemaa waliinuliwa kwa upendo kutoka kwenye viti vyao vyenye magurudumu kabla ya kubatizwa, kutia mmoja ambaye alikuwa ameletwa kwenye uwanja akiwa juu ya machela ili asikilize hotuba ya ubatizo.

“Ndiyo Tamati Kamili”

‘Yote hayo yasikika kuwa ya kuamsha hisia za moyo sana,’ huenda ukasema. Ndivyo ilikuwa! Lakini si aina ya hisia-moyo unayokuta kwenye mihuisho ya dini za Jumuiya ya Wakristo. Hisia-moyo ya wahudhuriaji wa mikusanyiko ya Polandi ilitegemea maarifa sahihi ya Neno la Mungu, kwa hiyo waliohudhuria wangekuwa na vifaa bora zaidi vya kutumikia Mungu baadaye. Ilikuwa hisia-moyo iliyochochewa na maarifa kwamba baada ya miongo mingi ya upinzani, Mashahidi katika Polandi walikuwa sasa hatimaye wanaweza kukusanyika kwa uhuru pamoja na waamini wenzao kutoka nchi jirani. Ilikuwa hisia-moyo yenye kumotishwa na shangwe ya kujua kwamba mjumbe aliyeketi kando yako labda alikuwa hajapata kuhudhuria mkusanyiko hapo mbeleni na kwa hakika si wa ukubwa huo. Ilikuwa hisia-moyo yenye kutokana na uthibitisho mkubwa wenye kuonekana kwamba Mashahidi wa Yehova ndio udugu mmoja ulioungana wa kimataifa unaotumikia Mungu aliye hai wa ukweli.

Mjumbe mmoja kutoka Ulaya ya Magharibi alijumlisha hayo kwa kusema: “Ijapokuwa nilikuwa nimehudhuria kila mkusanyiko tangu 1952, kwa habari ya mazingira ya idili, shangwe, upendo, uthamini, na shukrani, hili lilikuwa ndiyo tamati kamili.”

Bila shaka hisia-moyo ilifikia tamati katika Warsaw siku ya Jumapili wakati wa sala ya mwisho. Ingawa maelfu hawangeweza kuyaelewa maneno yayo, kila mtu alihisi roho , upendo, wakfu, utukuzo, utambuzi wa kutoka moyoni kwa Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, na azimio la kuendelea katika kazi ya Yehova ambayo tumejulishwa. Kimya yenye kutia hofu huku vichwa vipatavyo 60,000 vimeinama katika sala kwa Mungu wao kilikatizwa tu na vilio vya shangwe yenye uthamini. Sala ilipomalizika, hakuna aliyeona shida kusema “Amina” kutoka kwenye kina cha moyo wake. Kulifuata vifijo vya hiari ambavyo mwangwi wavyo ulisikika kwenye kusanyiko hilo kubwa kwa dakika zaidi ya 11.

Watu zaidi ya 166,000 walikuwa wamekuwa mashahidi wa kujionea kwa macho yao historia ya kitheokrasi ikifanyizwa katika Polandi. Kabla mfumo mbovu wa Shetani haujaanguka katika uharibifu wao wa mwisho, historia zaidi itafanyizwa—historia yenye kusisimua, yenye kustaajabisha, yenye kutia hofu ambayo tamati yayo itakuwa kuondolewa lawama kwa enzi kuu ya Yehova. Na ikiwa wewe unachagua, unaweza kuokoka kuwa sehemu ya historia hiyo. Je! utafanya hivyo?

[Maelezo ya Chini]

a Kadirio la gazeti hilo.

[Sanduku katika ukurasa wa 25]

MAMBO YA KIMAENDELEO YENYE KUTOKEZA HISTORIA

1928 Mashahidi 300 wa Polandi wafanya makusanyiko yao ya kwanza madogo.

1939 Vita ya Ulimwengu ya Pili inapoanza, Mashahidi 1,100 wanahubiri; wengi wafungwa gerezani, na wengine wafa katika kambi za mateso za Ujeremani.

1945 Kufikia mwisho wa Vita ya Ulimwengu ya Pili, hesabu ya Mashahidi imekuwa zaidi ya maradufu kufikia 2,5000.

1946 Mnamo Juni, 1,500 wahudhuria kusanyiko karibu na Lublin; 298 wabatizwa. Katika Septemba 5,600 wahudhuria kusanyiko katika Katowice.

1947 Mkusanyiko mmoja katika Kraków wahudhuriwa na 7,000; 476 wabatizwa. Wahitimu wawili wa Gileadi wawasili ili kusaidia kuipanga kazi ya kuhubiri kitengenezo.

1950 Kilele cha Mashahidi 18,000 chafikiwa katika Machi. Ukumbusho wahudhuriwa na 24,000. Katika Julai kazi yapigwa marufuku, na kufanya iwe lazima kufanya mikutano midogo katika nyumba za watu binafsi.

1968 Mikusanyiko ya wilaya ya siku moja yafanywa kwanza katika misitu kukiwako watu 100 au 200; baadaye, wengi kama 1,000 wahudhuria.

1980 Karibu Mashahidi 2,000 kutoka Polandi wasafiri kwenda Vienna, Austria, kwa ajili ya mkusanyiko wa wilaya.

1981 Mkusanyiko mkubwa hata zaidi ya ule wa 1980 wafanywa katika Vienna kwa ajili ya ndugu Wapolandi.

1982 Serikali ya Polandi yawapa Mashahidi ruhusa ya kukodisha majumba na nyanja kwa ajili ya makusanyiko ya siku moja.

1985 Mikusanyiko ya siku tatu iliyohudhuriwa na watu zaidi ya 94,000 yafanyiwa Polandi. Kuna mamia ya wageni kutoka nchi 16, kutia washiriki wanne wa Baraza Linaloongoza.

1989 “Ujitoaji Kimungu” Mikusanyiko ya Wilaya yafurika kwenye nyanja tatu, washiriki watano wa Baraza Linaloongoza wakihudhuria; jumla-hudhurio 166,518, na 6,093 wabatizwa. Trakti mbili zatolewa katika Kipolandi, Mashahidi wa Yehova Wanaamini Nini? na Sababu kwa Nini Unaweza Kuitumaini Biblia, na pia broshua yenye kurasa 32 Should You Believe in the Trinity?

[Picha katika ukurasa wa 27]

Wataka kubatizwa kule Warsaw wameketi mbele ya jukwaa, na umati ukitazama ubatizo wao

[Picha katika ukurasa wa 29]

Kipande cha kisehemu kilichowekwa kando kule Chorzów kwa ajili ya wajumbe kutoka Urusi, na baadhi ya mabasi yaliyosafirisha Mashahidi kuwapeleka Poznan

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki