Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g91 2/8 kur. 8-9
  • Kwa Nini Ile Migawanyiko?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kwa Nini Ile Migawanyiko?
  • Amkeni!—1991
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Theolojia au Ukweli wa Biblia?
  • Jamii ya Viongozi wa Dini Waliogawanyika
  • Kagawanyika Kisiasa
  • Kwa Nini Ule “Wasiwasi Mwingi”?
    Amkeni!—1991
  • Mtengano Mpya
    Amkeni!—1991
  • Kanisa—Mabadiliko na Mvurugo
    Amkeni!—1993
  • Kwa Nini Kanisa Linapoteza Uvutano?
    Amkeni!—1996
Amkeni!—1991
g91 2/8 kur. 8-9

Kwa Nini Ile Migawanyiko?

KISABABISHI kilicho msingi wa migawanyiko, au mitengano, ya kidini, kimepangiliwa katika ensaiklopedia moja ya dini kuwa chenye sehemu tatu: ya kimafundisho, ya kitengenezo, na ya kisiasa. Acheni tuone kama uchanganuzi huu unalingana na hali iliyo katika Kanisa Katoliki.

Theolojia au Ukweli wa Biblia?

Katika uchanganuzi wake mwenyewe wa sababu ya migawanyiko ya sasa katika Kanisa Katoliki, padri René Laurentin aliandika hivi: “Kisababishi chenye kuamua kinaonekana kuwa wazi kwangu. Hicho ni mawazo yenye kutofautiana.” Yeye anasema juu ya wazo la maendeleo. Hili linapingana na pokeo, yaani, ule udumishaji wa desturi za zamani uliotolewa mfano na Askofu Mkuu Lefebvre. Mdominika wa nyumba ya kitawa Jean-Pierre Lintanf anasema hivi: “Imani ni moja, theolojia ni za namna mbalimbali.”

Mawazo tofauti-tofauti, yenye kuleta migawanyiko ndani ya kanisa, yangeweza kuepukwa ikiwa kanisa lingeshikamana na Biblia kuwa chanzo cha mafundisho yalo. Kwa kweli, Baraza la Vatikani la Pili liliamrisha hivi: “Lile Neno takatifu ni chombo chenye thamani katika mkono hodari wa Mungu kwa ajili ya kufikia mwungamano ule ambao Mwokozi anatolea wanadamu wote.” Hata hivyo, likiibomoa thamani ya Biblia yenye kuungamanisha, hilo hilo Baraza la Vatikani lilisema hivi: “Kanisa halichukui uhakika walo juu ya kweli zote zilizofunuliwa kutokana na Maandiko matakatifu tu. Basi, Andiko na Pokeo ni lazima vikubaliwe vyote viwili na kuheshimiwa kwa maoni sawasawa ya ujitoaji na kicho.” Na tena: “Theolojia takatifu inategemea Neno la Mungu lililoandikwa, likichukuliwa pamoja na Pokeo takatifu.”

Maneno ya Yesu kwa Mafarisayo yangefaa kutumiwa kwa wenye mamlaka ya mafundisho katika Kanisa Katoliki: “Nyinyi mmefanya neno la Mungu likose matokeo kwa njia ya pokeo lenu.” (Mathayo 15:6, The New Jerusalem Bible) Mwanamke mmoja Mkatoliki mwenye moyo mweupe aliandikia hivi gazeti moja la Kikatoliki katika Ufaransa: “Ikiwa makasisi hawana tena kichocheo cha kulihubiri lile Neno Jema, je! inashangaza kwamba waaminifu ni wachache zaidi katika idadi, au wanatafuta mahali penginepo? (Kwa habari ya Mashahidi wa Yehova na watetea mapokeo, imani yao inafanya wawe tofauti.)”

Jamii ya Viongozi wa Dini Waliogawanyika

Sasa fikiria kisababishi cha kitengenezo kwa migawanyiko iliyo ndani ya kanisa. Mtengano ulioletwa na Askofu Mkuu Lefebvre ulihusiana moja kwa moja na mafundisho rasmi ya Kikatoliki juu ya “Uhalifa wa Kimitume” na cheo cha papa. Lefebvre anadai kwamba “uwezo wa kufundisha, kutawala, na kutakasa ambao Kristo aliweka juu ya Mitume Wake . . . unaendelezwa daima katika jamii ya maaskofu wa Kanisa.” Kwa upande mwingine, inadaiwa kwamba askofu wa Roma, yule papa, ndiye “wa kwanza kati ya maaskofu wote, si katika cheo au fahari tu, bali pia katika mamlaka ya kiuchungaji.”—New Catholic Encyclopedia.

Lakini je! mafundisho rasmi haya yana msingi wa Biblia? Ensaiklopedia ii hii ya Biblia inakiri kwamba “mtu hapati katika Agano Jipya maneno yoyote ya Kristo yenye kuonyesha jinsi amri ya kimitume ilivyopasa kupokezanwa.” Na pia inakubali kwamba “cheo cha papa” ‘hakikueleweka wazi wala kutajwa wazi’ katika “Kanisa la Magharibi [la Kilatini]” mpaka karne ya tano W.K.

Kwa sasa mfumo wa jamii ya viongozi wa Kanisa Katoliki unapingwa kutoka juu kufika chini. Hicho ni kisababishi kimoja katika ile migawanyiko, wakati maaskofu, wanatheolojia, mapadri, na watu wa kawaida wanapoeleza kutokubaliana kwao na papa juu ya mambo ya imani, maadaili, na serikali ya kanisa. Lile “Julisho Rasmi la Cologne” lilisema hivi: “Ikiwa papa anafanya yale yasiyo ya cheo chake, hawezi kudai utii kwa jina la Ukatoliki.”

Kagawanyika Kisiasa

Economist la Uingereza liliandika hivi: “Kama vile yalivyo maoni ya wafuasi wa Lefebvre, kanisa lao limeshikwa na hila ambayo imeliingiza mikononi mwa wafuasi wa Marx, wamamboleo na Waprotestanti. Monsinya Lefebvre anaamini yale Mapinduzi ya Ufaransa yalianzisha umamboleo na mfunguko wa akili wenye kuleta masikitiko ulimwenguni, na kwamba Vatikani 2 ilianzisha yale Mapinduzi ya Ufaransa . . . ndani ya kanisa.” Wakatoliki wengi wa bawa la kulia wanashiriki maoni haya. Kwa upande mwingine, Wakatoliki wa bawa la kushoto wanapendelea marekebisho ya kijamii, wengine wao wakifikia hatua ya kuikubali kanuni ya mapinduzi ya kutumia silaha. Hivyo, siasa ni kisababishi kingine cha mgawanyiko miongoni mwa Wakatoliki.

Akimalizia makala yake juu ya “Kwa Nini Migawanyiko Hii Miongoni mwa Wakristo?” padri Laurentin alisema kwamba kuaminika kwa Kanisa Katoliki kungetegemea kujipatanisha kwalo na maneno ya Yesu: “Ni kwa upendo wenu kwa mmoja na mwenzake, kwamba kila mmoja atatambua nyinyi kuwa wanafunzi wangu.”—Yohana 13:35, NJB.

Wakitumia kiwango hicho, Wakatoliki wengi wenye moyo mweupe kotekote ulimwenguni wamekata shauri kuwa dai la Kanisa Katoliki kwamba hilo ndilo kanisa moja la kweli haliaminiki. Kwa kufahamu, kama vile Yesu pia alivyosema, kwamba “hakuna nyumba iliyogawanyikana yenyewe inayoweza kudumu,” wengi ‘wametoka mzofafa’ (po-le-po-le) katika kanisa.—Mathayo 12:25, NJB.

Idadi kubwa kutosha ya Wakatoliki sasa wanatafuta “nyumba” yenye Wakristo wa kweli, ambao wameungamanishwa na upendo halisi wa kidugu na ambao hawagawanywi ama na mafundisho rasmi yasiyo ya Kibiblia, jamii ya viongozi wasio na mwungamano, ama na maoni ya kisiasa yenye kupingana. Maelfu wamekipata walichokuwa wakitafuta wakati walipoanza kushirikiana na Mashahidi wa Yehova.

[Picha katika ukurasa wa 9]

Yesu aliwalaani vikali Mafarisayo kwa kuweka mapokeo yao juu ya Neno la Mungu

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki