Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g97 6/8 uku. 3
  • Mitazamo Inayobadilika Yazusha Maswali Mapya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mitazamo Inayobadilika Yazusha Maswali Mapya
  • Amkeni!—1997
  • Habari Zinazolingana
  • Ni Nini Huathiri Mtazamo Wako?
    Amkeni!—1997
  • Kuukabili Huo Ugumu
    Amkeni!—1997
  • Je! Ni Busara Kutofanya Ngono Kabla ya Kufunga Ndoa?
    Kupata Faida Zote za Ujana Wako
  • Ngono Kabla ya Ndoa
    Amkeni!—2013
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—1997
g97 6/8 uku. 3

Mitazamo Inayobadilika Yazusha Maswali Mapya

“MVUVUMKO WA KUFANYA NGONO OVYOOVYO,” “ongezeko kubwa la kufanya ngono,” “mvuvumko wa kiadili.” Semi kama hizo zilitangaza mitazamo iliyobadilika kuelekea mwenendo wa kingono, hasa katikati ya miaka ya 1960 na baadaye. Wengi walipendelea ile shime isemayo “uhuru wa kufanya mapenzi,” ambayo ilikuwa mtindo-maisha uliofanya watu wakatae ndoa na ubikira.

Usemi wa mtungaji Ernest Hemingway, “Tendo la adili ni lile linalokufanya uhisi vizuri, na tendo lisilo la adili ni lile linalokufanya uhisi vibaya,” waweza kufafanua vizuri mtazamo wa wale walionaswa na uvutio wa uhuru wa kufanya ngono na kuridhika. Kukubali falsafa hiyo kulifanya wengi waone kwamba ni sawa kuwa na mahusiano ya muda mfupi-mfupi ya kingono pamoja na wenzi kadhaa, ambamo watu, waume kwa wake, walijaribu kutosheleza tamaa zao za kingono. ‘Uradhi’ wa kingono ukakosa mpaka. Vibonge vya kudhibiti uzazi, vilivyotokea katika mwongo huohuo, vilichangia kule kufanya ngono zaidi kusiko na mipaka.

Lakini, UKIMWI na maradhi mengine yanayopitishwa kingono yakawa matokeo ya mtindo-maisha wa kufanya ngono ovyoovyo. Mitazamo ya kingono ya kizazi kilegevu ilitikiswa kwelikweli. Miaka fulani iliyopita, gazeti Time lilikuwa na kichwa hiki kikuu “Ngono Katika Miaka ya 1980—Ule Mvuvumko Umekwisha.” Tangazo hilo lilitegemea hasa wingi wa maradhi ya kupitishwa kingono ambayo yalikuwa yameathiri Wamarekani wengi. Kufikia wakati huu, jumla ya visa vya UKIMWI ulimwenguni pote imefikia kiwango chenye kushtusha sana cha karibu watu milioni 30!

Hofu ya maradhi yanayopitishwa kingono ilitokeza badiliko jingine katika mitazamo ya watu wengi kuhusu kuwa na mahusiano ya muda mfupi-mfupi ya kingono. Toleo la 1992 la gazeti la burudani liitwalo US, likiripoti juu ya uchunguzi wa serikali, lilisema hivi: “Wanawake waseja wapatao milioni 6.8 wamefanya mabadiliko katika mwenendo wao wa kingono kwa sababu ya kuhofu UKIMWI na maradhi mengine yanayopitishwa kingono.” Kulingana na makala hiyo, ujumbe u wazi: “Ngono si jambo la kuchezea-chezea. Kufanya ngono ni hatari.”

Miongo hii yenye msukosuko imeathirije mitazamo kuelekea mahusiano ya kingono? Je, kuna somo lolote ambalo watu wamejifunza kutokana na kufanya mapenzi kiholela ambako kumekuwapo katika miongo ya majuzi na pia somo kutokana na kuzuka kwa maradhi ya kupitishwa kingono katika miaka ya 1980? Je, kuanzishwa kwa masomo ya ngono katika shule za umma kumesaidia vijana wa kiume na wa kike kukabiliana vema na mwenendo wa kingono? Ni ipi njia bora zaidi ya kukabili mitazamo inayobadilika kuelekea mwenendo wa kingono?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki