Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g 2/11 kur. 8-9
  • Kweli ya Biblia Iliwaweka Huru

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kweli ya Biblia Iliwaweka Huru
  • Amkeni!—2011
  • Habari Zinazolingana
  • Kutatua Matatizo ya Vijana
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
  • Kutoka Mshuko wa Moyo Hadi Furaha
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Aliazimia Aishi Kulingana na Viwango vya Adili za Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Mwishowe Mbegu Ilichipuka
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
Amkeni!—2011
g 2/11 kur. 8-9

Kweli ya Biblia Iliwaweka Huru

YESU KRISTO aliwaambia hivi watu waliokuwa wakimsikiliza: “Mtaijua kweli, nayo kweli itawaweka ninyi huru.” (Yohana 8:32) Kama vile mifano ifuatayo inavyoonyesha, uhuru huo unatia ndani kuwa huru kutokana na roho waovu, ambao ndio wanasema uwongo na kuwadanganya watu wakitumia uchawi.—Yohana 8:44.

Kila moja ya masimulizi haya inaonyesha jinsi kweli ya Biblia ina nguvu za kuweka watu huru. Naam, hiyo pekee ndiyo inayowaweka watu huru. Mbona usijichunguzie Biblia uone. Hutakatishwa tamaa.

[Sanduku/Picha katika ukurasa wa 8]

Picha hizi zimeigizwa

● Susanna alikuwa kuhani wa kike katika dini moja huko Brazili. Alitaka kutumia nguvu zake zisizo za kawaida kuwasaidia watu wenye uhitaji. Pia, alifurahia sana “kuzungumza na mama yake aliyekuwa amekufa.” Hata hivyo, baada ya muda, “mama” yake alimsihi sana ajiue ili waishi pamoja katika ulimwengu wa roho. Jambo hilo lilimsumbua sana Susanna na hata aliota ndoto mbaya. Kisha Susanna na mume wake wakaanza kujifunza Biblia na Mashahidi wa Yehova. Walijitahidi sana ‘kumpinga Ibilisi,’ na mwishowe ‘aliwakimbia.’ (Yakobo 4:7) Sasa wanaishi kwa amani, na Susanna haoti ndoto mbaya. Alisema, “Nina sababu nyingi sana za kumshukuru Yehova, lakini ninashukuru hata zaidi kwamba alitutoa kwenye giza la kiroho.”

[Sanduku/Picha katika ukurasa wa 8]

● Timothy, anayeishi Afrika Magharibi, ni kiziwi na bubu.a Kwa sababu madaktari wa kawaida hawakuweza kumsaidia, aliwaendea waponyaji wa kimuujiza, lakini wao pia walishindwa. Aliandika, “Nilivunjika moyo sana kutokana na uwongo nilioambiwa.” Baadaye Timothy alianza kujifunza Biblia pamoja na Mashahidi wa Yehova, ambao walimweleza kusudi la Mungu la kuondoa magonjwa na ulemavu wote. Timothy anasema, “Ninasubiri kwa hamu siku ambayo katika ulimwengu mpya wa Mungu ‘masikio ya viziwi yatazibuliwa . . . na ulimi wa bubu utapaaza sauti kwa furaha.’” (Isaya 35:1-6) Kwa sasa, yeye hufurahia kutumia mashini ndogo ya DVD kuwahubiria kweli za Biblia watu wengine walio na matatizo ya kusikia, na kuwasaidia kupata uhuru wa kweli.

[Maelezo ya Chini]

a Baadhi ya majina yamebadilishwa.

[Sanduku/Picha katika ukurasa wa 9]

● Evelyn anayeishi nchini Estonia, alikuwa amejiingiza sana katika uchawi. Kwa sababu Yesu aliwaponya watu, yeye pia alitaka kufanya hivyo. Alitaka hasa kumsaidia mama yake aliyekuwa na ugonjwa wa kudumu. Hivyo, ili atambue na kutibu magonjwa mabaya alijifunza kutumia pinduli. Baada ya muda, alianza kuchunguza Biblia. Matokeo? Alisema, “Nilitambua kwamba nilikuwa nimedanganywa sana. Kwa hiyo, niliteketeza vitabu na pinduli zangu za uchawi.” Sasa anafundisha kweli za Biblia zinazowaweka watu huru.

[Sanduku/Picha katika ukurasa wa 9]

● Mary alilelewa katika mojawapo ya visiwa vya Papua New Guinea ambako watu wanawahofu sana wafu. Iwapo mtu angekufa katika kijiji chake, Mary angelala chini ya kitanda cha mtu mwingine, kwani alihofu kuwa roho ya huyo mfu ingemsumbua akiwa peke yake. Kisha akajifunza kutoka katika Biblia kwamba wafu wamelala—kwamba wako kaburini wakisubiri kufufuliwa waishi katika Paradiso duniani. (Luka 23:43; Yohana 11:11-14) Tangu wakati huo, Mary hahofu wafu tena.

[Sanduku/Picha katika ukurasa wa 9]

● Alicia, aliyelelewa na wazazi ambao ni Mashahidi wa Yehova huko Marekani, alianza kusoma vitabu na kutazama sinema za kichawi. Kisha akaanza kufikiri kwa uzito kuhusu kweli za Biblia alizokuwa amejifunza. Alipotambua kwamba alikuwa akijaribu ‘kushiriki meza ya Yehova na meza ya roho waovu,’ alibadili njia zake na sasa anafurahia kuwa na dhamiri safi mbele za Mungu.—1 Wakorintho 10:21.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki