Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g99 4/8 kur. 3-4
  • Watoto Mashakani

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Watoto Mashakani
  • Amkeni!—1999
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Askari-Jeshi Watoto na Makao ya Mayatima
  • Kwa Kazi Ngumu ya Watoto
    Amkeni!—1999
  • Kunyanyasa Watoto Kingono—Tatizo la Ulimwenguni Pote
    Amkeni!—1997
  • Ubaguzi Dhidi ya Wanawake
    Amkeni!—1998
  • Sababu Inayofanya Watoto Wawe Wapiganaji Bora
    Amkeni!—1997
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—1999
g99 4/8 kur. 3-4

Watoto Mashakani

“Wakati, nishati, na uangalifu usipotolewa kwa ajili ya watoto, matatizo yote ya kibinadamu ambayo mengi ni ya muda mrefu yatabaki kuwa matatizo ya msingi ya muda mrefu”—Hazina ya Watoto ya Umoja wa Mataifa.

WATOTO wako mashakani ulimwenguni pote. Uthibitisho wenye kusadikisha unaokazia ukubwa wa msiba huu ulitolewa kwenye Mkutano wa Kimataifa Dhidi ya Biashara ya Ngono Inayoharibu Watoto uliofanywa Stockholm, Sweden, mwaka wa 1996 na kuhudhuriwa na wawakilishi wa nchi 130. Kwa kielelezo, ilisemwa kwamba katika sehemu nyingi za ulimwengu, kuna mamilioni mengi ya wasichana wachanga, wengine wana umri wa miaka kumi, wanaolazimishwa wafanye kazi wakiwa makahaba.

Gazeti la Australia Melbourne University Law Review lilisema kwamba ukahaba huo wa kulazimishwa umetajwa kuwa “mojawapo ya utumwa wa siku hizi ulio mbaya zaidi.” Baada ya miaka mingi ya kuumizwa kimwili, kiakili, na kihisia-moyo, wasichana hawa wanapata madhara mabaya sana katika maisha yao yote. Katika visa vingi wasichana hawa hukubali kutendwa ukatili huu kwa sababu tu wanataka kupata chakula ili waishi. Wasipofanya hivyo watakufa kwa sababu ya kukosa chakula. Kwa kusikitisha, wengi wa watoto hawa wasiokuwa na makao walilazimishwa kuwa makahaba na wazazi wao wenyewe walio maskini, waliowauza ili wapate pesa.

Jambo linaloongezea msiba huu wa watoto ulio dhahiri ni suala ambalo mara nyingi hujadiliwa kwa ukali sana kuhusu kufanyiza watoto kazi. Katika Asia, Amerika Kusini, na kwingineko na katika sehemu nyingine za wahamaji huko Marekani, watoto kama vile wenye umri wa miaka mitano wanalazimishwa kuingia katika ile inayoweza kuitwa “kazi ya utumwa.” Hufanya kazi kama roboti ndogo chini ya hali zenye kufadhaisha zinazoharibu kabisa miili na akili zao changa. Wengi wao hawana elimu, hawapati upendo wa wazazi, hawana makao salama, hawana vitu vya kuchezea vya watoto, hawana bustani za kuchezea. Wengi hutumiwa kwa faida kwa njia isiyo na hisia na wazazi wao wenyewe.

Askari-Jeshi Watoto na Makao ya Mayatima

Jambo linalofanya msiba huu uwe mbaya hata zaidi ni kwamba, watoto wanazidi kutumiwa kama askari-jeshi katika majeshi ya msituni. Watoto waweza kutekwa nyara au kununuliwa katika masoko ya watumwa na kisha kufanywa wawe wakatili hatua kwa hatua, nyakati nyingine wakifanywa watazame uuaji. Wengine hata wameamriwa wawaue wazazi wao au watumie dawa za kulevya kusudi wazidi kuua bila kufikiri.

Kielelezo kifuatacho chaonyesha madhara ya kutiwa kasumba ambayo yamewapata maelfu ya watoto walio askari-jeshi katika Afrika. Mazungumzo haya yenye kuvunja moyo yalikuwa baina ya mfanyakazi wa huduma za jamii na mvulana ambaye ni askari-jeshi ambaye yaelekea alikuwa akijaribu kudumisha hisia kidogo sana ya hatia aliyokuwa nayo:

“Je, uliua? ‘La.’

Je, ulikuwa na bunduki? ‘Ndiyo.’

Je, ulilenga shabaha? ‘Ndiyo.’

Je, ulifyatua risasi? ‘Ndiyo.’

Ni nini kilichotukia? ‘Walianguka tu.’”

“Baadhi ya vijana hawa ni wadogo tu kama watoto unapofikiria kwamba askari-jeshi fulani wana umri wa miaka sita na zaidi.” Imeripotiwa kwamba mapema mwaka wa 1988, kulikuwa na watoto askari-jeshi 200,000 ulimwenguni pote.

Inasemekana kwamba kati ya mwaka wa 1988 na 1992, katika makao ya mayatima katika nchi moja ya Asia, watoto 550, wengi wao wakiwa ni wasichana, walinyimwa chakula kimakusudi ili wafe njaa. Daktari mmoja anaripoti kwamba: “Mayatima hao hawakuwa na tembe za kumaliza maumivu yao. Hata walipokuwa wamelala wakiwa wamekufa, walifungiwa kwenye vitanda vyao.”

Vipi juu ya Ulaya? Nchi moja huko ilifadhaishwa na ugunduzi wa kikundi cha kimataifa kinachohusika na ponografia ya watoto ambacho kiliwateka nyara wasichana ili kuwatumia vibaya kingono. Kwa kusikitisha wasichana fulani waliuawa au wakanyimwa chakula hadi wakafa.

Kwa wazi ripoti hizi zinaonyesha kwamba nchi nyingi zina tatizo kubwa kuhusu kutenda watoto vibaya na kuwatumia ili kujifaidi. Lakini je, ni kutilia chumvi kusema kwamba tatizo hili limeenea ulimwenguni pote? Makala ifuatayo itajibu swali hilo.

[Picha katika ukurasa wa 4]

Mtoto ambaye ni askari-jeshi katika Liberia

[Hisani]

John Gunston/Sipa Press

[Picha katika ukurasa wa 4]

Kwenye kiwanda cha kutengenezea matofali katika Kolombia, watoto hutumiwa kama toroli za kibinadamu

[Hisani]

UN PHOTO 148000/Jean Pierre Laffont

[Hisani ya Picha katika ukurasa wa 3]

FAO photo/F. Botts

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki