Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g93 9/8 uku. 31
  • “Kujifunza Somo la Uvumilivu”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Kujifunza Somo la Uvumilivu”
  • Amkeni!—1993
  • Habari Zinazolingana
  • Kulinda Uhuru—Jinsi Gani?
    Amkeni!—1999
  • Ustahimilivu—Kutoka Mwisho Mmoja Hadi Ule Mwingine
    Amkeni!—1997
  • Uvumilivu
    Amkeni!—2015
  • Jinsi Biblia Inavyoweza Kukusaidia Kuwa Mstahimilivu
    Habari Zaidi
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—1993
g93 9/8 uku. 31

“Kujifunza Somo la Uvumilivu”

TUNAPOKARIBIA mwisho wa karne ya 20, je, ainabinadamu kwa ujumla imejifunza chochote kutokana na historia yayo yenye jeuri tangu 1914? Federico Mayor, mkurugenzi mkuu wa UNESCO (Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni), hakuwa na maoni chanya kupita kiasi kwenye makala aliyoandika katika The Unesco Courier. “Ulimwengu ambao kujitokeza kwao kwaweza kutambuliwa . . . hauleti idili ya moyo mzima. Ushupavu wa kidini, utukuzo wa taifa, chuki za kikabila na rangi, upingaji watu wa Kiyahudi: upepo wa uhuru umechochea moto wa chuki. . . . Kuanguka kwa utaratibu wa zamani kumeacha nafasi kwa aina zote za mianzo mipya, baadhi yayo ikiwa imechafuka kupita kiasi—na jeuri inaendelea kusitawi katika nafasi tupu.”

Kwa nini jeuri inasitawi? Kwa nini watu huchukia na kuua wengine kwa sababu tu ya tofauti za kidini au malezi ya kikabila? Iwe ni katika ile iliyokuwa Yugoslavia, katika India, katika Kaskazini mwa Ailandi, katika United States, au mahali penginepo pote katika ulimwengu huu, mojapo sababu kuu yaelekea kuwa elimu isiyo na mwongozo mzuri. Badala ya kujifunza kuvumiliana na kuheshimiana, watu wamejifunza kutotumaini na chuki kutoka kwa wazazi wao, shule zao, na kwa jamii kwa ujumla.

Federico Mayor aliendelea: “Acheni tuache uvumilivu huo usiofaa ambao huturuhusu kuvumilia yale yasiyovumilika—umaskini, njaa na kuteseka kwa mamilioni ya wanadamu. Tukifanya hivyo, tutapata ujoto wa mwanga-jua wa huruma na udugu.” Hayo ni maneno yenye kuvutia. Lakini ni njia gani iliyopo inayofanyakazi iwezayo kubadili roho ya giza ambayo ni msingi wa unaoitwa ulimwengu wetu ulionurishwa?

Zaidi ya miaka 2,500 iliyopita, Isaya alirekodi maneno haya ya Yehova: “Na watoto wako wote watafundishwa na BWANA [Yehova, NW]; na amani ya watoto wako itakuwa nyingi.” (Isaya 54:13) Kwa kuwa “Mungu ni upendo,” inamaanisha kwamba wale ambao kwa kweli wanaishi kulingana na kanuni zake watajifunza amani, si vita; upendo, si chuki; uvumilivu, si kutovumilia.—1 Yohana 4:8.

Ni nani wanaoendeleza fundisho hilo linaloongoza watu kwenye amani na upendo na uvumilivu? Ni nani wanaoishi kwa umoja licha ya asili ya taifa lao? Ni nani ambao wamepokea elimu ya Biblia ambayo imebadili mtazamo wao wote kutoka ule wa chuki mpaka ule wa upendo? Twapendekeza kwamba uchunguze mafundisho na mazoea ya Mashahidi wa Yehova ili ugundue ni kwa nini kwa kweli wana umoja wa ulimwenguni pote.—Yohana 13:34, 35; 1 Wakorintho 13:4-8.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki