Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g94 10/8 kur. 3-4
  • Wamishonari—Wapaswa Kuwa Nini?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Wamishonari—Wapaswa Kuwa Nini?
  • Amkeni!—1994
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Mishonari Ni Nini?
  • Wamishonari Wamekifuata Kielelezo kwa Kadiri Gani?
  • Je, Bado Kuna Uhitaji?
  • Kufanya Wanafunzi wa Kweli Leo
    Amkeni!—1994
  • Nuru ya Kiroho kwa “Kontinenti Yenye Giza”?
    Amkeni!—1994
  • Wamishonari “Mpaka Sehemu ya Mbali Zaidi ya Dunia”
    Jinsi Michango Yako Inavyotumiwa
  • Wamishonari Wasukuma Mpanuko wa Ulimwenguni Pote
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—1994
g94 10/8 kur. 3-4

Wamishonari—Wapaswa Kuwa Nini?

NENO “mishonari” laweza kuzusha hisia-moyo kali. Katika watu fulani, hilo huchochea uvutio, likiwakumbusha watu mmoja-mmoja kama Mama Teresa au Albert Schweitzer aliyekufa.

Tofauti na hivyo, wengine huitikia kwa ubaridi, uchukizo, au hata hasira wakati habari ya wamishonari iguswapo. Kwao neno hilo hudokeza wahadaaji wa akili za watu na huwakumbusha ukoloni.

Kwa habari ya wamishonari, swali lifaalo ni kwamba, Je, wao wamekuwa mawakili wa nuru au mawakili wa giza?

Mishonari Ni Nini?

Mishonari hufasiliwa kuwa “mtu anayechukua umisheni [utume] fulani,” yaani, kuchukua “huduma iliyoagizwa na shirika fulani la kidini ili kusambaza imani yalo au kuendeleza kazi ya kufadhili wanadamu.”

Msingi wa umishonari wa Kikristo uliandaliwa na Yesu Kristo alipowaambia wafuasi wake: “Kwa hiyo nendeni mkafanye wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote.” Hii hufanya iwe lazima kuhubiri ujumbe wa Kikristo katika ulimwengu mzima.—Mathayo 28:19, New World Translation.

Yesu mwenyewe alikuwa mishonari, aliyetumwa na Baba yake, Yehova, kutoka mbinguni aende kwenye mgawo wa kigeni, dunia. (Wafilipi 2:5-8) Kiakili, mishonari Mkristo apaswa kukifuata karibu-karibu kielelezo kilichowekwa na Yesu Kristo. Mishonari mmoja wa karne ya kwanza aliyefanya hivyo hasa alikuwa mtume Paulo, aliyepata kuwa kiolezo cha kuigwa na wamishonari Wakristo wa baadaye.—1 Wakorintho 11:1.

Ingawa Yesu alisikitishwa na matatizo ya kijamii yenye kukumba wanadamu, hakuchukua kwamba kuyatatua ndiko kulikuwa jambo la umaana wa kwanza alipokuwa duniani. Kama angalifanya hivyo angaliwapunguzia shida kwa muda tu. (Yohana 6:26, 27; 12:8) Jambo fulani jingine lilikuwa la umaana mkubwa zaidi. “Mimi nimezaliwa kwa ajili ya haya, na kwa ajili ya haya mimi nalikuja ulimwenguni,” Yesu akamwambia Pilato, “ili niishuhudie kweli.” Thamani ya kuwa na ujuzi juu ya kweli hiyo haiwezi kukaziwa kupita kiasi, kwa kuwa mapema kidogo Yesu alikuwa ametaarifu hivi katika sala: “Hii yamaanisha uhai udumuo milele, kutwaa kwao ujuzi juu yako wewe, Mungu pekee wa kweli, na juu ya yule uliyemtuma, Yesu Kristo.”—Yohana 17:3, NW; 18:37.Je, wamishonari wa Jumuiya ya Wakristo wamekifuata karibu-karibu kielelezo kilichowekwa na Yesu? Je, wamethibitika kuwa mawakili wa nuru kama alivyokuwa, wakirudisha nuru ya Neno la Mungu, ambalo kuwa na ujuzi walo huongoza kwenye uhai udumuo milele? Au wamewaacha watu gizani? Jibu kwa maswali haya lapasa kutupendeza sisi sote kwa sababu tunda lililotokezwa na wamishonari Wakristo muda wa karne zilizopita hutusaidia kuitambua dini ya kweli, na pia dini ya bandia. Kwa hiyo Amkeni! lafurahi kutangaza kwamba litazungumzia habari hii kwa kina kirefu katika matoleo yalo matano yanayokuja.

Wamishonari Wamekifuata Kielelezo kwa Kadiri Gani?

Wamishonari wamefanya michango ya thamani kubwa katika kueneza ujumbe wa Kristo. Kwa kielelezo, wengine wameitafsiri Biblia katika lugha za kienyeji, hivyo kuwezesha watu waisome wao wenyewe.

Hata hivyo, siku hizi yaonekana kwamba wamishonari fulani huhisi kutimiza mahitaji ya kijamii kwapaswa kutangulizwa mbele ya jitihada za kuhubiri au kutafsiri. Makala moja katika gazeti Time yenye kichwa “Mishonari Mpya” ilisema: “Kati ya Waprotestanti, kumekuwako badiliko la kuelekea kujihusisha zaidi na matatizo ya msingi ya kiuchumi na kijamii ya watu ambao wamishonari wanajaribu kuwafikia.” Kwa habari ya Wakatoliki, mkuu wa misheni za Wayeswiti aliyetumwa kutoka Marekani alisema kwamba kushiriki imani za Kikristo “kumechukua mahali pa pili kufuatia kutumikia wanadamu.” Na mwandishi wa misheni ya Kikatoliki alitoa hoja hii: “Wakati uliopita, tulikuwa na yale yaitwayo madhumuni ya kuokoa nafsi. . . . Sasa, kwa msaada wa Mungu, twaamini kwamba watu wote na dini zote tayari zinaishi katika neema na upendo wa Mungu na zitaokolewa na rehema ya Mungu.”

Je, hii yamaanisha kwamba hakuna tena uhitaji wa kufundisha Neno la Mungu kama Yesu alivyofanya?

Je, Bado Kuna Uhitaji?

Katika 1985 nyumba kama 18,000 katika Hamburg, Ujerumani, zilipigiwa simu na wajitoleaji mamia kadhaa katika kile ambacho gazeti moja lilikiita “umishonari wa kufikia halaiki ya watu kwa kutumia simu.” Ni wazi kwamba haukufua dafu sana. Desemba uliopita The European liliandika hivi: “Kanisa la Kiprotestanti katika Ujerumani . . . limeona mahudhurio yakishuka kwa zaidi ya 500,000 tangu 1991.”

Kundi halipungui kondoo katika makanisa ya Ujerumani tu. Mamilioni ya watu ulimwenguni pote wameipa dini kisogo, wasiione tena kuwa yafaa kwa maisha katika miaka ya 1990 yenye kuona mambo kama yalivyo hasa. Lakini kuujua Ukristo ni muhimu ikiwa tutakabiliana kwa mafanikio na giza la ulimwengu wa leo na kutegemezwa na tumaini la ulimwengu mzuri zaidi kwa wakati ujao. Amri ya Yesu kufanya wanafunzi wa watu wa mataifa yote ni njia ifaayo ya kutimiza uhitaji wa haraka.

Yesu Kristo alikusudia wamishonari Wakristo wawe mawakili—yaani, wajumbe—wa nuru, si mawakili wa giza. Wamishonari wa Jumuiya ya Wakristo wametimiza hilo kwa kadiri gani? Ni kigezo gani ambacho wamefuata?

[Hisani ya Picha katika ukurasa wa 3]

Culver Pictures

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki