Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g96 2/8 uku. 30
  • Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kutoka kwa Wasomaji Wetu
  • Amkeni!—1996
  • Habari Zinazolingana
  • Kutoka kwa Wasomaji Wetu
    Amkeni!—1996
  • Kutoka kwa Wasomaji Wetu
    Amkeni!—1996
  • Kutoka kwa Wasomaji Wetu
    Amkeni!—1996
  • Kutoka kwa Wasomaji Wetu
    Amkeni!—1996
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—1996
g96 2/8 uku. 30

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Makusanyiko ya Mashahidi Asanteni kwa jambo lililoonwa lenye kichwa “Siku Iliyobadili Maisha Yake.” (Machi 22, 1995) Jambo lililoonwa la mwanamke mmoja mchanga ambaye shangazi yake alimwalika kwenye siku ya kusanyiko la pekee la Mashahidi wa Yehova lilinikumbusha kwamba jambo hilohilo lilinipata mimi. Nilihudhuria kusanyiko langu la kwanza wakati wa kiangazi cha 1985, baada ya kualikwa na ndugu yangu. Kutotumaini kwangu kwa kwanza upesi kulibadilishwa na hisia ya uchangamfu; nilihisi kana kwamba nilikuwa katikati ya familia moja kubwa. Niliamua kuendelea kujifunza Biblia, na leo mimi ni painia wa kawaida, mweneza-evanjeli wa wakati wote.

E. F., Italia

Deni Asanteni kwa makala yenu “Je, Yafaa Kujiingiza Katika Deni?” (Juni 8, 1995) Nina umri wa miaka 13 tu, lakini sikuwa nikitumia pesa zangu vizuri. Nafikiri makala hii itanisaidia sana.

C. A., Marekani

Utumwa Nikiwa mwanamke Mmarekani mwenye asilia ya Kiafrika, nilithamini sana mfululizo wa makala wa Juni 8, 1995, “Ile Minyororo na Machozi ya Utumwa.” Picha ya jalada ilinifanya nilie machozi. Niliguswa moyo kwamba mlikuwa na moyo mkuu wa kushughulikia mambo haya ya uhakika yenye kutahayarisha ya kihistoria. Makala hiyo ilitolewa kwa njia yenye kugusa hisia sana nayo ilikuwa yenye kuarifu sana.

B. M., Marekani

Makala hiyo ilikuja kwa wakati ufaao kabisa kwa kuwa tulikuwa tunazungumza habari hiyo kwenye somo la historia. Nilitumia makala hiyo kumalizia baadhi ya masomo ya nyumbani ya hiari, na nikapata maksi nyingi. Pia niliwasikitikia sana wale watumwa.

M. C., Ujerumani

Simulizi la Maisha “Utafutaji Wangu Wenye Mafanikio wa Maana ya Uhai” (Mei 22, 1995) ilikuwa makala yenye kugusa moyo sana. Masimulizi ya Harold Dies yalinisaidia niamue ama kuingia katika utumishi wa wakati wote. Pia nilikuwa na fursa ya kutembelea Betheli, makao makuu ya Mashahidi wa Yehova katika Brooklyn, New York, na nilipendezwa sana. Sasa sina shaka kuhusu kuingia kwangu katika utumishi wa wakati wote!

A. C., Marekani

Samehe na Usahau Asanteni kwa makala bora zaidi “Maoni ya Biblia: Samehe na Usahau—Yawezekanaje?” (Juni 8, 1995) Nilikuwa nikijiuliza kama Biblia ilikuwa ikidai jambo lisilowezekana kutoka kwa watu wasio wakamilifu. Lakini sasa naelewa linalomaanishwa na kusamehe na kusahau. Makala hiyo imechangia sadikisho langu kwamba amri za Mungu si nzito.

C. I. C., Nigeria

Ilinibidi niandike kuwajulisha jinsi ninavyothamini makala hiyo. Nikiwa mtoto mdogo, nilitendwa vibaya kingono na ami zangu wawili. Baadaye, nilitendwa vibaya nikiwa mke. Nilipokuja kuwa Mkristo, nilijaribu kuonyesha upendo na kuwa mwenye kusamehe. Hata hivyo, sijaweza kusema kwa moyo mweupe kamwe kwamba niliwasamehe watu hao watatu walionisababishia uchungu mwingi sana kwa miaka mingi. Sasa natambua kwamba kuna mambo mengine ambayo lazima yaachwe mikononi mwa Yehova, nami naweza kuendelea na maisha yangu. Ufunuo 21:4 hunihakikishia kwamba umizo hili kubwa mno ambalo limeniathiri litakwisha hivi karibuni.

A. B., Marekani

Nimemaliza tu kusoma makala hiyo, na sijapata kamwe kuhisi nikiwa karibu zaidi na Yehova Mungu kuliko nihisivyo sasa hivi. Muda uliopita nilihusika katika dhambi nzito kwa ajili yayo ambayo nilitafuta msaada wa wazee wa kutaniko. Hata ingawa nilipokea shauri lenye fadhili, na lenye upendo kutoka kwao, bado nahisi nimezuiwa kusema na Yehova katika sala. Makala hii ilinipa uelewevu ulio wazi zaidi niliouhitaji sana wa jinsi Baba yetu wa kimbingu husamehe na kusahau. Huo umeniwezesha kumfikia kwa uhuru katika sala ya kutoka moyoni—pendeleo ambalo nilikuwa nikiliepuka kipumbavu. Namshukuru Yehova kwa kunipa ‘chakula changu kwa wakati ufaao.’—Mathayo 24:45.

D. J. S., Marekani

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki