Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g95 7/22 uku. 3
  • Msiba Unapopiga

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Msiba Unapopiga
  • Amkeni!—1995
  • Habari Zinazolingana
  • Misiba ya Asili-Je! Mungu Ndiye Huisababisha?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
  • Biblia Inasema Nini Kuhusu Misiba ya Asili?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Matetemeko Makubwa ya Ardhi—Biblia Ilitabiri Nini?
    Habari Zaidi
  • Misiba ya Asili-Ni Ishara ya Nyakati?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—1995
g95 7/22 uku. 3

Msiba Unapopiga

KARNE ya 20 imetiwa alama na misiba mikubwa, na mingi yayo imesababishwa na mwanadamu. Ingawa hivyo, baadhi yayo sivyo. Akitabiri kuhusu siku zetu, Yesu Kristo alisema hivi: “Taifa litaondoka kupigana na taifa, na ufalme kupigana na ufalme; kutakuwa na njaa, na matetemeko ya nchi mahali mahali.” (Mathayo 24:7) Kweli, mwanadamu ndiye wa kulaumiwa kwa vita na upungufu wa chakula, lakini yeye hana daraka kuhusu matetemeko ya dunia. Katika njia inayofanana na hiyo, huku baadhi ya misiba ya mafuriko ikisababishwa na utendaji wa mwanadamu, yeye hawezi kulaumiwa kwa sababu ya matetemeko ya dunia. Wala vimbunga wala milipuko ya volkeno si kosa la mwanadamu.

Hata kisababishi kiwe kipi, misiba ya asili huonyesha udogo wa mwanadamu, kutoweza kwake akabilipo kani za asili zenye kutisha. Dunia hii, makao yetu, kwa kawaida huhisi ikiwa salama na thabiti sana. Lakini inapotikiswa na tetemeko la dunia, kufurikishwa kwa maji yanayofurika, ama kuyumbishwa na pepo kali ambazo huikumba kana kwamba ni kani za milipuko, hisia hiyo ya usalama hutoweka.

Misiba ya asili imesababisha uharibifu mkubwa na hasara kubwa ya uhai wakati wa hii karne ya 20. Je, hili lingeweza kuwa liliepukwa? Je, kuna lolote liwezalo kufanywa ili kupunguza hayo madhara yenye maafa? Tukiwa mmoja-mmoja, ni nini tunaloweza kufanya ili kujilinda? Je, tumebaki bila tumaini kabisa wakati msiba unapopiga? Je, jamii ya kibinadamu sikuzote itazidi kupatwa na mabaya yasiyoistahili kwa njia hii? Makala zifuatazo zitazungumzia maswali haya.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki