Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • kc sura 5 kur. 37-45
  • Ule Ufalme—Sababu Gani Umekawia Sana ‘Kuja’?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ule Ufalme—Sababu Gani Umekawia Sana ‘Kuja’?
  • “Ufalme Wako Uje”
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • ENZI KUU YA MUNGU YAPINGWA
  • LILE SUALA LA UKAMILIFU WA MWANADAMU
  • SHTAKA LA MDHIHAKI LAJIBIWA
  • Mateseko ya Binadamu—Mbona Mungu Anayaruhusu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
  • Suala Linalokuhusu Wewe
    Amani na Usalama wa Kweli—Wewe Unaweza Kuupataje?
  • Suala Ambalo Lazima Sote Tukabili
    Mwabudu Mungu wa Pekee wa Kweli
  • Kwa Nini Muda Mrefu Sana Kulijibu Suala
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
Pata Habari Zaidi
“Ufalme Wako Uje”
kc sura 5 kur. 37-45

Sura ya 5

Ule Ufalme—Sababu Gani Umekawia Sana ‘Kuja’?

1. Kwa sababu ya maneno ya Waroma 8:22, kunatokea maulizo gani?

MTUME Paulo anaandika: “Tunajua ya kuwa viumbe vyote pia vinaugua, na vina uchungu pamoja.” (Waroma 8:22, ZSB) Sababu gani iko hivyo? Sababu gani Mungu ameruhusu vita, uhalifu, magonjwa na huzuni kwa muda wa miaka 6,000 iliyopita ya historia iliyoandikwa? Kulikuwa na kasoro gani, hivi kwamba wanadamu, walioumbwa waishi kulingana na sheria ya kimungu, wanasumbuliwa sasa na uasi wa sheria? Sababu gani Baba yetu wa kimbingu hakusahihisha hali hiyo? Ikiwa ule Ufalme ndilo suluhisho, sababu gani umekawia sana ‘kuja’? Je! kweli twaweza kutumaini kwamba Mungu atabadili hali hizo mbaya ziwe nzuri?

2. Chini ya enzi kuu ya Mungu, dunia ingalikuwaje sasa?

2 Chini ya ule utawala mkuu zaidi, au enzi kuu, wa “Mfalme wa umilele,” hali bora zingalienea duniani tangu ule wakati wa uumbaji katika Edeni. Wakati mwanamume na mwanamke wa kwanza wangeendelea kuzaa watoto, na jamaa ya kibinadamu iongezeke kuwa maelfu ya mamilioni ya vikundi vya jamaa, dunia nzima ingaligeuka kuwa paradiso yenye uzuri, yenye kujaa vicheko vya furaha na upendo wa jirani wa jamii zote za wanadamu zenye amani.—Linganisha Mhubiri 2:24.

3. (a) Mtu aliumbwa kwa sura ya nani? (b) Wale watu wa kwanza wawili waliagizwa kufanya nini? (c) Ni maulizo gani ambayo ni lazima tuulize sasa?

3 Hivyo ndivyo Muumba mwenye upendo alivyoikusudia dunia hii alipoumba mtu kwa mfano wake mwenyewe wa adili na kufanya mwanamke kutokana na mwanamume. Maana masimulizi ya Biblia juu ya uumbaji yanatuambia hivi:

“Wa kiume na wa kike akawaumba. Zaidi ya hapo, Mungu akawabariki na Mungu akawaambia: ‘Mwe wenye kuzaa sana na kuwa wengi na kuijaza dunia na kuitiisha, na kuweka chini ya mamlaka samaki wa bahari na viumbe wenye kuruka wa mbingu na kila kiumbe anayetembea juu ya dunia.’ . . . Baada ya hapo Mungu aliona kila kitu alichokuwa amefanya na, tazama! kilikuwa kizuri sana.” (Mwanzo 1:26-31, “NW”)

Sababu gani, basi, uumbaji wa Mungu duniani hauonekani ‘mzuri sana’ leo?

ENZI KUU YA MUNGU YAPINGWA

4. (a) Ni sheria gani ya Mungu inayopita zote, na kwa sababu gani (b) Ni nani aliyetaka kutunga sheria zilizo tofauti, naye alifanyaje hivyo?

4 Msingi wa uumbaji ulikuwa sheria za Mungu. Na yenye kutokeza kati ya hizo ni ile sheria ya upendo Mungu mwenyewe “ni upendo.” (1 Yohana 4:8) Lakini sasa mtu fulani akatokea aliyetaka kutungia wanadamu sheria tofauti. “Mtu fulani” huyo alikuwa ‘mwana wa Mungu’ wa kimalaika asiyeonekana, bila shaka mmoja wa wale ‘waliopiga kelele kwa furaha’Yehova alipoiumba dunia na kila kitu juu yake. (Ayubu 38:7) Malaika huyo alijifanya kuwa shetani, adui ya Mungu. Yeye alitaka kujitegemea, akatafuta kuabudiwa na kupanda roho ya uasi. (Waefeso 2:1, 2; linganisha Luka 4:5-7.) Alifanya mpango wenye hila atumie wazazi wetu wa kwanza kutimiza malengo yake mwenyewe yenye choyo. Alifanyaje hivyo?

5, 6. (a) Ni amri gani rahisi ambayo Mungu alimpa Adamu? (b) Shetani alitumia njia gani ya kudanganya, na kwa sababu gani anaitwa “Ibilisi” kwa kufaa?

5 Katika ile bustani ya kiparadiso ya Edeni, Adamu na Hawa walikuwa ndio wapokeaji wa utawala wenye fadhili wa Yehova. Mungu aliandaa kila kilichohitajiwa kuwadumisha kiroho na kimwili. Ili waendelee na hali njema, aliwataka pia wamtii kuwa Bwana Mwenye Enzi Kuu wao. Kwa kusudi hilo alikuwa amempa Adamu amri rahisi, kwamba ni lazima asile kutokana na ule “mti wa ujuzi wa mema na mabaya.” Hiyo ilimhusu Hawa pia, baada ya kuumbwa kwake. Si kwamba Mungu alikuwa akiwanyima cho chote, maana ile miti mingine katika bustani ilitoa matunda yenye kujenga mwili ya namna nyingi zenye kupendeza. Walakini, kama wangekataa kumtii Mungu, wale sehemu ya tunda hilo moja, ‘wangekufa hakika.’ Kwa ujanja, kwa kutumia nyoka, mwasi yule Shetani akamfikia Hawa kwanza, akisema: “Hakika hamtakufa, kwa maana Mungu anajua ya kwamba siku mtakayokula matunda ya mti huo, mtafumbuliwa macho, nanyi mtakuwa kama Mungu, mkijua mema na mabaya.”—Mwanzo 2:17; 3:1-5.

6 Hilo lilimfanya Mungu aonekane kuwa mwongo. Lakini kwa kweli Shetani ndiye aliyekuwa mwongo. Kwa kufaa, huyo “baba ya wongo” akaja kuitwa Ibilisi pia, maana yake “Mchongezi.” (Yoane 8:44, ZSB) Huko kulikuwa ni kupinga moja kwa moja enzi kuu ya Yehova, Uufalme wake juu ya viumbe vyake. Kulidokeza kwamba Mungu alikuwa akiwanyima maarifa ambayo walistahili kupata, kwamba utawala wa Mungu haukupasa kutumainiwa, kwamba wangefanikiwa kwa njia ya kujitegemea, wakijiwekea viwango vyao wenyewe vya “mema na mabaya.”

7. Wale watu wawili walishindwa jaribu katika mambo gani?

7 Yule mwanamke alitendaje aliposikia uchongezi huo? Alishindwa kulinda moyo wake, akaruhusu tamaa mbaya ipate mizizi humo. Ndipo tamaa hiyo ilipopata rutuba, akadanganywa afanye dhambi makusudi kwa kutokumtii Mungu. Kwa kufanya hivyo alidharau pia ukichwa wa mume wake Adamu, ambaye ingalimpasa amwombe shauri kwanza. Mwanamume huyo naye alitendaje? “Adamu hakudanganywa,” bali akachagua kumwunga mkono Hawa, akajiweka kwa makusudi katika uasi wake. Loo, hiyo ilikuwa siku yenye huzuni kwa wazazi wetu wa kwanza, na kwa jamii nzima ya wanadamu!—Mwanzo 3:6, 7; 1 Timotheo 2:14; linganisha Yakobo 1:14, 15.

8. (a) Ni hukumu gani ya haki ambayo Mungu alipasisha juu ya Adamu na Hawa? (b) Je! walikuwa na nafsi ambazo zingeenda mbinguni au kwenye moto wa mateso baada ya kufa? (c) Ni mfalme gani aliyekuja kututawala, na kwa sababu gani?

8 Adamu na Hawa walikuwa wameonyesha dharau kubwa sana kwa enzi kuu ya Mungu. Sasa basi, kupatana na sheria yake, Mungu akatangaza hukumu ya kifo, akimwambia Adamu hivi:

“Maana u mavumbi wewe, nawe mavumbini utarudi.” (Mwa-nzo 3:19)

Hapa Mungu hakumaanisha kwamba ni mwili tu wa Adamu ungekufa, lakini “nafsi” au “roho” fulani ya ndani itoroke ule mwili na kuendelea kuishi mbinguni au motoni. Sivyo, maana Adamu mwenyewe alikuwa “nafsi.” Ni kama masimulizi ya uumbaji yanavyosema, katika Mwanzo 2:7: “[Yehova] Mungu akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi, akampulizia puani pumzi ya uhai; mtu akawa nafsi hai.” Mwishowe, wote wawili Adamu na Hawa wakafa—wakiwa nafsi. Na kwa sababu jamii nzima ya kibinadamu ndiyo uzao wa Adamu mwenye madoa ya dhambi, sisi sote tumerithi dhambi na kifo. “Nafsi inayofanya zambi, itakufa.” (Ezekieli 18:4, 20, ZSB; NW; The Old Testament in Swahili (Mombasa), chapa ya 1949) Ndiyo, kwa kuwa sisi ni nafsi za kibinadamu, tunakufa. Kifo kimetutawala kama mfalme.—Warumi 5:12, 14; 6:12; Mhubiri 3:19, 20; 9:5, 10; Zaburi 6:5; 115:17.

LILE SUALA LA UKAMILIFU WA MWANADAMU

9. Ni suala gani jingine lililotokezwa katika Edeni?

9 Walakini, si enzi kuu ya Mungu tu iliyotiliwa mashaka kwa ule uasi katika Edeni. Suala jingine lilitokezwa. Kwa kuwa watu wenyewe wa kwanza ambao Mungu alikuwa ameweka duniani walikuwa wamekuwa wasioaminika katika jaribu, je! uumbaji wa Mungu ulikuwa na kasoro fulani? Je! ingeweza kusemwa kweli kweli kwamba kazi zake zote zilikuwa “kamilifu”?

10. (a) Je! uumbaji wa Mungu ulikuwa na kasoro, na sababu gani unajibu hivyo? (b) Ni kwa njia gani wanadamu wanaweza kuonyesha wana ‘sura ya Mungu’?

10 Kama Mungu angalitaka, angaliharibu Adamu na Hawa mara hiyo na kuumba watu wengine wawili. Lakini je! huko hakungalikuwa ni kukubali kwamba uumbaji wake wa kwanza ulikuwa na kasoro? Haukuwa na kasoro. Ni kwa sababu tu wazazi wetu wa kwanza walikuwa wamechagua kutumia vibaya uwezo wao wa hiari. Kama wangalikuwa mashine ambazo zilitakwa kufanya vizuri katika hali zote, hapo wangalikuwa hawana uwezo wa kupambanua mema na mabaya. Hapo hawangalikuwa ‘kwa sura ya Mungu.’ Daima Yehova anafanya vitu kwa ukamilifu, kwa usawa, kwa sababu yeye ni upendo. Anataka viumbe vyake vyenye akili vilevile visukumwe na upendo katika kufanya yaliyo sawa.—Mwanzo 1:26, 27; 1 Yohana 5:3.

11. Andiko la Kumbukumbu la Torati 32:4, 5 linasaidiaje kujua hali ilivyokuwa nyuma huko?

11 Imeandikwa hivi kwa habari ya Yehova: “Yeye Mwamba, kazi yake ni kamilifu; maana, njia zake zote ni haki. Mungu wa uaminifu, asiye na uovu, yeye ndiye mwenye haki na adili.” Uumbaji wake pia, yaani, wanadamu, unaweza kuwa wenye uaminifu, wenye uadilifu na unyofu. Basi aliruhusu Adamu na Hawa wazae watoto. Ijapokuwa hao walirithi tabia zenye dhambi kutoka kwa wazazi wao, wangekuwapo kati yao wale ambao wangempenda Muumba wao kwa uthabiti na ukamilifu wao, hata wakiwa na kutokamilika kwa kimwili na wanapopata majaribu makali na mateso. Lakini wengine kati ya wanadamu ‘wangetenda mambo ya uharibifu’ na kujionyesha kuwa si watoto wa Mungu. Hilo lingekuwa chaguo lao. Wao ndio wangelaumika kwa kasoro hiyo wala si Mungu.—Kumbukumbu la Torati 32:4, 5.

12, 13. (a) Shetani alimdhihakije Mungu kwa habari ya Ayubu? (b) Ayubu alitoa jibu gani. akapata matokeo gani?

12 Kwamba Shetani Ibilisi alikaza suala hilo juu ya ukamilifu wa mwanadamu mbele ya Mungu inaonyeshwa katika kitabu cha Biblia cha Ayubu. Mwanamume yule Ayubu, aliyeishi miaka kama 2,500 baada ya kupotoka kwa Adamu, alikuwa “mtu mkamilifu na uelekevu, mwenye kumcha Mungu na kuepukana na uovu.” Shetani alimdhihaki Mungu akisema uelekevu wa Ayubu haukuwa wa kweli, kwamba yeye alimtumikia Mungu kwa kutazamia kupewa faida fulani. Ayubu alipata hasara kubwa ya mali; watoto wake 10 waliuawa katika msiba; baadaye yeye mwenyewe akasumbuliwa na ugonjwa wenye kuchukiza sana, na mwishowe mkeye mwenyewe akamcheka, akisema: “Je! wewe hata sasa washikamana na utimilifu wako? umkufuru Mungu, ukafe.” Kisha, Ayubu akalazimika kupambana na mashutumu yenye kutia uchungu ya wafariji watatu wa uongo.—Ayubu 1:6- 2: 13.

13 Katika majaribu yote hayo Ayubu alishikamana na azimio lake hili:

“Hata nitakapokufa sitajiondolea [ukamilifu] wangu.” Alijithibitisha kuwa mwaminifu kwa Mungu, hivyo akatoa jibu lenye nguvu kwa mashtaka ya Shetani. Kwa hiyo Yehova alimpa Ayubu thawabu ya kupata maradufu vyote alivyokuwa navyo pale mwanzoni. Pia alibarikiwa akawa tena na wana saba na binti tatu—hao binti wakiwa ndio wenye sura nzuri zaidi katika nchi yote.—Ayubu 27:5; 42:10-15.

14. Wengine wamejibuje dai la Shetani vile vile, na ni nani aliye mfano bora zaidi katika kufanya hivyo?

14 Walakini, Ayubu ni mmojawapo tu wa mamia ya maelfu ya watumishi waaminifu wa Mungu ambao wamefurahisha moyo Wake kwa sababu ya kulitolewa jibu dai la uongo la Shetani la kwamba wenye kumpenda Yehova wanamtii na kumtumikia kwa sababu za kichoyo tu. Aliye mfano bora kupita wote ni Mwana wa Mungu mwenyewe, Yesu, ambaye, alipokuwa duniani, “aliustahimili [mti wa mateso] na kuidharau aibu,” kwa sababu ya ile furaha ya kuendelea kutumkia bila choyo katika mgawo ambao Mungu alimpa.—Waebrania 12:2.

SHTAKA LA MDHIHAKI LAJIBIWA

15. Sababu gani inaweza kusemwa kwamba upande wa Yehova lile shtaka umethibitishwa?

15 Sasa, ule wakati uliowekwa ni kama umekwisha. Wakati wa miaka kama 6,000 Yehova amekuwa akithibitisha upande wake kwa kujibu lile shtaka. Ameonyesha kwamba anaweza kuwa na wanaume na wanawake wanaoshika ukamilifu hata Shetani awalete mateso au majaribu mabaya sana, na anao. Ibilisi ametumia juu yao kila shauri bovu linalowazika, lakini imekuwa kazi bure. Watumishi waaminifu wa Mungu wamefurahisha moyo wa Baba yao, maana wamemtolea jibu la kumpa yule ‘anayemlaumu’ Mungu yaani, yule adui mkubwa, Shetani.—Mithali 27:11.

16. (a) Ni ushindi gani ambao washikamanifu fulani wa Mungu wamekwisha kushiriki? (b) Sababu gani raia za ule Ufalme wanawe; kuwa na uhakika na watawala wao?

16 Wakati uo huo, na kwa kutenda kwa njia ya uwekevu, Yehova amekuwa akichagua miongoni mwa hao washikamanifu watu watakaotawala pamoja na Kristo katika ufalme wa kimbingu. Ijapokuwa Shetani amewashtaki “mbele za Mungu wetu, mchana na usiku,” wamemshinda “kwa neno la ushuhuda wao; ambao hawakupenda maisha yao hata kufa.” Kama Yesu Kristo, Mfano wao, wamekuwa na nia ya kuonyesha ile sifa yenye kupita zote ya upendo wao kwa Mungu na jirani kwa kutoa hata maisha zao. Lo! wanadamu wataweza kuwa na uhakika kama nini na ule ufalme wa kimbingu ambao wafalme ni Kristo na washirika wake 144,000—wote wakiwa wamejaribiwa wakaonekana kuwa wenye kushika ukamilifu!—Ufunuo 12:10, 11; 14:1-5; 20:4; Yohana 15:13.

17. Ni nani watakaoirithi milki ya kidunia ya ule Ufalme?

17 Wengine, kama vile Ayubu, aliyekufa akiwa mwaminifu kwa Mungu nyakati zilizotangulia Ukristo, wanahakikishiwa kupata “ufufuo ulio bora” waingie katika “dunia mpya.” (Waebrania 11:35, UV; 2 Petro 3:13, NW) Wanakuwa sehemu ya wale “kondoo wengine” wa yule “mchungaji mwema” Yesu Kristo, wakiwa na taraja la kupata uzima wa milele katika dunia-paradiso. Pia, hao walio mfano wa kondoo wanaowafadhili “ndugu” za Kristo waliopakwa mafuta wakati wa “umalizio wa mfumo wa mambo” wanakaribishwa wairithi milki ya kidunia ya huo Ufalme. (Yohana 10:11, 16; Mathayo 24:3, NW; 25:31-46) Wataokolewa wakiwa hai wakati wale malaika wa mbinguni watakapoziachilia pepo za “dhiki ile iliyo kuu” juu ya dunia yetu. Je! wewe wataka kuwa mmoja wa huo “mkutano mkubwa” wa waokokaji wakati ufalme wa Mungu ‘utakapokuja’ kuyaponda-ponda mataifa yenye uovu? Huenda ukawa! Maana, ukiwa mshika-ukamilifu, wewe pia unaweza kuthibitisha kwamba njia ya Mungu pekee inaweza kukuongoza ufurahie uzima milele.—Ufunuo 7:1-3, 9, 13, 14.

18. (a) Sababu gani haitakuwa lazima Lena kamwe kuondolea enzi kuu ya Yehova lawama? (b) Ni nani sasa walio na tumaini lenye kung’aa? (Zaburi 37:11. 29)

18 Ufalme wa Mungu utakapokwisha kuponda-ponda Shetani na mfumo wake wa mambo machafu, haitakuwa lazima tena kabisa kuondolea enzi kuu ya Mungu lawama. Masuala yaliyotokezwa na yule Shetani mwasi yatakuwa yamejibiwa mara moja kwa wakati wote. (Nahumu 1:9) Apa hapa, penye dunia hii, ule uhalali, ule uadilifu, ule ubora wa utawala wenye kutegemea sheria ya Mungu ya upendo, utakuwa umethibitishwa, na ule Ufalme utakuwa ‘umekuja’ kulitakasa lile jina tukufu sana la Yehova Bwana Mwenye Enzi Kuu. Loo! ufalme wa Mungu unawatolea tumaini lenye kung’aa kama nini wale wa ‘viumbe vinavyougua’ wanaomtumikia Mungu sasa kwa kushika ukamilifu! Je! wewe unasali kwa bidii nyingi ufalme huo “uje”?—Warumi 8:22-25.

[Sanduku katika ukurasa wa 44]

SABABU GANI MUNGU AMERUHUSU UOVU KWA MUDA MREFU SANA?

• Ili athibitishe uhalali, uadilifu, ubora na udumu wa enzi kuu ya Yehova ya ulimwengu mzima

• Ili aonyeshe kwa wakati wote kwamba kila aina ya utawala wa mwanadamu usiomtegemea Mungu unaongoza kwenye huzuni na msiba tu

• Hi kuandalia ukuzi wa ahadi za Ufalme wa Mungu na kuchaguliwa na kujaribiwa kwa warithi wa Ufalme

• Ili kuruhusu wakati wa kuthibitisha, kama katika mahakama, kwamba watumishi wa Mungu wanaweza kushika ukamilifu lijapokuja kila jaribu kutoka kwa Shetani

• lli kuonyesha kwamba utii, unaotegemea sheria ya Mungu ya upendo, ndio mwendo pekee unaoongoza kwenye kufurahia uzima milele

• Ili kujibu kikamilifu sana shtaka la Shetani na kuweka kifano hicho halali kilicho wazi kwamba kamwe kamwe haitakuwa lazima tena kuondolea jina na enzi kuu ya Yehova lawama.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki