Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • su sura 17 kur. 129-137
  • Mwelekeo Tofauti Juu ya Utii

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mwelekeo Tofauti Juu ya Utii
  • Kuokolewa Kuingia Katika Dunia Mpya
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • SABABU HUENDA ISIWE RAHISI KUTII
  • AMRI ZINAZOTUFAIDI SISI
  • Alitaka Kusaidia
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
  • Shujaa na Msichana Mdogo
    Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
  • “Jifungeni Unyenyekevu”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Alikuwa Mkaidi Lakini Mwishowe Alitii
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
Pata Habari Zaidi
Kuokolewa Kuingia Katika Dunia Mpya
su sura 17 kur. 129-137

Sura 17

Mwelekeo Tofauti Juu ya Utii

1. Kwa nini Yehova aliruhusu Wababuloni waharibu Yerusalemu?

KWA MIAKA mingi kabla Yerusalemu haujaharibiwa na Wababuloni, Yehova aliwaonya Wayahudi juu ya jambo lililokuwa linakuja, na sababu ya hilo. Walikuwa wakifuata maelekeo ya mioyo migumu yao wenyewe badala ya kumtii Mungu.—Yeremia 25:8, 9; 7:24-28.

2. (a) Kwa kiasi, ni faida gani zinazotegemea kumtii Mungu? (b) Waisraeli walikuja kuwaje katika uhusiano wa agano pamoja na Yehova?

2 Yehova halazimishi mtu amtumikie, lakini, bila kudai mengi, yeye anataka utii wa wote wanaotaka kibali yake na baraka za uzima zinazoenda pamoja na utii. Alipokwisha kukomboa Waisraeli kutoka Misri, Yehova aliwaambia hivi: “Ikiwa mtaitii sauti yangu kweli kweli, na kulishika agano langu, hapo ndipo mtakapokuwa tunu kwangu kuliko makabila yote ya watu; maana dunia yote pia ni mali yangu, nanyi mtakuwa kwangu ufalme wa makuhani, na taifa takatifu.” (Kutoka 19:5, 6) Mungu alipokuwa amekwisha kuwaambia matakwa yake, nao walipokuwa wamekwisha kusikia kusomwa kwa “kitabu cha agano,” kwa hiari yao wenyewe walilikubali daraka lililofuatana na uhusiano huo pamoja na Mungu.—Kutoka 24:7.

3. (a) Ni kwa njia zipi baada ya hapo Waisraeli walionyesha roho ya uasi kuelekea Yehova? (b) Kwa nini matukio hayo yameandikwa katika Biblia?

3 Ingawa hivyo, baada ya muda mfupi tu roho ya uasi ikaanza kujitokeza. Wana wa Israeli hawakukana imani yao katika Yehova waziwazi; lakini, kwa kuvunja sheria yake, wengi walijaribu kuchanganya mazoea ya Kimisri pamoja na ibada ya Yehova. (Kutoka 32:1-8) Baadaye baadhi yao wakalaumu wanaume ambao Yehova alikuwa akitumia kuwa wawakilishi wake waonekanao. (Hesabu 12:1-10; 16:1-3, 31-35) Wakiwa taifa, Waisraeli walionyesha kukosa imani ya kufuata neno la Mungu, wakiongozwa na woga wa mwanadamu. (Hesabu 13:2, 31-33; 14:1-4; Waebrania 3:17-19) Wakati makosa hayakufanywa kwa kukusudiwa, wale waliotubu kwa unyenyekevu wangeweza kupata msamaha. Lakini kwa kipindi cha zaidi ya karne tisa taifa hilo likapungukiwa kimakusudi tu kwanza takwa moja la kimungu, kisha jingine, na mara nyingi mengi ya matakwa hayo. Mambo waliyofanya na matokeo ya kuyafanya yameandikwa katika Biblia yawe mifano ya kutuonya sisi.—2 Mambo ya Nyakati 36:15-17; 1 Wakorintho 10:6-11.

4. (a) Warekabi walikuwa akina nani? (b) Ni wajibu gani ambao Yehonadabu alikuwa amewawekea?

4 Katika siku za Yeremia, baada ya maonyo kutolewa mara nyingi juu ya matokeo mabaya ya mwendo wao, Yehova akaweka mbele ya Wayahudi mfano—Warekabi. Hao hawakuwa Waisraeli, walikuwa wazao wa Yehonadabu aliyekuwa ameonyesha kwamba alikuwa katika upatani kamili na kutovumilia kwa Yehu ushindani kuelekea Yehova. Yehonadabu (au Yonadabu) huyo akiwa mzee wa kichwa cha kabila la Warekabi, alikuwa amewaamuru washike mwiko wa kunywa divai kwa wakati usiojulikana, pia wasiishi katika nyumba wala kulima mashamba bali wakae katika mahema kama wahamaji. Kwa njia hiyo wangeishi maisha ya kiasi, yasiyo na mambo mengi, pasipo kujitafutia anasa na maovu ya maisha ya mjini, huku wakimwabudu Yehova pamoja na Waisraeli, ambao miongoni mwao waliishi.

5. Warekabi walikuwaje mfano mzuri wa kutii?

5 Kwa kuwa Wayahudi walikuwa wakikataa kumsikiliza Yehova, Mwenye Enzi Kuu ya Ulimwengu Mzima, je! ingeweza kutazamiwa kwamba Warekabi wangetii babu yao wa kibinadamu? Walimtii, tena kwa njia iliyo mfano mzuri. Ijapokuwa Warekabi walitafuta kimbilio katika Yerusalemu wakati majeshi ya vita ya Kibabuloni na ya Kishami yalipovamia Yuda, wao waliendelea kukaa katika mahema. Lakini azimio lao la kutogusa divai lilikuwa imara kadiri gani, hata ijapo watu ambao wao waliishi miongoni mwao waliruhusiwa kuinywa? Yehova alimwagiza Yeremia awaingize Warekabi hao katika chumba cha hekalu cha kulia chakula, akaandaa vikombe vya divai na kuwaalika wanywe. Walikataa. Kwa nini? Inaonekana wazi kwamba walithamini kujitoa kwa babu yao kwa Yehova, walifahamu jinsi alivyohangaikia kwa upendo hali njema yao, hivyo wakatii amri yake. Yehova alipendezwa na mfano mzuri huo wa utii ulioonyesha ukosefu wa kumtii Yehova ambao Wayahudi walidhihirisha.—Yeremia 35:1-11.

6. (a) Ni nani leo walio kama Warekabi? (b) Ni nani ambaye amechukua mfano wa Waisraeli wasiotii?

6 Leo kuna watu walio kama Warekabi hao. Hao ni “kondoo wengine” wa Bwana. Wawe watakunywa divai au hawatakunywa, hilo si kitu leo. (Linganisha 1 Timotheo 5:23.) Hilo ni shauri la mtu binafsi kuamua mradi hawawi wanywaji wa kupindukia au labda walevi. (Mithali 23:20; 1 Wakorintho 6:9, 10) Lakini utii wa kimungu ni wa maana sana. Tofauti na Jumuiya ya Wakristo, inayochukua mfano wa Israeli mwasi-imani, jamii ya Warekabi wa kisasa inaonyesha kwa vitendo vyao kwamba wanaujua ubora wa utii wa kimungu. Hilo litawafaidi namna gani?

7. (a) Ni ahadi gani yenye kutia moyo ambayo Yehova aliwapa Warekabi? (b) Hiyo inatoa tumaini gani kwa jamii ya kisasa ya Warekabi?

7 Kwa sababu ya kujitoa kwao, Yehova aliwapa Warekabi ahadi iliyo na maana ya kiunabii yenye nguvu kwa wakati wetu, akisema: “Kwa sababu mmeitii amri ya Yonadabu, baba yenu, na kuyashika maagizo yake yote, na kutenda sawasawa na yote aliyowaamuru; basi, kwa sababu hiyo, [Yehova] wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi, Yonadabu, mwana wa Rekabu, hatakosa kuwa na mtu wa kusimama mbele zangu hata milele.” (Yeremia 35:18, 19) Walikuwa kati ya waokokaji wa uharibifu wa Yerusalemu mwaka wa 607 K.W.K. Na jamii inayofananishwa nao itauokoka uharibifu unaokuja wa Jumuiya ya Wakristo na sehemu nyingine yote ya ulimwengu unaofuata njia zake kwa kujitegemea wenyewe, ukikataa kukubali enzi kuu ya Yehova.

SABABU HUENDA ISIWE RAHISI KUTII

8. Kwa nini watu wengi wanaona ni vigumu kutii?

8 Watu wengi wanaona ni vigumu kutii. Wamekulia katika ulimwengu ambamo kila mtu anafanya kivyake. Huenda wanapenda mambo ambayo wanajifunza juu ya kuishi chini ya Ufalme wa Mungu. Lakini ikiwa kiburi kinafunika fikira zao, huenda wakachukia baadhi ya matakwa ya Mungu au wakalaumu namna matakwa hayo yanavyotolewa. (Mithali 8:13; 16:18) Naamani, mkuu wa jeshi la Kishami (Siria) siku za nabii Elisha, alikuwa na tatizo hilo.

9. (a) Ilitokeaje kwamba Naamani akaenda kumwona Elisha? (b) Alitazamia nini, lakini hasa ni jambo gani lililotukia?

9 Naamani alisumbuliwa na ukoma. Lakini kwa sababu mateka mchanga, msichana Mwisraeli, alionyesha imani yake kwa ujasiri kwa kusema kwamba kama Naamani angemwendea Elisha nabii wa Yehova, angeponeshwa, Naamani akafunga safari kwenda Israeli. Akiwa na farasi na magari ya vita akaenda mpaka kwenye nyumba ya Elisha. Basi, Naamani alikuwa mtu mwenye cheo kikubwa na alitazamia Elisha atoke kuja kumlaki kisha afanye sherehe, amwombe Yehova na kusukasuka mkono huku na huku juu ya mwili wenye ugonjwa mpaka aponeshwe. Badala ya kufanya hivyo, Elisha alituma tu mjumbe akamwambie aende kwenye Mto Yordani na kuoga huko mara saba.—2 Wafalme 5:1-12.

10. (a) Naamani alitendaje? (b) Hatimaye ni kitu gani kilichomwongoza atii? (c) Matokeo yalikuwa nini?

10 Fahari ya Naamani ilishushwa. Akaondoka kwa hasira sana. Lakini watumishi wake walipozungumza naye wakimpa sababu, akajinyenyekeza akiwa na imani. “Ndipo akashuka, akajichovya mara saba katika Yordani, sawasawa na neno lake yule mtu wa Mungu; nayo nyama ya mwili wake ikarudi ikawa kama nyama ya mwili wa mtoto mchanga, akawa safi.” Naamani akasadikishwa kwamba Yehova ndiye Mungu pekee wa kweli, akafahamu kwamba yale maelekezo aliyopewa na Elisha yalitoka kwa Mungu kweli kweli, ingawa hapo mwanzo alitenda tofauti.—2 Wafalme 5:13-15.

11. (a) Ni kwa njia zipi “kondoo wengine” walifananishwa na Naamani? (b) Ni somo gani la maana ambalo ni lazima sote tujifunze?

11 Je! labda wewe unajiona una baadhi ya tabia za Naamani? Kama wengine wasio Waisraeli waliozoea imani, Naamani anatumiwa katika Maandiko kufananisha “kondoo wengine” wanaojiunga katika ibada ya kweli. Wote hao, wakiwa wamezaliwa katika dhambi, wakati mmoja walikuwa wagonjwa kiroho. Wote walilazimika kutafuta msaada wa jamii ya mtumishi-mpakwa-mafuta wa Yehova kisha wakafuata kwa utii yale ambayo “mtumwa” huyo amewafundisha katika Neno la Mungu. (Mathayo 24:45-47) Wakati mmoja wengine hawakuthamini shauri lote la Kimaandiko walilopewa—kama vile uhitaji wa kuhudhuria kwa ukawaida mikutano ya kundi, umaana wa kujitenga na ulimwengu au wa ubatizo wa Kikristo katika maji. Labda walisita kujiweka wakfu na kubatizwa katika maji kwa sababu moyo wao ulipinga uhitaji wa ‘kujikana’ ili kuwa mfuasi wa Kristo. Katika visa fulani walilaumu namna shauri lilivyotolewa kwao na wenye madaraka katika kundi. Lakini baadaye wote ambao wangekuwa “kondoo wengine” kweli kweli wa bwana wamehitaji kujifunza umaana wa unyenyekevu na utii wa upendo.—Yakobo 4:6; Mathayo 16:24.

AMRI ZINAZOTUFAIDI SISI

12, 13. (a) Kwa nini kutii amri za Yehova kunatufaidi sisi? (b) Hilo laweza kuonyeshwaje mfano?

12 Tunapopata kumjua Yehova na njia zake, tunapata kuthamini jinsi yalivyo ya kweli maneno aliyoambia watumishi wake nyakati za zamani: “Mimi ni [Yehova], Mungu wako, nikufundishaye ili upate faida, nikuongozaye kwa njia ikupasayo kuifuata. Laiti ungalisikiliza amri zangu!” (Isaya 48:17, 18) Yehova anatamani sana watu wake waepuke msiba wafurahie uzima kwa kusikiliza amri zake. Yeye anajua jinsi tulivyoumbwa na kitakachotuletea furaha ya kweli kweli. Anatuonya juu ya mwenendo ambao ungeweza kutushushia heshima au kuharibu uhusiano wetu pamoja na wengine.

13 Wale ambao wametii maonyo yake juu ya uasherati na uzinzi wameepushwa na hangaiko la moyo, magonjwa na kuzaa watoto haramu wanaotokana na uasherati na uzinzi. (1 Wakorintho 6:18; Waebrania 13:4) Kwa kufuata shauri kama lile katika 2 Wakorintho 7:1, wameepuka mazoea mabaya ya kuvuta tumbaku na dawa nyingine za kulevya, zinazoharibu afya ya mtu na zinazoweza kutokeza kifo cha mapema. Amri yake ya ‘kujiepusha na damu’ imesaidia watumishi wake watie nguvu tegemeo lao kwake kuwa Ndiye juu yake matazamio yao yote ya uzima wa wakati ujao yanakaa, na wakati uo huo imewalinda juu ya magonjwa yenye kuogopesha yanayoweza kuenezwa kwa kutiwa damu mishipani.—Matendo 15:28, 29.

14. Tunafaidikaje kwa kutafuta kwanza Ufalme badala ya kujihusisha wenyewe bure na ulimwengu?

14 Muda tunaokuwa katika ulimwengu, ni lazima tuwe na uhusiano wa kadiri fulani nao. Lakini Yehova anatuonya tusiweke matumaini yetu juu ya ulimwengu, tusiwe sehemu yao. Yeye anajua yatakayoupata ulimwengu wakati ujao. Ingekuwa upumbavu kama nini mtu kutumia maisha yake awe akijenga kile ambacho Mungu atabomoa! Na bado lililo baya zaidi ni kwamba, wale wanaofanya hivyo watakuja kuona kwamba watapatwa na msiba ule ule utakaoupata ulimwengu ambao wametolea maisha zao. Kwa hiyo, ni lenye faida kama nini shauri alilotoa Mwana wa Mungu: Tafuta Ufalme wa Mungu! Uweke kwanza katika maisha yako!—1 Yohana 2:17; Mathayo 6:33.

15. (a) Ili tuwe miongoni mwa wale watakaopata tena alichopoteza Adamu, ni lazima tujifunze kufanya nini? (b) Yehova atasema na sisi namna gani wakati wa Miaka Elfu?

15 Kwa kujua sana tunachohitaji, Yehova anatayarisha watu wake waje waishi katika mfumo wa mambo wake mpya wenye uadilifu. Kutokutii kwa Adamu kuliongoza kwenye kutokamilika kwa kibinadamu, kupoteza uzima wa milele na kufukuzwa katika Paradiso. Bila shaka ikiwa tutakuwa kati ya wale watakaobarikiwa wapewe kile alichopoteza Adamu, ni lazima tutoe ushahidi wa kwamba tunasikiliza wakati Mungu anaposema. Na atasema na sisi namna gani wakati wa Miaka Elfu inayokuja, wakati wanadamu watakapokuwa wakikamilishwa? Ni kupitia Ufalme wa Kimasihi. Je! serikali hiyo pia itakuwa na wawakilishi wa kidunia wenye kuonekana? Ndiyo. Mfalme atatumikiwa na “wana-wafalme katika dunia yote.” (Zaburi 45:16, New World Translation; linganisha Isaya 32:1, 2.) Kwa kuwatii kwa upendo wana-wafalme hao, wanadamu wataonyesha utii kwa Mfalme wao wa kimbingu.

16. Kwa nini kutii wazee ni ulinzi sasa, na ni tayarisho zuri namna gani la kuishi katika Utaratibu Mpya wa Mungu?

16 Ili atutayarishe kwa ajili ya wakati huo, sasa Yehova anatoa mazoezi kupitia tengenezo la kitheokrasi lake linaloonekana. Ametokeza katika makundi wanaume wazee kiroho. Wanatoa usimamizi unaohitajiwa kwa mikutano ya kundi na wanaongoza katika kazi ya kuhubiri ujumbe wa Ufalme. Wanasaidia wote wanaotaka kumtumikia Yehova wajifunze jinsi ya kutumia kanuni za Biblia maishani mwao na kwa upendo wanaonya juu ya mitego ambayo ingeweza kuharibia mtu uhusiano wake pamoja na Mungu. Mashahidi wa Yehova ulimwenguni pote wamejua pia kwamba kufuata maelekezo ya wazee kunatokeza mara nyingi kuhifadhiwa kwa uhai wakati wa tufani, matetemeko ya ardhi na kutokea kwa jeuri ya kutumia silaha. Kundi si mali ya wazee; ni mali ya Mungu. Wazee hawajidai kuwa wasioweza kukosea. Lakini, kama Maandiko yanavyoonyesha, Mungu anawatumia ili waongoze, na kuwatii wao kunaonyesha kuheshimu mpango ambao Yehova anatumia ili kutayarisha watumishi wake waje waokoke na kuingia katika Utaratibu Mpya.—Matendo 20:28; Waebrania 13:17.

17. Kichocheo chetu cha kutii chapasa kuwa nini?

17 Ingawa hivyo, utii huo hauchochewi na tamaa tu ya kuja kuwa miongoni mwa waokokaji wa uharibifu unaokuja wa ulimwengu. Kuna zaidi ya hilo. Ni nini? Ni kuthamini uhai na maandalizi yote ambayo Mungu amefanya ili auendeleze. Shukrani kwa zawadi zinazotajirisha maisha zetu—uwezo wa kufikiri, kuthamini uzuri na mambo bora ya kiroho, uwezo wa kujua na kuabudu Muumba wetu. Pia, kuujua ule upendo mkubwa wa Mungu mwenyewe uliomwongoza amtoe Mwanaye mwenyewe atutolee uhai wake iwe dhabihu ili sisi tuweze kuwa na nafasi ya kuishi milele.

18. Tunapopata kumjua Mungu sana, tunakuwa na maoni gani juu yake yeye na tengenezo lake?

18 Wale ambao wamemjua Mungu sana, hawaoni utii kuwa jambo lisilopendeza ambalo mtu analazimika kufanya. Ufahamu sahihi wa makusudi na matakwa yake, pamoja na kuona matokeo mazuri ya kufuata hayo, hauachi shaka katika akili zao kwamba kutenda kwa njia anayotaka Mungu ndio mwendo wa busara na wa akili peke yake. Wanatambua kwamba ni ulinzi. Pia ni njia ya kumwonyesha Mungu upendo wao. Wanapata furaha kubwa ya kumtii.—1 Yohana 5:3; Zaburi 119:129.

[Picha katika ukurasa wa 135]

Watu fulani wanahitaji kushinda kiburi, kama Naamani mkoma alivyofanya

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki