Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g95 6/22 kur. 20-21
  • Aliathiri Maisha Nyingi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Aliathiri Maisha Nyingi
  • Amkeni!—1995
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Vijana Wanatiwa Moyo Kumtumikia Mungu
  • Wenye Umri Mkubwa Watiwa Moyo Pia
  • Kutoka kwa Wasomaji Wetu
    Amkeni!—1995
  • Kwa Nini Mimi Hujikata Kimakusudi?
    Vijana Huuliza
  • Mungu Aikuza Katika Alaska
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
  • Saidieni Vijana ‘Wawe Vielelezo kwa Waaminifu’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—1995
g95 6/22 kur. 20-21

Aliathiri Maisha Nyingi

KATIKA Novemba 19, 1994, Kathy Roberson alikufa katika umri wa miaka 26. Yeye alihudhuria kwa uaminifu mikutano ya Kikristo hadi juma la kifo chake. Vita yake dhidi ya kansa tangu umri wa miaka tisa ilikuwa imerekodiwa katika Amkeni! la Agosti 22, 1994, chini ya kichwa “Maisha Yawapo Magumu.” Baada ya kusoma hiyo makala, wengi kutoka ulimwenguni pote waliitikia kwa barua na kueleza jinsi kielelezo cha moyo mkuu cha Kathy kilivyowaathiri kwa kina.

Vijana Wanatiwa Moyo Kumtumikia Mungu

Loida, kutoka Hispania aliandika hivi: “Nina umri wa miaka 16, na nililia niliposoma lile ono kuhusu uvumilivu wa Kathy. Nilikuwa mwoga wa kufa, lakini kwa sababu ya makala hii, naelewa kwamba, kama alivyosema, ‘jambo lililo la maana sana, si kama tuishi ama tufe sasa, bali ni kama tunapata baraka za Yehova Mungu, Yule awezaye kutupa uhai wa milele.’”

Mari, kutoka Japani, aliandika hivi: “Kwa kuwa nina umri karibu sawa na wa Kathy na nilibatizwa siku moja naye, kusoma ono lake kulionekana kama kusoma barua yenye kutia moyo kutoka kwa rafiki wa karibu. Tumaini lake kwamba simulizi lake lingesukuma wengi watumie afya yao, si katika kufuatia mambo ya ubatili, bali kwa hekima katika utumishi wa Yehova lilisababisha moyo wangu uwake, kwa kuwa niko karibu kuanza upainia wa kawaida [utumishi wa wakati wote].”

Noemi, kutoka Italia, aliandika vivyo hivyo, akisema kwamba tamanio la Kathy la vijana kutumia afya yao, si katika kufuatia mambo ya ubatili, bali kwa hekima katika utumishi wa Yehova “litakuwa kitia-moyo kwa maelfu ya vijana, kutia ndani mimi.” Noemi aliongeza hivi: “Natamani sana kumwona katika ulimwengu mpya wakati yote haya yatakuwa yamepita. Mara tu nimalizapo shule ya sekondari, nitaanza kupainia.”

“Nina umri wa miaka 18,” akaandika Rachelle kutoka Florida, Marekani, “nami nimekuwa nikifikiria kazi ya upainia kwa muda sasa. Nilipokuwa nikisoma ile makala ‘Maisha Yawapo Magumu,’ nilipata kikiwa kitia-moyo kikubwa kuona mtu mchanga kama mimi akivumilia magumu hayo. Kathy amenichochea kutumia afya yangu, kama alivyosema, ‘si kufuatia mambo ya ubatili, bali kwa hekima katika utumishi wa Yehova.’”

Wamishonari fulani kutoka kisiwa cha Chuuk, katika Mikronesia, waliandika hivi: “Mapainia wetu huku ni maskini kimwili. Hata hivyo, ono la Dada Roberson liliwasaidia kuthamini kile walicho nacho. Walitambua kwamba ingawa wako maskini kimwili wamebarikiwa na miili yenye nguvu inayowawezesha kumtumikia Yehova kwa wakati wote. Kilikuwa kikumbusha kizuri kwao kuwa wenye shukrani kwa kile walicho nacho na kutumia nguvu zao katika utumishi wa Yehova.”

Kikundi cha wanafunzi 16 kilichokuwa kikihudhuria shule ya upainia katika Ufaransa kilisukumwa kumpelekea Kathy picha ya maua pamoja na hiki kitia-moyo: “Hatutasahau himizo lako la kutumia wakati wetu kwa ajili ya Muumba wetu mkuu.”

Kijana mwingine kutoka Ufaransa aliandika hivi: “Tukiwa wachanga na shabaha kuu za Shetani, nyakati fulani sisi huhisi ikiwa vigumu kubaki washikamanifu kwa Yehova. Hata hivyo, tusomapo masimulizi kama hayo yenye kutokeza na kugusa moyo, twapokea nguvu mpya na bidii, tukijua kwamba vijana wengine, kama Kathy, hushika uaminifu-maadili wao licha ya kuteseka. Ni kielelezo chenye kuvutia kama nini!”

“Nina umri karibu sawa na wako na nina afya nzuri sana,” aliandika Nadine kutoka Ohio, Marekani. “Mara nyingi ninaacha mambo madogo yazuie utumishi wangu kwa Yehova. Kusoma simulizi lako kulifanya nichunguze maisha yangu kwa uzito zaidi, nikitambua wakati wa thamani ambao nimepoteza. Umekuwa msukumo kwangu.”

Mwanamke fulani mchanga kutoka Brazili alisema hivi: “Aligusa moyo wangu na kuongeza tamaa yangu ya kutumikia Mungu wetu kwa ukamili zaidi.”

Kijana fulani wa Kanada aliandika hivi: “Nina umri wa miaka 15. Miaka miwili iliyopita, nilipata kujua kwamba nilikuwa na mchochota wa ini unaosababishwa na zindiko zenye kujitengeneza. Kwa sababu ya ono la Kathy Roberson, nilitambua kwamba ijapokuwa hali yangu ya afya, naweza pia kutumikia Yehova kwa uaminifu kukiwa bado na wakati na kwamba lazima ningojee kwa subira mfumo mpya wa Mungu ulioahidiwa kwa ajili ya kurudia afya kikamili.”

Jennette kutoka New Jersey, Marekani, aliandika hivi: “Vizuizi vyote alivyopitia na imani aliyoonyesha hutusaidia kupiga moyo konde kuendelea kujitahidi kufanya mengi zaidi katika utumishi wa Yehova ijapokuwa magumu yoyote ambayo huenda tukawa nayo. Ninapanga kutumia ono lake pamoja na baadhi ya mafunzo yangu ya Biblia ili kuwahamasisha kuweka miradi ya utumishi wa upainia wanapohitimu kutoka shuleni.”

Wenye Umri Mkubwa Watiwa Moyo Pia

Mwanamke fulani kutoka California, Marekani, aliandika hivi: “Kwa hakika umeweka kando kuwa yasiyo na maana sana mambo yote madogo katika maisha yetu na ukaonyesha kihususa kile kilicho na umaana mkubwa katika maisha—uhusiano wetu na Yehova.” Yeye aliongeza hivi: “Ingawa nimepita ujana wangu kwa mbali sana, nilichochewa kwa kina na kuhamasishwa na maono yako na mtazamo wako. Imenisaidia kupitia mambo yangu ninayohitaji kutanguliza.”

Barua nyingine kutoka California ilisema hivi: “Lile ambalo umepitia ni mtihani mkubwa mno kama ule uliopitiwa na ndugu na dada katika Ujerumani au Malawi au mahali penginepo ambapo nimesoma juu yapo. Nina umri wa miaka 68 sasa, kwa hiyo, nimejionea, kusikia, na kusoma yaliyoonwa mengi sana. Simulizi lako litakuwa baraka kwa wachanga na wakubwa pia.”

Mwanamke fulani kutoka South Carolina, Marekani, alikubali hivi: “Mimi si mtoto. Nina karibu umri wa miaka 70.” Yeye aliandika kwa uthamini hivi: “Wewe ni Ayubu mwingine. Natumaini wote wachanga kwa wakubwa wataona uvumilivu wako.”

Barua nyingine ilisema hivi: “Imani ya Kathy na azimio viligusa moyo wangu. Ninaelekea miaka 57, na mmoja wa miradi yangu ulikuwa kuweka wakati mwingi zaidi katika utumishi wa Yehova ninapostaafu, lakini hivi majuzi niliyakinishwa kansa. Jinsi nilivyosikitika kwamba nilipokuwa mchanga na kuwa na afya yangu, sikufanya mengi zaidi kwa Yehova! Hakuna yeyote kati yetu anayeweza kutabiri wakati ambao ugonjwa mbaya utakapoondolea mbali pendeleo hilo.”

Mzee fulani Mkristo aliandika hivi: “Nitaweka makala hii katika faili ya kipekee kwa ajili ya usomaji wangu wakati jambo lisilotazamiwa lenye kujaribu imani yangu litokeapo. Pia nitaweka makala hii katika faili yangu ya ziara za uchungaji kwa matumizi ya kutia moyo marafiki wapendwa ambao wanakumbwa na magumu mfumo huu ukaribiapo mwisho wao.”

Kwa hakika, tunatiwa nguvu kupitia imani na moyo mkuu wa washiriki wote wa udugu wetu wa ulimwenguni pote. (1 Petro 5:9) Sisi sote twatazama mbele, kama alivyofanya Kathy, kwenye utimizo wa ahadi ya Biblia ya wakati ambapo “mauti haitakuwapo tena.” (Ufunuo 21:3, 4) Utakuwa wakati mtukufu ulioje wakati “hapana mwenyeji atakayesema, Mimi mgonjwa.”—Isaya 33:24.

[Picha katika ukurasa wa 20]

Kathy Roberson

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki