Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • su sura 23 kur. 175-182
  • “Mna Haja ya Uvumilivu”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Mna Haja ya Uvumilivu”
  • Kuokolewa Kuingia Katika Dunia Mpya
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • WAKRISTO WAMEPASWA WATENDE NAMNA GANI?
  • ‘WENYE FURAHA NI WALE WANAOENDELEA KUVUMILIA’
  • Mthawabishaji wa Wote Wanaomtumikia
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Mtumikie “Mfalme wa Mataifa” Ukaokoke
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
  • Kuvumilia Kwa Uaminifu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
  • Ebed-meleki​—Mfano wa Ujasiri na Fadhili
    Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2017
Pata Habari Zaidi
Kuokolewa Kuingia Katika Dunia Mpya
su sura 23 kur. 175-182

Sura 23

“Mna Haja ya Uvumilivu”

1. (a) Kwa nini Mashahidi wa Yehova ni wenye furaha kweli kweli? (b) Lakini ni shauri gani katika Waebrania 10:36 linalotuhusu sote?

WALE ambao wamemfanya Yehova kuwa uhakika wao ndio watu wenye furaha kweli kweli kuliko wengine duniani leo. Wanajua mahali linapoweza kupatikana shauri lililo bora zaidi sana juu ya kushughulika na matatizo ya maisha. Lapatikana katika Neno la Mungu mwenyewe. Wao hawaogopi wanapotazamia wakati ujao, kwa sababu wanajua ni nini kusudi la Mungu kwa dunia hii. (Yeremia 17:7, 8; Zaburi 46:1, 2) Ingawa hivyo, mtume Paulo aliandikia Wakristo wenzake hivi: “Mna haja ya uvumilivu, ili, mkiisha kuyafanya mapenzi ya Mungu, mpate kupokea utimizo wa ahadi.” (Waebrania 10:36, New World Translation) Ni nini kinachofanya kuwe na uhitaji huo wa uvumilivu?

2. Kwa nini wanafunzi wa Yesu wangehitaji uvumilivu?

2 Kabla ya kufa kwake mwenyewe, Yesu aliwaonya mitume wake juu ya mambo yaliyokuwa mbele yao, akisema: “Kama mngalikuwa sehemu ya ulimwengu, ulimwengu ungalikipenda kilicho chake wenyewe. Sasa kwa sababu ninyi si sehemu ya ulimwengu, bali mimi niliwachagua katika ulimwengu, kwa sababu hii ulimwengu unawachukia ninyi. Kumbukeni neno nililosema kwenu, Mtumwa si mkubwa kuliko bwana mkubwa wake. Ikiwa wamenitesa mimi, watawatesa ninyi pia; ikiwa wameshika neno langu, watashika lenu pia. Lakini watafanya mambo yote hayo juu yenu kwa sababu ya jina langu, kwa sababu hawamjui yeye aliyenituma mimi.” (Yohana 15:19-21, New World Translation) Na hivyo ndivyo imekuwa hasa!

3. (a) Wanafunzi wa Yesu wanateswaje ‘kwa sababu ya jina lake?’ (b) Ni katika maana gani watesi “hawamjui” Yeye aliyemtuma Yesu? (c) Ni nani hasa aliye na lawama la kuchochea mateso hayo?

3 Wafuasi wa Yesu ndio watu wenye kufanyiwa uhasama kwa sababu wanaishi katikati ya ulimwengu unaokataa kinachowakilishwa na Ukristo wa kweli. Kristo maana yake “Mpakwa Mafuta.” Yesu Kristo ndiye aliyepakwa mafuta na Yehova awe Mfalme, aitawale dunia nzima. Hivyo Yesu aliposema kwamba wanafunzi wake wangeteswa ‘kwa sababu ya jina lake,’ alimaanisha kwamba mateso hayo yangekuwapo kwa sababu wanamfuata sana kuwa Mfalme wa Kimasihi wa Yehova, kwa sababu wanamtii Kristo kwanza kuliko kutii kwanza mtawala ye yote wa kidunia, kwa sababu wanaunga mkono kwa ushikamanifu Ufalme wake na hawajiingizi katika mambo ya serikali za wanadamu. Yesu aliongeza kusema kwamba wangepingwa kwa sababu watesi hao “hawamjui yeye aliyenituma mimi”—yaani, wanakataa kumkubali Yehova Mungu kuwa Mwenye Enzi Kuu ya Ulimwengu Mzima. (Linganisha Kutoka 5:2.) Aliye mchochezi mkuu wa mateso hayo ni nani? Ni Shetani Ibilisi.—Ufunuo 2:10.

4. (a) Utimizo wa Ufunuo 12:17 unahusuje maisha zetu? (b) Lengo la Shetani ni nini?

4 Mkazo juu ya Wakristo wa kweli umekuwa mwingi sana hasa tangu Shetani afukuzwe mbinguni baada ya kuzaliwa kwa Ufalme wa Kimasihi wa Mungu mwaka wa 1914. Usipunguze uzito wa mambo. Kuna vita vya kufa na kupona ambavyo Ibilisi na mashetani wake wanapiga juu ya wote ambao wamechukua msimamo wao upande wa Ufalme wa Mungu ulio mikononi mwa Yesu Kristo. Kwa habari hiyo, Ufunuo 12:17 unasema: “Joka [Shetani Ibilisi] akamkasirikia yule mwanamke [tengenezo la Mungu lililo kama mke], akaenda zake afanye vita juu ya wazao wake waliosalia [wafuasi wa Kristo wapakwa-mafuta kwa roho waliopo duniani], wazishikao amri za Mungu, na kuwa na ushuhuda wa Yesu.” “Kondoo wengine,” pia, wanajikuta katikati ya vita vikali hivyo. Kwa kutumia ujanja, Shetani anajaribu kuwashawishi au kuwalazimisha waache kutii amri za Mungu. Anataka kupunguza nguvu kisha aiharibu kabisa hali yao ya kiroho. Lengo lake ni kunyamazisha tangazo juu ya Yesu kuwa Mfalme wa Kimasihi wa Yehova. Lakini watumishi washikamanifu wa Mungu wanashinda katika vita hivyo vya kiroho.

WAKRISTO WAMEPASWA WATENDE NAMNA GANI?

5. Ni hatua gani ambazo serikali zimechukulia Mashahidi wa Yehova?

5 Wakuu wengi wa serikali wanakubali kwamba Mashahidi wa Yehova ni watu wenye kutii sheria na kwamba wana uvutano mzuri katika jumuiya ya watu. Ingawa hivyo, serikali zote za kibinadamu ni sehemu ya mfumo wa mambo ya ulimwengu wa Shetani. (1 Yohana 5:19; Ufunuo 13:2) Hivyo isije kama mshangao wakati serikali fulani zinapokataza mikutano ya wale wanaomwabudu Mungu wa kweli, zinapopiga marufuku vitabu vyao vya Biblia, zinapopiga marufuku kuhubiri kwao juu ya Ufalme wa Mungu, ndiyo, hata zinapowafunga gerezani na kuwatesa kimwili. Ikiwa wewe binafsi utapatwa na mkazo kama huo, utafanya nini?

6. (a) Imetupasa tuwe na mwelekeo gani juu ya wakuu wa serikali? (b) Lakini sisi tumeazimu kwa dhati kufanya nini? (c) Hata tujapoteswa, tunaweza kuendeleaje kuwa wenye furaha?

6 Mitume wa Yesu Kristo waliheshimu wakuu wa serikali. Walipoteswa, hawakulipa kisasi. Lakini walipoamriwa waache kufanya aliyoamuru Mungu, walijibu kwa dhati hivi: “Imetupasa kumtii Mungu kuliko wanadamu.” (Matendo 5:29; Warumi 12:19; 1 Petro 3:15) Hata maisha zao zilipotiwa hatarini, kuogopa kufa hakukuwafanya wakane imani yao. Walijua walikuwa wakimtumikia “Mungu, awafufuaye wafu.” (2 Wakorintho 1:9; Waebrania 2:14, 15) Wajapoteswa, walikuwa wenye furaha—wenye furaha kwa sababu walijua walikuwa wakimpendeza Mungu, wenye furaha kwa sababu ya kuwa na nafasi ya kushiriki kuliondolea jina lake malawama na kumthibitishia Mfalme wake mpakwa-mafuta ushikamanifu wao. (Matendo 5:41, 42; Mathayo 5:11, 12) Je! wewe ni mtu wa aina hiyo? Je! wewe unajitambulisha waziwazi kuwa upande wa wale wanaoteswa hivyo? Ebedmeleki alikuwa mtu ambaye hakusita kwa kuogopa. Alikuwa nani?

7. (a) Ebedmeleki alikuwa nani, na kwa nini tunapendezwa naye sasa? (b) Aliposikia kwamba Yeremia alikuwa ametupwa katika kisima chenye matope, ni hatua gani ambayo Ebedmeleki alichukua, na kwa nini?

7 Ebedmeleki alikuwa Mwethiopia mwenye kuogopa Mungu na alikuwa akiishi Yerusalemu wakati wa kipindi kilichotangulia kuharibiwa kwao na Wababuloni. Aliajiriwa kazi katika nyumba ya Mfalme Sedekia. Wakati huo Yeremia alikuwa akitumikia akiwa nabii wa Yehova kwa Ufalme wa Yuda na mataifa yaliyozunguka. Kwa sababu yeye alitoa ujumbe wa Mungu wa kuonya pasipo kuyumbayumba, akawa mtu wa kuteswa sana. Kwa uchochezi wa wana-wafalme fulani katika Yerusalemu, yeye hata alitupwa katika kisima ili azame katika matope afie humo. Ijapokuwa Ebedmeleki hakuwa Mwisraeli, yeye alimkubali Yeremia kuwa nabii wa Yehova. Aliposikia yaliyokuwa yamefanywa, bila kukawia Ebedmeleki alimwendea mfalme kwenye lango la mji ili amtetee Yeremia. Kwa kufuata amri ya mfalme, akachukua upesi wanaume 30, pia kamba na nguo kuukuu. Akamwelekeza Yeremia atie nguo kuukuu makwapani ili asiumizwe na kamba, kisha wakamwinua nabii huyo kutoka kisimani.—Yeremia 38:4-13.

8. Ni ahadi gani yenye kutumainisha ambayo Yehova alimpelekea Ebedmeleki, na kwa nini?

8 Kwa wazi Ebedmeleki alikuwa na wasiwasi kwa sababu ya jambo ambalo wana-wafalme wangemtendea kwa kuzuia mpango wao mbaya, lakini kuheshimu nabii wa Yehova na kumtumainia Mungu kulishinda hangaiko lake. Kwa sababu hiyo, Yehova alimhakikishia Ebedmeleki hivi kupitia Yeremia: “Tazama, nitaupatiliza mji huu maneno yangu kwa mabaya, wala si kwa mema; nayo yatatimizwa mbele yako katika siku hiyo. Lakini nitakuokoa wewe katika siku hiyo, asema [Yehova]; wala hutatiwa katika mikono ya watu wale unaowaogopa. Kwa maana ni yakini, nitakuokoa, wala hutaanguka kwa upanga, lakini nafsi yako itakuwa kama nyara kwako; kwa kuwa ulinitumaini mimi, asema [Yehova].”—Yeremia 39:16-18.

9. (a) “Kondoo wengine” wamekuwaje kama Ebedmeleki? (b) Hivyo, ahadi ambayo Yehova alimpa Ebedmeleki ina maana gani kwa “kondoo wengine” leo?

9 Lo! ahadi hiyo ni yenye maana sana kama nini kwa watumishi wa Yehova leo! Kama Ebedmeleki, “kondoo wengine” wanaona jamii ya kisasa ya Yeremia, mabaki wapakwa-mafuta wakitendwa mambo yasiyo ya haki, na jitihada zinazofanywa ili kuzuia kuhubiri kwao ujumbe wa Yehova. Hawakusita kuchukua hatua yo yote ambayo wangeweza kuchukua ili walinde na kuunga mkono jamii ya wapakwa-mafuta. Kwa hiyo, kwa kufaa ahadi ambayo Yehova alimpa Ebedmeleki inawatia nguvu, inakaza uhakika wao kwamba Mungu hataruhusu wapinzani wawaangamize bali Yeye atawahifadhi wakiwa jamii katika maangamizi ya ulimwengu yanayokaribia sana waingie katika “dunia mpya” Yake yenye uadilifu.

10. Ni katika sehemu gani za maisha ambazo Wakristo wanateswa?

10 Si wote wanaotembea katika hatua za Yesu Kristo wamo katika hatari ya kufungwa gerezani, lakini wote wanateswa kwa njia hii au hii. (2 Timotheo 3:12) Maelfu ya wake wa Kikristo, na waume, wamevumilia kwa uaminifu upinzani mkubwa mle mle nyumbani mwao wenyewe kwa miaka mingi. Watoto, pia, kwa sababu ya tamaa yao ya kumtumikia Yehova, wamekanwa na wazazi wao. (Mathayo 10:36-38) Huenda vijana Wakristo pia wakapata mateso shuleni; watu wazima, mahali pao pa kazi. Mashahidi wa Yehova wote wanaonja mateso fulani wanaposhiriki kutoa ushuhuda waziwazi juu ya Ufalme wa Mungu. Maneno haya ya Yesu, yanawahusu hao wote: “Kwa uvumilivu upande wenu mtajipatia nafsi zenu.”—Luka 21:19, New World Translation.

11. (a) Ni hali gani nyingine zinazotokeza jaribu kwa wengi? (b) Nani mwingine alipatwa na mambo hayo, na kwa sababu gani?

11 Kuna hali nyingine zinazojaribu wengi. Huenda wakawa na ugonjwa mahututi, unaoondolea maisha furaha nyingi. Au, labda wanapatwa na hali ngumu sana za kiuchumi. Huenda ikawa kwamba, mara nyingine, maneno ya wenzi wao wa karibu si mazuri na si ya fadhili. Kwa habari ya Ayubu, Shetani alitumia njia zote hizo kwa kujitahidi kuvunja ukamilifu wake. Sisi tutatendaje tukijikuta tumo katika hali kama hizo?—Yakobo 5:11.

12. (a) Kwa nini Noa hasa alihitaji uvumilivu katika huduma yake? (b) Hali imefananaje na hiyo wakati wetu?

12 Kwa upande mwingine, namna gani ikiwa sisi binafsi tunaona jitihada zetu za kutoa ushuhuda juu ya makusudi ya Yehova haziitikiwi vizuri sana? Hilo, pia, ni jambo linalotaka uvumilivu. Kumbuka, miaka yote ambayo Noa alihubiri kabla ya Gharika, ni mke na wanaye na wake zao tu waliojiunga naye katika kumtumikia Yehova. Wengine wote kati ya wanadamu “hawakujali.” (Mathayo 24:39, NW) Hali moja na hiyo, leo, walio wengi ‘hawajali.’ Ingawa hivyo, katika sehemu fulani ambamo wakati mmoja itikio zuri kwa ujumbe wa Ufalme lilikuwa dogo sana, sasa kuna mavuno mengi ya waabudu wa Mungu wa kweli. Wenye furaha ni wale ambao wamevumilia miaka yenye ubaridi au upinzani wa wazi na sasa wanashiriki mkusanyo huo ulio bora!

‘WENYE FURAHA NI WALE WANAOENDELEA KUVUMILIA’

13. (a) Ili tuendelee kuvumilia, ni lazima tuendelee kuweka kitu gani wazi sana mbele yetu? (b) Ni nini tunachohitaji kutambua juu ya mbinu za Shetani?

13 Ili kuepuka kukosa tazamio zuri ajabu la kuishi katika “dunia mpya,” ni lazima kuendelea kulifanya liwe wazi sana mbele yetu lile suala kuu linalokabili uumbaji wote—suala la enzi kuu ya ulimwengu mzima. Je! sisi tuko upande wa Yehova bila kuyumbayumba? Je! tunafahamu kwamba kuna pande mbili tu, kwamba hakuna hali ya kuwa katikati? Ikiwa hatutaangamizwa katika vita hiyo, tunahitaji kutambua kwamba uhasama na vishawishi ni mbinu anazotumia Shetani ili avunje ukamilifu wetu, atufanye tuache kumtii Mungu, tuiache kazi ya lazima ya kutoa ushuhuda wa Ufalme wa Kimasihi.—1 Petro 5:8, 9; Marko 4:17-19.

14. (a) Ni lazima tusitawishe uhusiano gani, pamoja na nani? (b) Atatusaidiaje?

14 Ni lazima pia tusitawishe hali ya kumtegemea kabisa Yehova. Ungekuwa upumbavu kama nini kujaribu kuepuka mitego hiyo ya werevu ya adui asiye wa kibinadamu kwa kutegemea nguvu zetu wenyewe! Lakini tukimtumaini Yehova kwa moyo wetu wote, ndipo tutakapomkaribia zaidi tupatapo shida na kukabili kishawishi. (Waefeso 6:10, 11; Mithali 3:5, 6) Yehova hatulazimishi tuingie katika njia fulani. Yeye hatatuongoza kinyume cha kupenda kwetu. Lakini tukifuata Neno lake kuwa mwongozo, tukiomba kwa sala atupe nguvu na kuendelea kuwa karibu sana na tengenezo lake, ataelekeza hatua zetu. Naye atatukaza kwa kuwa na ushahidi uliofanywa upya wa upendo wake mwenyewe usioshindwa.—Warumi 8:38, 39.

15. (a) Ni nani anayepaswa kuwa wa kwanza katika maisha zetu? (b) Tuzioneje hali zinazojaribu imani yetu?

15 Shida na vishawishi unavyopata vinakujaribu wewe. Ni nani unayeweka kuwa wa kwanza katika maisha yako? Shetani anapinga akisema kwamba sote tunahangaikia nafsi yetu. Watu wengi wako hivyo. Yesu Kristo alikuwa tofauti. Wewe uko tofauti? Je! umejifunza kuweka kutukuzwa kwa jina la Yehova kuwa ndilo jambo la kwanza? Ikiwa ndivyo, basi, badala ya kuepa hali zinazojaribu imani yako, utakuwa na uwezo wa kuzikabili kabisa, ukimwomba kwa sala Yehova akupe hekima ya kuzitumia hali hizo ili umheshimu. Dhiki unayopata sasa itafanyiza uvumilivu; nao uvumilivu kwa sababu unampenda Yehova utaleta kibali yake. “Mwenye furaha ni mtu wa kiume anayeendelea kuvumilia jaribu, kwa sababu akiisha kukubaliwa atapokea taji la uzima, ambalo Yehova aliwaahidi wale wanaoendelea kumpenda.”—Yakobo 1:2-4, 12; Warumi 5:3, 4, New World Translation.

16. Ni mradi gani ambao imetupasa tuwe tukijitahidi kufikia?

16 Haitoshi kuanza utumishi wa Yehova au kuvumilia kwa muda mfupi tu. Tumo katika mashindano ya mbio, na wanaopata tuzo ni wale wanaouvuka mstari wa mwisho. Watakaokuwa wenye furaha ni wale ambao bado wanajitahidi wakiwa wamekaza sana macho yao kwenye tuzo wakati huu mfumo wa kale utakapoanguka! Lo! wana akiba ya tazamio tukufu wakati huo kama nini!—Waebrania 12:1-3; Mathayo 24:13.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki