Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g92 7/8 kur. 17-19
  • Kwa Nini Ni Lazima Niwe Mtunza-Mtoto?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kwa Nini Ni Lazima Niwe Mtunza-Mtoto?
  • Amkeni!—1992
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • ‘Je! Mimi Ni Mlinzi wa Ndugu Yangu?’
  • ‘Kwa Nini Mimi’?
  • Kupata Maoni Yanayofaa
  • Nawezaje Kuwa Mtunza-Mtoto Mzuri?
    Amkeni!—1992
  • Nawezaje Kuwa Kiolezo kwa Ndugu na Dada Zangu Wachanga?
    Amkeni!—1992
  • Kwa Nini Ni Lazima Niwe Kielelezo kwa Ndugu na Dada Zangu Wadogo Zaidi?
    Amkeni!—1990
  • “Kwa Vinywa vya Watoto”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—1992
g92 7/8 kur. 17-19

Vijana Wanauliza. . .

Kwa Nini Ni Lazima Niwe Mtunza-Mtoto?

“UNAHISIJE kuhusu kutunza ndugu na dada zako wachanga?” Amkeni! iliuliza swali hili vijana kadhaa. Maitikio yalikuwa uamuzi uliochanganyika.

“Napenda watoto wadogo.” akasema msichana mmoja tineja, “kwa hivyo hakuna shida.” Mvulana mmoja tineja hata alijigamba: “Mimi nafurahia uwezo huo!” Wengine, hata hivyo, walionyesha waziwazi kutopendelea—au kuchukia. “Nafanya hivyo kwa kuwa najua wazazi wangu wanahitaji msaada,” akaeleza msichana mchanga. “Lakini sina furaha kuhusu hilo.” Akasema msichana mwingine: “Mimi wakati mwingine ningependa kwenda sinema au jambo lingine, halafu mama yangu ataniambia, ‘mchukue ndugu yako pamoja nawe.’ Kwa kweli huwa sitaki.”

‘Je! Mimi Ni Mlinzi wa Ndugu Yangu?’

Mwana wa kwanza wa Adamu, Kaini bila huruma aliuliza swali hilo kuhusu ndugu yake Abeli. (Mwanzo 4:9) Na wewe pia huenda ukahisi chuki ikiwa waulizwa kuwa na daraka kwa ajili ya ndugu zako wachanga. Kwa nini wakati wako wa starehe utumiwe kubadilisha nepi au kutunza magoti yaliokwaruzwa? Kama vile msichana wa miaka 15 anavyosema kwa uchungu: “Sina daraka kwa ajili yangu mwenyewe tu bali kwa yale ndugu na dada zangu wanafanya, pia.”

Kijana Marna ana lalamiko tofauti: “Tukienda kwenye bustani kubwa au jambo lingine, kila wakati ni lazima niangalie watoto na siwezi kufurahia. Yanifanya nirukwe akili. . . Wakati niambiapo [mama], anasema, ‘Wewe ndiwe dada mkubwa na wapaswa kuangalia watoto.’ Nikawa na kiruu na kumwambia, ‘labda wangu mwenyewe, lakini si wako! Wewe ndiwe mwenye mtoto sio sisi. Wewe wapaswa kuwaangalia.’”—The Private Life of the American Teenager, cha Norman na Harris.

Wachanga wako wanaweza kuwa wasio na furaha juu ya wewe kuwatunza. Na huenda wakafurahia kuharibu jitihada zako nzuri za kutunza sheria na utaratibu. “Wakati mwingine nachukia kuwatunza ndugu na dada yangu,” msichana mmoja mwenye miaka 14 alikubali kwa Amkeni! “Mambo wanayofanya! Wakati mwingine wao hupigana, nami huamua, nao huniambia, ‘Wafikiri wewe ni nani? Wewe si mama!’ Singejali kama wangekuwa rahisi kushughulika nao.”

‘Kwa Nini Mimi’?

Wakati kikundi kikubwa cha matineja kiliulizwa, “Ni migawo gani ambayo mnafikiri matineja wapaswa kufanya nyumbani?” Kutunza watoto kuliorodheshwa kwa asilimia 32! Ndiyo, madaraka ya kutunza watoto ni halisi kwa maisha ya vijana wa leo. Jambo moja, kazi ya nyumbani huenda ikawa yenye juhudi, yenye kulemeza kwa mama. Akina baba hukabili kazi ngumu ya kila siku mahali pa kazi ya kuajiriwa. Akina mama wengi pia lazima wafanye kazi nyumbani na kazi ya nje. Wao wanakazwa mno mara nyingi.

Mtunza mtoto hufanya iwezekane kwa mama na baba kupata pumziko linalohitajiwa mara kwa mara. Na ikiwa wote wanaenda kazi, mtunza mtoto ataona kwamba watasimamiwa vizuri hadi wazazi watakapofika nyumbani. Kweli, wazazi wako wanaweza kuajiri mtunza mtoto wa nje. Lakini je! hawatahisi usalama zaidi kujua kwamba watoto wao wadogo wako chini ya mikono ya mmoja wa familia yao mwenye kustahili na mwenye upendo?

Ni kweli, daraka la kutunza wachanga wako hatimaye lawaangukia wazazi wako. (Waefeso 6:4) Lakini kusaidia kwako kutunza mtoto kwaweza kutolea wazazi wako msaada watimize wajibu wao. Pia ni njia moja ya “Kuheshimu baba yako na mama yako.” (Waefeso 6:2) Zaidi ya hilo, kutunza mtoto ni zoezi zuri kwa utu mzima. Mwanamke mmoja mchanga akumbuka akitunza ndugu zake na dada yake mchanga wakati mama yake, mzazi mmoja, alifanya kazi akiwa mtumishi wa mezani wa hoteli: “Kila siku ningewaangalia hadi mama arudi nyumbani. Angeniwachia orodha ya mambo ya kufanya: ‘Anika nguo, safisha nyumba, anza kutengeneza chakula cha jioni.” Mzigo kama nini kwa msichana tineja! Lakini asema: “Nikikumbuka hayo naweza kuona kwamba lilikuwa jambo zuri kwangu kufanya katika ulimwengu. Nilikua upesi na nikawa mwenye kuchukua daraka.”

Hata hivyo, hakuna kutokuwa kiume kuhusu mvulana kutunza watoto. Wanaume walifanya hivyo katika siku za Biblia. (Hesabu 11:12) Na mtume Paulo hakuona kuwa jambo lisilofaa kujilinganisha mwenyewe na “mama mlezi.”—1 Wathesalonike 2:7, NW.

Kupata Maoni Yanayofaa

Kujifanya mwenyewe ufurahie kutunza wachanga wako, hata hivyo, huenda kukawa kazi. Kadiri fulani ya mashindano mara nyingi hutokea miongoni mwa ndugu na dada. Na ikiwa daima unagombana na wachanga wako, au ikiwa unawafikiria kuwa kundi la watukutu, inaweza kuwa vigumu kwa wewe kuwa na maoni yanayofaa kuwatunza. Huenda, basi, ikakusaidia ufikirie baadhi ya masomo yanayofundishwa katika Biblia.

Fikiria, kwa mfano, habari ya kijana Yusufu na ndugu zake. Kwa sababu Yusufu alipendelewa na baba yake, ndugu zake “wakaanza kumchukia, na hawakuweza kumnenea kwa amani.” Kisha wazia jinsi Yusufu alihisi wakati baba yake alimwambia: “Je! ndugu zako hawachungi kondoo katika Shekemu? Njoo, nikutume kwao. . . Enenda, basi, ukaone kama ndugu zako hawajambo, na kundi nalo li salama, ukaniletee habari.” Wakazi wa mahali pale bila shaka wangekumbuka machinjo yaliyofanywa na ndugu za Yusufu miaka ya mbeleni huko Shekemu. (Mwanzo 34:25—31) Ingekuwa hatari kwa Yusufu kwenda huko! Si hilo tu, lakini ndugu zake wangekuwa na chuki ya kujionyesha kwake. Ijapokuwa hivyo, kwa ajili ya heshima kwa baba yake na upendo halisi kwa ndugu zake, Yusufu alijibu: “Mimi hapa!” na akakubali huo mgawo.—Mwanzo 37:4, 13, 14.

Miriamu mchanga alikuwa kijana mwenye kutokeza. Wakati Farao wa Misri alitunga shauri la kuwauwa watoto Waebrania, Miriamu alisaidia kumlinda ndugu yake mchanga Musa. Wakati mtoto mchanga huyo alipowekwa kwa usalama katika kisafina na akawa anaelea kwenye mto Naili, Miriamu hakufutilia mbali msiba wa ndugu yake kuwa ilikuwa shida ya mama yake. La, “akasimama mbali ili ajue yatakayompata.” Miriamu hata aliweza kufanya mpango ili mama ya Musa mwenyewe amtunze!—Kutoka 2:4-10.

Ndiyo, tofauti na Kaini, ambaye bila huruma hakujali ndugu yake, vijana wenye kumcha Mungu leo wanahesabu kuwa pendeleo na daraka la kutunza wachanga wao—hata ikiwa ni vigumu na sumbufu. Yohana wa kwanza 4:21 husema: “Yeye ampendaye Mungu, ampende na ndugu yake.” Na wakati hili hasa latumika kwa ndugu wa kiroho, haitakuwa kweli pia juu ya wale ambao tuna uhusiano wa kiroho na kimwili?a

Kuhusika na kupendezwa kwako, tamaa yako ya kulinda, na, zaidi ya yote, upendo usio na kifani kwa wachanga wako unaweza hata kufanyiza sehemu ya maana katika maendeleo yao ya kimwili, kihisia, na kiroho. Bado, kutunza watoto wadogo kwaweza kuwa kugumu, na makala ya wakati ujao itakuwa na madokezo yenye kutumika kukusaidia utunze mtoto kwa kufaa.

[Maelezo ya Chini]

a Sura ya 6 ya kitabu Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi (kilichochapishwa na Watchtower Bible and Tract Society of New York, Inc.) kina madokezo zaidi juu ya kufanyia maendeleo uhusiano na wachanga.

[Sanduku katika ukurasa wa 19]

‘Mimi ni Mkubwa Vyakutosha Kuhitaji Mtunza-Mtoto!’

Wakati Amkeni! iliuliza kikundi kimoja cha vijana wakati mtoto alikuwa mkubwa vyakutosha kuhitaji mtunza mtoto, wengine walidokeza miaka “11,” “13,” na hata “7”! Hata hivyo, msichana mmoja mchanga alisema: “Sifikiri kuna kiwango cha umri. Nafikiri inahusu ukomavu. Unaweza kuwa na umri wa miaka 15 na uwe mchanga sana kuwa bila mtunza-mtoto.”

Bila shaka, kadirio la wazazi wako kuhusu ukomavu wako laweza kuwa mbali sana na lako. Na familia tofauti huenda zikachagua kuchukua mambo tofauti. Kwa hivyo wakati baadhi ya marafiki zako huenda wakawa wanaendesha kazi za nyumba wakati wazazi wao wameenda sinema, huenda ukastahimili “uchungu” wa kuwa na mtunza mtoto. Hili laweza kuwa gumu ikiwa mtunzaji ni ndugu au dada mkubwa. “Sikutaka ndugu yangu anitunze mimi,” alikiri Alisha mchanga. “Sikutaka wakati alikuwa akiniambia la kufanya.”

Wazazi wako, hata hivyo, wana upendezi wako bora mioyoni mwao. Wanasoma katika magazeti juu ya ongezeko la uhalifu na kuwatendea watoto vibaya, na wana sababu nzuri ya kuwa na wasiwasi. Kando na hilo, kuwa peke yako katika nyumba kwaweza kuogopesha zaidi ya unavyokubali. “Nilikuwa nikiogopa sana kuwa peke yangu nyumbani,” akasema msichana mmoja. “Kwa hivyo nikaamua ni afadhali niudhiwe kidogo kuliko kuogopeshwa.”

Ni kweli, wazazi huwadhania watoto wao kuwa wadogo. Na ikiwa yaonekana kuwa hivyo, labda waweza kuwa na mazungumzo pamoja nao na kuwahakikishia kwamba unaweza kuachwa peke yako. Ikiwa utapiga domo na kunung’unika, labda utawaonyesha kutokomaa kwako. Hata hivyo, ikiwa utaongea wazi pamoja nao—kwa mfano, jinsi ungeshughulika na wakati wako na mambo ya dharura—unaweza kuwafanya waone mambo kama unavyoyaona. Ikiwa sivyo, labda masikilizano yenye kukubalika, kama vile kukaa kwenye nyumba ya rafiki, kwaweza kuwa na matokeo.

Bila shaka, huenda wazazi wako bado wakasisitiza uwe na mtunzi. Badala ya kufanya mambo yawe magumu kwako na mtunzi wako, jaribu kumwona yeye kama mwendelezo wa mamlaka ya wazazi wako na ushirikiane naye kama uwezavyo. Vipi ikiwa utumizi mbaya wa uwezo watumiwa kidogo? (“Dada yangu alinitumia kwa kujifaidi,” akaomboleza msichana mmoja.” Alinifanya mimi nifanye kazi zake.”) Huenda ikawa vizuri kungoja hadi wazazi wako warudi nyumbani na kuongea jambo hilo pamoja nao badala ya kuzozana na mtunzi wako.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki