Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g97 7/8 kur. 3-4
  • Wanyama wa Pori wa Dunia Wanaotoweka

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Wanyama wa Pori wa Dunia Wanaotoweka
  • Amkeni!—1997
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Ni Nani Apaswaye Kulaumiwa?
  • Spishi Zilizo Hatarini mwa Kutoweka—Mweneo wa Hilo Tatizo
    Amkeni!—1996
  • Mwanadamu Dhidi ya Mazingira
    Amkeni!—2001
  • Mfumo Tata wa Viumbe
    Amkeni!—2001
  • Bustani ya Wanyama—Je, Ni Tumaini la Mwisho la Wanyama wa Pori?
    Amkeni!—1997
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—1997
g97 7/8 kur. 3-4

Wanyama wa Pori wa Dunia Wanaotoweka

NA MLETA-HABARI WA AMKENI! KATIKA AUSTRALIA

JE, WEWE husisimuki kuona na kusikia wanyama halisi wa pori—simbamarara, nyangumi, au gorila? Je, husisimuki kumtunza koala? Kuhisi ardhi ikitetemeka chini ya kwato zenye kishindo za makundi ya wanyama wenye kuhama ambao ni wengi sana kufikia upeo wa macho? Lakini, kwa kusikitisha huenda watu wengi wasifurahie maono kama hayo—ila tu wazuru jumba la makumbusho, wasome kitabu, au wawaone katika kompyuta. Kwa nini?

Hii ni kwa sababu usomapo makala hiihii, maelfu ya mimea na wanyama yanatoweka kwa kasi. Dakt. Edward O. Wilson, mwanabiolojia kwenye Chuo Kikuu cha Harvard, akadiria kwamba spishi 27,000 kwa mwaka, au spishi tatu kwa kila saa, hutoweka. Kwa kiwango hicho, kufikia asilimia 20 ya spishi za dunia zingeweza kutoweka katika miaka 30 ijayo. Lakini kutoweka hakudumu kwa kiwango kilekile; kunazidi kuongezeka. Inatabiriwa kwamba kufikia mwanzo-mwanzo wa karne ifuatayo, mamia ya spishi zitakuwa zikitoweka kila siku!

Kifaru mweusi wa Afrika yumo hatarini mwa kutoweka. Uwindaji wa haramu ulipunguza idadi zao tokea 65,000 hadi 2,500 kwa muda unaopungua miaka 20. Orangutangu wanaopungua 5,000 ndio wamebaki katika misitu inayopunguka ya Borneo na Sumatra. Uharibifu huo umeathiri pia viumbe vya bahari za dunia. Mhasiriwa mmoja ni yule dolfini-baiji mwenye madaha apatikanaye katika Mto Yangtze wa China. Uchafuzi na uvuvi wa kiholela umeacha 100 pekee, na huenda wote wakafa kwa mwongo mmoja.

“Wanasayansi wa nyanja mbalimbali hawakubaliani kuhusu mambo mengi,” asema Linda Koebner katika Zoo Book, “lakini kuhusu udharura wa kuokoa spishi na uhai wa sayari hii, wao husema hivi kwa kauli moja: Miaka hamsini [50] ijayo ni ya muhimu kabisa.”

Ni Nani Apaswaye Kulaumiwa?

Idadi ya watu yenye kuongezeka imeharakisha kiwango cha kutoweka kwa wanyama, lakini si msongo wa idadi ya watu pekee ambao unapaswa kulaumika. Viumbe vingi—njiwa aina ya passenger, moa, auk mkubwa, na thilasini, kwa kutaja vichache tu—vilitoweka muda mrefu kabla ya tatizo la idadi kubwa ya watu kuzuka. Dakt. J. D. Kelly, mkurugenzi wa Kamati ya Hifadhi za Wanyama ya New South Wales, Australia, asema hivi juu ya rekodi ya nchi hiyo: “Kupotezwa kwa aina nyingi za mimea na wanyama tangu makao hayo yaanze katika 1788 ni aibu kubwa ya kitaifa.” Bila shaka maoni hayo ni ya kweli kuhusu nchi nyinginezo nyingi. Pia yadokeza visababishi vingine vibaya zaidi vya kutoweka kwa wanyama—ukosefu wa ufahamu na pupa.

Kwa sababu ya tatizo la kutoweka kwa wanyama duniani pote, kuna mteteaji mpya asiyetazamiwa ambaye anatetea hao wanyama wenye kung’ang’ania uhai—zile bustani za wanyama. Kwa kuongezeka, bustani hizo za wanyama zilizo katikati ya miji ndizo himaya za pekee za spishi nyingi. Lakini bustani nyingi za wanyama hazina nafasi za kutosha, na kuwatunza wanyama wa pori kuna gharama kubwa na vilevile ni kazi ngumu. Pia kuna maswala ya maadili kuhusu kuwafungia, hata kama wanatendewa kwa huruma. Isitoshe, wakiwa katika bustani za wanyama wao hutegemea kabisa upaji wa kifedha kutoka kwa wanadamu na mifumo dhaifu ya kisiasa na kiuchumi ambayo mara nyingi haitegemeki. Kwa hiyo hao wakimbizi kutoka porini wako salama kadiri gani?

[Sanduku katika ukurasa wa 3]

Je, Kutoweka kwa Wanyama Ni Jambo la Asili?

“Je, kutoweka kwa wanyama si utaratibu wa kiasili? Jibu ni la, angalau si kwa kiwango ambacho kutoweka kumetukia katika nyakati za majuzi. Kwa muda mrefu katika miaka 300 ambayo imepita, kiwango cha kutoweka kwa spishi kilikuwa karibu spishi moja kwa mwaka. Kwa sasa, kiwango cha kutoweka kunakosababishwa na wanadamu ni angalau mara elfu moja kuliko cha awali. . . . Kisababishi cha ongezeko hilo la kutoweka kwa wanyama ni utendaji wa kibinadamu.”—The New York Public Library Desk Reference.

“Nimevutiwa na viumbe vingi visivyo vya kawaida vilivyotoweka, na kuhuzunishwa, na mara nyingi nikikasirika kwa sababu vilitoweka. Kwa sababu katika visa vingi ni Mwanadamu ambaye kwa sababu ya pupa au ukatili, uzembe au kutojali amechangia moja kwa moja au kwa njia isiyo ya moja kwa moja kutoweka kwa viumbe hivyo.”—David Day, The Doomsday Book of Animals.

“Utendaji wa kibinadamu unasababisha kutoweka kwa spishi kabla hazijarekodiwa.”—Biological Conservation.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki