Vyeo vya Kuchaguliwa kwa Kura
Katika shule nyingi, wanafunzi wanapigiwa kura ya kuinua mikono ili wawe na cheo kama cha msimamizi wa darasa. Shule fulani fulani zinafanya kampeni ndogo za kisiasa, kutia na matangazo ya kuweka vikaratasi kwenye kuta ili kutangaza wagombea uchaguzi. Kusudi la kufanya hivyo ni kufahamisha vijana mpango mzima wa siasa. Lakini, vijana-Mashahidi hawajichanganyi katika siasa za shule, ama kukubali cheo cha kuchaguliwa ama kupigia kura wengine wawe na cheo. Hivyo ikiwa wanawekwa au kuchaguliwa wawe na cheo, wanakataa kwa busara. Kwa njia hiyo wanafuata mfano wa Yesu aliyeondoka wakati watu walipotaka wamfanye kuwa mfalme.—Yohana 6:15.
Lakini, sisi tunaona kuwekwa na mwalimu kuwa jambo tofauti. Hivyo ikiwa vijana-Mashahidi wanawekwa wasaidie kuelekeza magari au shughuli nyingine kama hiyo, wanatiwa moyo washirikiane kwa kadiri wawezavyo.
Bila shaka, watoto wetu wanajua si kura zote ambazo ni za kisiasa. Mara nyingine wanafunzi wanaombwa na mwalimu watoe kauli zao. Huenda kusiwe kuvunjwa kwa kanuni za Biblia mtu kusema shughuli fulani fulani anazopendelea au kutoa maneno ya kusifu hotuba au mtungo fulani mzuri wa habari. Watu wanapoonyesha kauli zao kwa kuinua mikono ili kuonyesha ubora wa jambo fulani, ni tofauti na kuchagua mtu mwingine kwenye cheo cha kisiasa.
[Blabu katika ukurasa wa 23]
Vijana-Mashahidi hawajichanganyi katika siasa za shule