Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w75 1/15 uku. 46
  • “Kwa Vinywa vya Watoto”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Kwa Vinywa vya Watoto”
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Habari Zinazolingana
  • “Kutoka Kinywani mwa Watoto Wachanga”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • Mmoja Aliye Mchanga Amsifu Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Kwa Nini Ni Lazima Niwe Mtunza-Mtoto?
    Amkeni!—1992
  • Mwishowe Mbegu Ilichipuka
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
w75 1/15 uku. 46

“Kwa Vinywa vya Watoto”

YESU Kristo alipopanda kuingia Yerusalemu katika masika ya mwaka wa 33 C.E. kusudi ajitoe mwenyewe kama mfalme, watoto wa kiume hekaluni walipaza sauti: “Hosana, Mwana wa Daudi’.” Kwa kuukubali ufalme wa Yesu kwa njia hiyo, watoto hawa wa kiume walikuwa wanamsifu Yehova, Yeye ambaye alikuwa amemchagua kama mfalme. (Mt. 21:15, 16) Vivyo hivyo, watoto kati ya mashahidi wa Yehova wa Kikristo leo, kwa maneno yao na matendo, wamemletea Muumba wao sifa.

Mtoto mwenye umri wa miaka mitano katika Japan alifundishwa kwa uaminifu na mamaye juu ya makusudi ya Mungu. Lakini baba yake, ambaye si mmoja wa mashahidi wa Yehova, alimpeleka binti yake kwenye chuo cha wafuasi wa Buddha. Hapo mtoto huyu mdogo wa kike alikataa kumsujudia Buddha alipokuwa anaingia mlangoni, wala hakuiabudu sanamu. Mwalimu alimkaripia kwa ukali na vile vile akajaribu kumzuia asimshukuru Yehova mbele ya chakula cha mchana kila siku. Mwishowe mwalimu alijaribu kumlazimisha ashiriki katika Sikukuu ya wafuasi wa Buddha ya Tanabata, lakini ilikuwa kazi bure. Kwa hiyo akauliza: ‘Ni kwa sababu mama yako alikukataza kufanya hivi?’ Yule mtoto wa umri wa miaka mitano akajibu: ‘Hapana, sitaki kufanya hivi kwa maana haimpendezi Yehova Mungu.’ Lo! ni usemi mzuri kama nini kutoka kwa mtoto mdogo!

Juu ya mateso yake kutoka kwa wanafunzi wenzake, mtoto wa kike mwenye umri wa miaka minane kutoka Bolivia anasema: Siku moja wakati wa masomo wenzi wangu shuleni waliamua kunilazimisha niambatane nao kwenye kanisa la Katoliki la mahali hapo tukaone namna lilivyo la kupendeza likiwa na sanamu zake zote na mapambo. Nikawaambia kwamba hata ikiwa kanisa limepambwa vizuri na sanamu, hakuna faida. Sanamu zenyewe zina macho lakini hazioni, miguu lakini haziwezi kutembea, masikio lakini hazisikii na kinywa lakini hazisemi. Wanadarasa wenzangu walinitisha, wakisema: “Tutakapokufa, tutakuvuta miguu yako kusudi kwamba uanguke kwa ajili ya unayoyasema.” Nikawaambia kwamba sikuogopa, kwa maana Biblia inasema kwamba mtu afapo anayarudia mavumbi wala hajui cho chote.

‘Masomo yalipokwisha, walianza kunipiga na kuniangusha chini na, niliposimama, walinitega. Wakaniburuta kwenye mlango wa kanisa. Niliogopa nami nikasali kwa Yehova. Wakanishika nywele zangu, wakaniburuta kanisani kisha wakasema: “Sasa utazitazama sanamu zetu na kufanya tutakayoyafanya.” Wakati uo huo mtu fulani akaingia. Wanadarasa wenzangu wakakimbia, lakini niliweza kusimama mara hiyo na kupasa sauti kwamba nilikuwa ningali mmoja wa mashahidi wa Yehova na nitakuwa hivyo sikuzote.’

Nini kilichomwezesha mtoto huyu wa kike kuushinda mkazo huo kutoka kwa wanadarasa wenzake? Yeye mwenyewe alieleza kwamba ni funzo la Biblia la jamaa la kawaida la kila juma lililoongozwa na wazazi wake lililoitia nguvu imani yake.

Kwamba watoto wanaweza kuwa vyombo vya kuwasaidia wengine waje kwenye ujuzi wa kweli wa Biblia inaonyeshwa na kisa cha mtoto mdogo wa kike wa Canada. Mamaye alianza kujifunza Biblia pamoja na mashahidi wa Yehova na akatiwa moyo ajifunze na bintiye mwenye umri wa miaka mitano, akitumia kitabu Kutoka Paradiso Iliyopotea mpaka Paradiso Iliyopatikana. Mtoto huyu mdogo wa kike alianza kuzungumza na yaya wake juu ya yale aliyokuwa anajifunza. Kwa mfano, alimwambia, ‘Kila mara sisi tunasali mbele ya kula.’ Kwa hiyo naye yaya akaanza kusali kwa Bikira Maria. Lakini yule mtoto wa miaka mitano akamkatiza, akisema kwamba yeye na mamaye wanasali kwa Yehova peke yake. Nyuma ya chakula cha mchana alisisitiza kwamba yaya amsomee kitabu Paradiso. Kwa kadiri alivyozidi kusoma, ndivyo yule kijana yaya alivyozidi kupendezwa. Mwishowe akaanza kumwuliza maulizo mama ya kijana mdogo wa kike. Nyuma ya hapo, yaya huyo akasema na mmojawapo wa rafiki zake naye akasema na jamaa yake. Hii ilileta matokeo ya ajabu. Kwa mwaka mmoja, si kwamba tu mama ya yule mtoto mwenye umri wa miaka mitano alikuwa Shahidi aliyebatizwa wa Yehova, lakini, watu wengine wanne walichukua hatua hii katika utumishi wa Mungu vile vile.

Vile vile watoto wadogo wanashiriki katika utangazaji wa waziwazi wa ujumbe wa Biblia. Katika Afrika ya Kusini James mwenye umri wa miaka minne anakwenda pamoja na mamaye katika huduma ya nyumba kwa nyumba. Kwa kumtanguliza, mamaye anasema: “Kama mashahidi wa Yehova, tunawafundisha watoto wetu Biblia na vile vile tunawazoeza kusema na wengine. Je! ungependa kusikia anachotaka kusema?” Kufikia hapo kila mtu amekuwa akitaka kumsikiliza anapozungumza, ama katika Kiingereza ama Kiafrikaans: “Jina langu ni James, nafanya kazi ya Biblia, nikiwaambia watu habari njema za Ufalme.” Kisha anawaonyesha picha ya kwanza katika kitabu Kweli Iongozayo kwenye Uzima wa Milele, akitoa maelezo machache.

Kwa kweli watoto si wachanga mno wasiweze kujifunza Biblia na kumsifu Yehova. Ni vizuri kama nini, basi, kwa wazazi kuwa wenye bidii katika kuwafundisha watoto wao mafundisho yaliyo bora kutoka kwa Neno la Mungu!

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki